GE2025 Polisi: Polepole afike Ofisi ya Mpelelezi wa Makosa ya Jinai ili kuthibitisha Tuhuma anazozitoa

GE2025 Polisi: Polepole afike Ofisi ya Mpelelezi wa Makosa ya Jinai ili kuthibitisha Tuhuma anazozitoa

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Wild Flower

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2023
Posts
844
Reaction score
1,606

Jeshi la Polisi limemwelekeza aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey Polepole afike katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) atoe maelezo na ushahidi kuhusiana na tuhuma ambazo amekuwa akizitoa kupitia mitandao ya kijamii. Jeshi hilo limesema mbali na kukusanya ushahidi, limekuwa likifanya jitihada za kumpata ili aweze kutoa maelezo na vielelezo vitakavyothibitisha tuhuma hizo ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa.

Soma majibu ya Polepole kwa Polisi: Polepole: Jeshi la Polisi hamjafanya juhudi zozote za kunitafuta| Mawasiliano yangu rasmi yanajulikana

===

Leo Septemba 15, 2025 Jeshi la Polisi limetoa taarifa kuwa lilifungua jalada la uchunguzi na linaendelea kuchunguza tuhuma mbalimbali ambazo amekuwa akitoa Humphrey Herson Polepole toka Julai 2025.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo Jeshi limesema Polepole amekuwa akitoa tuhuma hizo Tuhuma hizo kupitia mitandao ya Kijamii. Baada ya kufungua jalada na kuanza uchunguzi, Jeshi la Polisi mbali na kukusanya ushahidi, limekuwa likifanya jitihada za kumpata ili aweze kutoa maelezo/ushahidi na vilelezo vitakavyo thibitisha tuhuma hizo ili kuwezesha hatua zingine za kisheria ziweze kuchukuliwa kwa mujibu wa sheria na ndivyo utaratibu wa kisheria ulivyo.​

1757923901864.png


 
Leo Jumatatu tarehe 15/09/2025 Jeshi la Polisi la Tanzania limetoa taarifa kwa umma kwamba limekua likifuatilia taarifa zinazotolewa na Balozi aliyejiuzuru Ndugu Humprey Polepole toka mwezi Julai, 2025.

Jeshi limeeleza kwamba tuhuma hizo zimekua zikiashiria uwepo wa makosa ya jinai, ambayo yanahitajika kuthibitishwa mbele ya Mahakama.

Hivyo baada ya kufungua jalada la uchunguzi, Jeshi la Polisi limemuelekeza Ndugu Polepole kufika katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, ili aweze kutoa maelezo/ushahidi kuhusiana na tuhuma ambazo amekua akizitoa kwa njia ya mtandao.

1757922986550.png
 

Attachments

  • Polisi kumuita Polepole.jpg
    Polisi kumuita Polepole.jpg
    88.6 KB · Views: 19
Hivi mnadhani Polepole atakuwa mjinga kiasi gani ajisalimishe

Hata hivyo, mnavyosema mmefungua jalada la uchunguzi, ni juu ya tuhuma zipi maana Polepole ametaja tuhuma nyingi

Hata hivyo, tangu lini mtu anayetuhumiwa akajifungulia jalada la kujichunguza

Karibu Tanzania uone maajabu
 

TAARIFA KWA UMMA​


Jeshi la Polisi Tanzania, lingependa kutoa taarifa kuwa lilifungua jalada la uchunguzi na linaendelea kuchunguza tuhuma mbalimbali ambazo amekuwa akitoa Humphrey Herson Polepole toka Julai 2025.

Tuhuma ambazo ametoa na anaendelea kuzitoa kulingana na jinsi alivyovielezea zinaashiria uwepo wa makosa ya kijiina na kwa mujibu wa sheria zinahitaji ushahidi wa kuthibitisha zitakapo wasilishwa mahakamani.

Tuhuma hizo amekuwa akizitoa kupitia mitandao ya Kijamii. Baada ya kufungua jalada na kuanza uchunguzi, Jeshi la Polisi mbali na kukusanya ushahidi, limekuwa likifanya jitihada za kumpata ili aweze kutoa maelezo/ushahidi na vilelezo vitakavyo thibitisha tuhuma hizo ili kuwezesha hatua zingine za kisheria ziweze kuchukuliwa kwa mujibu wa sheria na ndivyo utaratibu wa kisheria ulivyo.

Hivyo Jeshi la Polisi kupitia taarifa hii linaendelea kumwelekeza afike katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai ili aweze kutoa maelezo/ushahidi kuhusu tuhuma ambazo amekuwa akizitoa kwa umma kupitia Mitandao ya Kijamii.​

Imetolewa na:
Msemaji wa Jeshi la Polisi
Makao Makuu ya Polisi
Dodoma, Tanzania
1757923340275.png
 
Atoe ushahidi dhidi ya nani aliyefunguliwa mashtaka? Waanze kuwakamata kina Rostam ndipo Polepole aje mahakamani kutoa ushahidi.

Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA, Sura 20 R.E 2019) inawapa Polisi mamlaka ya kuchunguza tuhuma mara zinapotolewa. Wanaposema “tunamuita Polepole aje atoe ushahidi”, inamaanisha wanategemea mtoa tuhuma pekee badala ya wao wenyewe kufanya uchunguzi.
 

TAARIFA KWA UMMA​


Jeshi la Polisi Tanzania, lingependa kutoa taarifa kuwa lilifungua jalada la uchunguzi na linaendelea kuchunguza tuhuma mbalimbali ambazo amekuwa akitoa Humphrey Herson Polepole toka Julai 2025.

Tuhuma ambazo ametoa na anaendelea kuzitoa kulingana na jinsi alivyovielezea zinaashiria uwepo wa makosa ya kijiina na kwa mujibu wa sheria zinahitaji ushahidi wa kuthibitisha zitakapo wasilishwa mahakamani.

Tuhuma hizo amekuwa akizitoa kupitia mitandao ya Kijamii. Baada ya kufungua jalada na kuanza uchunguzi, Jeshi la Polisi mbali na kukusanya ushahidi, limekuwa likifanya jitihada za kumpata ili aweze kutoa maelezo/ushahidi na vilelezo vitakavyo thibitisha tuhuma hizo ili kuwezesha hatua zingine za kisheria ziweze kuchukuliwa kwa mujibu wa sheria na ndivyo utaratibu wa kisheria ulivyo.

Hivyo Jeshi la Polisi kupitia taarifa hii linaendelea kumwelekeza afike katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai ili aweze kutoa maelezo/ushahidi kuhusu tuhuma ambazo amekuwa akizitoa kwa umma kupitia Mitandao ya Kijamii.

Imetolewa na:
Msemaji wa Jeshi la Polisi
Makao Makuu ya Polisi
Dodoma, Tanzania
Sijui mtafanya nini kuirejesha imani yangu juu ya yote kwenu?
 
Back
Top Bottom