Polisi na wanasheria wa serikali wanawapa wanasiasa umaarufu kwa gharama nafuu

Mr Kind

Senior Member
Mar 4, 2017
178
308
Huo ndo mtazamo wangu hasa nikiangalia tukio la kukamatwa kwa Mh Lema na lilipofikia sasa hivi.

Pili, ni kuhusu kukamatwa kamatwa kwa Tundu Lisu na namna kesi zake zinavyoishia hewani hewani.

Jingine ni namna mashabiki, wafuasi na wakekereketwa wa vyama pinzani wanavyowindwa windwa kila kona na kukamatwa kamatwa au kupigwa mabomu ya machozi hata pasipo na sababu.

Hayo na mengine mengi yanaishia kuwapa au kuwafanya wanasiasa fulani kuzidi kuwa maarufu. kama serikali inadhani inawakomoa wapinzani ijue inawatengeneza wengi zaidi
 
Back
Top Bottom