Polisi mtaacha lini Rushwa?

Polisi mtaacha lini Rushwa?

Huyo mwenye kesi ndo alishirikiana na hao polisi kunibambikia hiyo kesi.. Pia niliwasikia wakizozana wao kwa wao baada ya kuona sina hatia yoyote ndio wakang'ang'ania niwape hiyo hela kama usumbufu wa kuishughulikia kesi yangu au waipeleke mbele nikashindane nao mahakamani..

Nikaona potelea mbali Funika Kombe Mwanaharamu apite.. Nikawapa tu hiyo hela yaishe!
Samahani kidogo mjomba! Mimi binafsi yangu natilia shaka saaana mazungumzo yako kuwa polisi " alishirikiana na mlalamikaji wako kukubambikia kesi".
Halafu unasema walipogundua kuwa huna hatia. Ndipo wakang'ang'ania uwape hizo pesa iweje wagundue? Wakati wanakubambikia kesi
 
umesahau kuingia kule ni bure kutoka unalipia...
 
Kuna wakati unaona wanakulazimisha na kutaka kukupotezea muda wako wakati una kazi nyingi za kufanya kulijenga Taifa pia familia inakuangalia basi inabidi uwe mpole tu, kwa sababu mimi mmoja wao zaidi ya 2

Na pia muda wote utakaopotea kudai haki naumia mwenyewe kwa gharama nyingi.. nikaona niwape tu yaishe!
Hapo ndipo mnapokosea!

Kwani wewe hujui KUTOA rushwa ni kosa sawasawa na KUPOKEA rushwa? ??
 
Itaisha tu wakiwapandishia maslahi yao na kuwajali sio muda wote kazini.
 
TAKUKURU? Kuna mhasibu wao bilionea unafikiri ni za mshahara?
Yule mhasibu alikuwa akifisadi hela za miradi mbalimbali ya Taasisi akishirikiana na mabosi wake. Ninaamini wote walioko kwenye hiyo chain watawajibishwa kwa mujibu wa sheria.

Kitendo cha muhasibu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa kuamua kuwa fisadi hakumaanishi tusiripoti matukio ya rushwa Taasisini. Wanalipwa kwa kodi zetu hivyo ni lazima watufanyie kazi! - Nao kama wakituomba tena rushwa, tuwaripoti kwenye mamlaka nyingine hadi KIELEWEKE!!!!
 
Samahani kidogo mjomba! Mimi binafsi yangu natilia shaka saaana mazungumzo yako kuwa polisi " alishirikiana na mlalamikaji wako kukubambikia kesi".
Halafu unasema walipogundua kuwa huna hatia. Ndipo wakang'ang'ania uwape hizo pesa iweje wagundue? Wakati wanakubambikia kesi

Kesi yenyewe ni ya kimtandao kuna group nilijiunga la whatsapp ikawa kuna kazi za msanii fulani zililetwa na admin sasa wakanikamata mimi ambaye sikushiriki kwa lolote zaidi ya kuwepo kwenye hilo group na ushahidi nilikuwa nao kwenye simu yangu maana pia nilikuwa mvivu wa kuchat kutokana na ubize wa kazi zangu...

Lakini wamenisumbua ili tu niwape hela hadi nikawapa ili yaishe, kwa sababu wamedai watapeleka kesi BASATA ili nisimame na serikali..
 
Salaam wanaJF
Leo mida ya asubuhi nimekuwepo central kufuatilia namna ya kumdhamini mfanyakazi mwenzangu aliekamatwa Kwa kesi ya madai
Sasa nimepeleka barua ya kumdhamini toka Kwa Afisa mtendaji
Kilichofuata hapo nikaanza kuzungushwa ili mradi nitoe fedha jamaa angu aachiwe wakati dhamana ni bure na nlitimiza vigezo vya kisheria
Jamaa wakanizungusha na kudai niwape angalau elfu 50 ili jamaa yangu wamuachie
Kiukweli nliwakomalia Sana hadi mwisho wa Siku wakamuachia
Kimsingi rushwa nchi hii haiwezi kuisha hasa Kwa hawa wenzetu wanaolinda usalama wa raia na Mali zao waache kuomba omba rushwa wakati salary wanapokea
Nlienda central saa 2 asubuhi jamaa anakuja kuachiwa saa 8 mchana
SAY NO TO CORRUPTION!
Hiyo ni pesa kidogo tu ya kupigia viatu kiwi siyo rushwa hiyo
 
Wataacha rushwa mbaka wakilipwa mishahara inayo kidhi mahitaji, nishackia police wengi wakilalamikia mishahara.
 
Kesi yenyewe ni ya kimtandao kuna group nilijiunga la whatsapp ikawa kuna kazi za msanii fulani zililetwa na admin sasa wakanikamata mimi ambaye sikushiriki kwa lolote zaidi ya kuwepo kwenye hilo group na ushahidi nilikuwa nao kwenye simu yangu maana pia nilikuwa mvivu wa kuchat kutokana na ubize wa kazi zangu...

Lakini wamenisumbua ili tu niwape hela hadi nikawapa ili yaishe, kwa sababu wamedai watapeleka kesi BASATA ili nisimame na serikali..
Kwa maana hiyo tuseme jamii iache rushwa kupitia jeshi la polisi. Tusiilalamikie polisi peke yake. Jamii nzima IJITATHMINI
 
Salaam wanaJF,

Leo mida ya asubuhi nimekuwepo central kufuatilia namna ya kumdhamini mfanyakazi mwenzangu aliekamatwa Kwa kesi ya madai.

Sasa nimepeleka barua ya kumdhamini toka Kwa Afisa mtendaji.

Kilichofuata hapo nikaanza kuzungushwa ili mradi nitoe fedha jamaa angu aachiwe wakati dhamana ni bure na nlitimiza vigezo vya kisheria.

Jamaa wakanizungusha na kudai niwape angalau elfu 50 ili jamaa yangu wamuachie
Kiukweli nliwakomalia Sana hadi mwisho wa Siku wakamuachia.

Kimsingi rushwa nchi hii haiwezi kuisha hasa Kwa hawa wenzetu wanaolinda usalama wa raia na Mali zao waache kuomba omba rushwa wakati salary wanapokea
Nlienda central saa 2 asubuhi jamaa anakuja kuachiwa saa 8 mchana.

SAY NO TO CORRUPTION!
Kesi ya madai polisi? Hebu fafanua hapo, maana polisi haihusiki na kesi hizo navyojua.
 
Mi sina hamu nao, nilishawahi kushikiliwa kuanzia saa 1 asubuhi hadi saa 12 jioni kwa kesi ya kusingiziwa tu na mazingira yote yanaonekana sikukosa chochote ila walikuwa wanalazimisha rushwa na walikomaa hadi nilitoa 100,000 ndio waliniachia... Yaani hawa watu Mungu anawaona!
Kusikiliza upande mmoja utaamini tu. Pamoja na hivyo, hebu elezea mazingira ya kukamatwa ili tuone kama kweli ulifanyiwa hujuma au wewe ndo ulifanya hujuma kuukwepa mkono wa dola
 
Umewaon polisi tu mbona wengin hamsemi ao takukuru ndo hao hao mbona hamsemi yule mhadibu wao
Ha ha ha mbuzi hule kulingana na urefu wa kamba yake. Hata kwenye tuhuma, hutuhumu yule unayekutana naye
 
Kuna wakati unaona wanakulazimisha na kutaka kukupotezea muda wako wakati una kazi nyingi za kufanya kulijenga Taifa pia familia inakuangalia basi inabidi uwe mpole tu, kwa sababu mimi mmoja wao zaidi ya 2

Na pia muda wote utakaopotea kudai haki naumia mwenyewe kwa gharama nyingi.. nikaona niwape tu yaishe!
Elezea mazingira tuyapime.
 
upo sahihi mtoa mada na hali hii inawafanya raia wengi wasiwe na imani na askari wengi ambao wanalichafua jeshi la polisi na kusababisha hata polisi waaminifu waonekane ni walewale
kumbe kuna polis waaminifu pia?
 
Hata mahakamani ndo hayohayo tu....Nimejionea mwenyewe this week"!
 
Polepole kasema hata mkulu wachenjua mchanga walitaka kumhonga bilioni 300 aipotezee ile ripoti ya mchanga. Na wala hajawachukulia hatua yoyote.
 
Salaam wanaJF,

Leo mida ya asubuhi nimekuwepo central kufuatilia namna ya kumdhamini mfanyakazi mwenzangu aliekamatwa Kwa kesi ya madai.

Sasa nimepeleka barua ya kumdhamini toka Kwa Afisa mtendaji.

Kilichofuata hapo nikaanza kuzungushwa ili mradi nitoe fedha jamaa angu aachiwe wakati dhamana ni bure na nlitimiza vigezo vya kisheria.

Jamaa wakanizungusha na kudai niwape angalau elfu 50 ili jamaa yangu wamuachie
Kiukweli nliwakomalia Sana hadi mwisho wa Siku wakamuachia.

Kimsingi rushwa nchi hii haiwezi kuisha hasa Kwa hawa wenzetu wanaolinda usalama wa raia na Mali zao waache kuomba omba rushwa wakati salary wanapokea
Nlienda central saa 2 asubuhi jamaa anakuja kuachiwa saa 8 mchana.

SAY NO TO CORRUPTION!
Luka 3:14
Neno: Bibilia Takatifu

14 Na baadhi ya askari wakamwuliza, “Na sisi je, tufanye nini?” Akawajibu: “Msichukue fedha za watu kwa kutumia nguvu; msiwashtaki watu kwa kuwasingizia makosa; bali mtosheke na mishahara yenu!”
 
Kiukweli nliwakomalia Sana hadi mwisho wa Siku wakamuachia
Wataacha utakapoendelea kukomaa bila kutoa rushwa na wengine wasipu toa rushwa polisi wataacha kupokea rushwa kwa kuwa hakuna wakuwapa rushwa.
 
Back
Top Bottom