Polisi: Marehemu Ally Zona aligongwa na kitu kizito na sio Risasi

madibira1

Member
Dec 18, 2011
80
16
Nimeona katika Channel Ten polisi wametoa ripoti kwamba marehemu Ally aliyeuawa katika maandamano ya Chadema Morogoro amefariki kutokana na kugongwa na kitu kizito sio risasi, hiyo ni baada ya uchunguzi wa madaktari.

 
ni ngumu sana kumkabidhi fisi bucha au zizi la mbuzi hatutaweza kupata suluhu hadi tume huru ya mahakama
 
Hili ni picha la kihindi hivi na wale majeluhi na wenyewe wapondwa na vyuma vizito? Nauliza mwenye habari zao atuhabalishe.
 
Ukweli anao mungu. Mungu hafichi kitu. Ipo siku itajulikana tu. Ee mola mrehem ally mpumzishe kwa aman. Damu yake imetumika na uonyeshe ukweli kwa kutumia damu yake. Amin.
 
Aahhh hawana jipya kama tume imeundwa na IGP kwa nini RPC anashupalia kutoa tamko??si angesubiri uchunguzi wa tume??
 
Mtu utarajie majibu gani kama unanituhumu kwa mauaji na mimi nichunguze mazingira ya kifo na thn nitoe taarifa mimi..." kabisa haiingii akilini...hatungeshangaa hata kma wangesema kafa kwa ajari ya basi!
 
Kweli siku hizi Binadamu kawa kama kuku anakufa watu wanakuja na majibu ya uongo anazikwa na kusaulika........Nasikitika sana
 
ahaa...kwahiyo nani kaua sasa...hii nchi kuna watu wanafikiri watanzania ni kama viongozi wa ccm....sisi akili zinafanya kazi hatupelekwi kama ng'ombe na tunajua nin kimetokea kwa hiyo hatudanganyiki...
 
Nimeona katika Channel Ten polisi wametoa ripoti kwamba marehemu Ally aliyeuawa katika maandamano ya Chadema Morogoro amefariki kutokana na kugongwa na kitu kizito sio risasi, hiyo ni baada ya uchunguzi wa madaktari

are u serious? Ngoja tusubiri kama kuna mwingine kaangalia hio taarifa, kama ni kweli basi kuna haja ya kukapindua haka kaserikali legelege
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…