Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,437
- 5,235
Jeshi la Polisi nchini Tanzania limetoa ufafanuzi kuhusu matukio ya utekaji na kupotea kwa watu ambayo yamekuwa yakiripotiwa mara kwa mara katika vituo vya polisi ambapo kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa kwa kina, imebainika kuwa si matukio yote yanayotokana na uhalifu wa kweli, bali mengine yamekuwa yakisababishwa na sababu binafsi au za kijamii
Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) David Misime, amesema kuwa baadhi ya matukio hayo yanatokana na watu kujiteka wenyewe, wivu wa mapenzi, imani za kishirikina, migogoro ya kugombea mali, pamoja na nia ya kulipiza kisasi.
Aidha (DCP) Misime amesema kuwa jeshi la polisi linaendelea kufanya uchunguzi wa kina katika kila tukio linaloripotiwa, ili kuhakikisha ukweli unajulikana na hatua stahiki zinachukuliwa. Aidha, amewaasa wananchi kuacha kutumia njia za udanganyifu au kuchukua sheria mikononi mwao, na badala yake kushirikiana na vyombo vya dola katika kutatua migogoro na matatizo yao.
Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) David Misime, amesema kuwa baadhi ya matukio hayo yanatokana na watu kujiteka wenyewe, wivu wa mapenzi, imani za kishirikina, migogoro ya kugombea mali, pamoja na nia ya kulipiza kisasi.
Aidha (DCP) Misime amesema kuwa jeshi la polisi linaendelea kufanya uchunguzi wa kina katika kila tukio linaloripotiwa, ili kuhakikisha ukweli unajulikana na hatua stahiki zinachukuliwa. Aidha, amewaasa wananchi kuacha kutumia njia za udanganyifu au kuchukua sheria mikononi mwao, na badala yake kushirikiana na vyombo vya dola katika kutatua migogoro na matatizo yao.