Polisi: Baadhi ya matukio ya utekaji ni kujiteka wenyewe na migogoro ya kifamilia

Polisi: Baadhi ya matukio ya utekaji ni kujiteka wenyewe na migogoro ya kifamilia

Mkalukungone Mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
2,437
Reaction score
5,235
Jeshi la Polisi nchini Tanzania limetoa ufafanuzi kuhusu matukio ya utekaji na kupotea kwa watu ambayo yamekuwa yakiripotiwa mara kwa mara katika vituo vya polisi ambapo kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa kwa kina, imebainika kuwa si matukio yote yanayotokana na uhalifu wa kweli, bali mengine yamekuwa yakisababishwa na sababu binafsi au za kijamii

Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) David Misime, amesema kuwa baadhi ya matukio hayo yanatokana na watu kujiteka wenyewe, wivu wa mapenzi, imani za kishirikina, migogoro ya kugombea mali, pamoja na nia ya kulipiza kisasi.

Aidha (DCP) Misime amesema kuwa jeshi la polisi linaendelea kufanya uchunguzi wa kina katika kila tukio linaloripotiwa, ili kuhakikisha ukweli unajulikana na hatua stahiki zinachukuliwa. Aidha, amewaasa wananchi kuacha kutumia njia za udanganyifu au kuchukua sheria mikononi mwao, na badala yake kushirikiana na vyombo vya dola katika kutatua migogoro na matatizo yao.

 
Haya wafafanue sasa uchunguzi juu ya kushambuliwa kwa Lissu umefikia wapi?

Ni ndugu yupi amempoteza:
1. Ben Saanane,
2. Ali Kibao,
3. Mdude,
4. n.k
 
Back
Top Bottom