Alisema mtoa taarifa alieleza kwamba wakati askari huyo anaingia Friend's Pub, aliteleza na kuanguka kwenye ngazi na baadaye alimwinua na kumtoa nje kisha askari huyo alirejea na kukaa kwenye kochi wakati huo mhudumu akiendelea kuhudumia wateja.
“Ilipofika majira ya saa 4:15 asubuhi jana (juzi), wahudumu wakiwa wanafanya kazi za usafi, ndipo walipomwona PC Donald akiwa kwenye kochi wakidhani amelala lakini walipojaribu kumwamsha hakuamka ndipo walipotoa taarifa polisi. Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufani ya Mkoa wa Ruvuma