Enzi hiyo alikuwa anatetea Serikali 3(tatu) kwenye makongamano tofauti Na msimamo wa Chama.Polepole aache unafiki kwani kwa kauli zake alithibitisha kuwa chama kilioza.
Chama kilichoka mpaka akasema kuwa uchaguzi ukiwa wa haki ccm hakitashinda.
Inamaana chama kilioza na yeye alikuwa kwenye upande wa kukibeza chama wakati nape na kinana wakikipigania chama.
Polepole acha unafiki hukua na uchungu na chama kama nape.
Madaraka yasikutie upovu na kujidhalilisha.
Kumbuka kauli zako
Kwani alifanya kazi hiyo pekee? Si aliajiriwa kwa kazi hiyo? Nani anayembeza na zawadi ya kazi aliyoifanya alishapewa na kachezea hela kwenye shimo la choo na pesa imetumbukia shimoni. Akafie mbele huko... ati kakitoa chama shimoni.....fankuuuuroooHata Tanganyika ilikuwepo kabla ya Nyerere. Huenda hakuitoa shimoni, lakini mchango wake kwenye uchaguzi 2015 si wa kubeza.
Kajamaa kanafki sana.polepole ni ndumilakuwili
itasaidia nini muda huu? Ndio atapokewa upinzani? ama ataonesha utoto na uvunjaji wa sheria?? Besides nani atamwamini??Mwageni ugali amwage mboga mpaka alivyofunga goli la mkono.
Itasaidia tunaofuata na kutunza historia kuondoa ukungu kutoka katika mdomo wa kada wa CCM.itasaidia nini muda huu? Ndio atapokewa upinzani? ama ataonesha utoto na uvunjaji wa sheria?? Besides nani atamwamini??
acha kujidanganya, hana lolote awezalo kaka,,,,,Mwageni ugali amwage mboga mpaka alivyofunga goli la mkono.
Mkuu wanaolima wengine wanaovuna wengine na wanaokula wengine, nape, kinana, mangula walilima. Magufuli, Samia hawa walivuna. H polepole, makonda hawa wanakulaHiyo ni kweli,lakini huwez kukataa jitihada za Nape na Mzee Kinana kukiokoa,labda kama kichwa chako kina hitilafu,lakini ukiwa na akili timamu,ukaacha kujitoa ufahamu kishabiki mchango wa Nape au Mzee Kinana wa kuiokoa CCM ya Mzee Mkama huwez kubeza.
Ashugulikiwe Nape. Ikiwezekana AFUKUZWE UANACHAMA
Katibu wa Itikadi na Uenezi (KIU) wa CCM, Humphrey Polepole akizungumza na waandishi wa Mwananchi Communications Limited (MCL) wakati alipotembelea chumba cha habari cha kampuni hiyo, Tabata Relini jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni Katibu wa UVCCM wa Makao Makuu Idara ya Vyuo Vikuu, Debora Charles. Picha na Salim Shao
- Nape, ambaye alikuwa akishikilia nafasi ya Polepole kabla ya Uchaguzi Mkuu, alisema maneno hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari Machi 23, siku moja baada ya kuachwa katika mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri.
- Nape aliyetishiwa bastola kabla ya mkutano huo, alikuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.
Dar es Salaam. Katibu wa Itikadi na uenezi wa CCM, Humphrey Polepole amekitaka chama hicho kumwajibisha Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye kwa kauli yake kuwa alikitoa chama hicho shimoni.
Nape, ambaye alikuwa akishikilia nafasi ya Polepole kabla ya Uchaguzi Mkuu, alisema maneno hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari Machi 23, siku moja baada ya kuachwa katika mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri.
Nape aliyetishiwa bastola kabla ya mkutano huo, alikuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.
“Wamesahau wakati mimi nalala porini, wenyewe walikuwa wanakunywa bia baa. Nimekuwa mzalendo kwa nchi yangu, nimekuwa muungwana kwa chama changu na ninaapa kuwa muungwana kwa nchi yangu, hilo hakuna atakayelibadilisha. Lakini mimi nimekuwa mzalendo kwa CCM ambayo nimeikuta kwenye shimo inakwenda,” alisema Nape.
Lakini Polepole, ambaye jana alitembelea ofisi za kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL) inayozalisha magazeti ya Mwananchi, The Citizen na Mwanaspoti, alisema kama Nape alitoa kauli hiyo, alikuwa amekengeuka.
“Amekitoa Chama cha Mapinduzi shimoni? Kwamba, wakati anakitoa chama shimoni wengine walikuwa wanafanya nini?” alihoji Polepole.
Sasa mbona mnamshikia bango na kumtishia nyau?acha kujidanganya, hana lolote awezalo kaka,,,,,
kwani ye ni chama gani kaka,Sasa mbona mnamshikia bango na kumtishia nyau?
Kwani ubunge wa Mtama anawakilisha kwa chama gani?kwani ye ni chama gani kaka,