Aneth Anton
Member
- Nov 22, 2019
- 20
- 10
Duniani kuna njia 3 tu za kutwaa uongozi wa taifa.
Njia ya kwanza ni ya mazungumzo. Njia hii mfano mzuri ni Mwalimu Nyerere. Aliitumia akatwaa uongozi wa Taifa.
Ni njia ngumu mno inayohitaji kipaji cha kupanga hoja (power of thinking and analyzing), kuongea (power of oratory), ushawishi (convincing power), uadilifu (integrity) na uhamasushaji umma (mass mobilization).
Mwalimu alikuwa gwiji wa yote haya. Njia hii mpumbavu au mjinga akiitumia hafanikiwi ng'o!
Njia ya pili ni ya kutumia mabavu. Museveni ni mfano mzuri. Unatwaa utawala kwa mabavu.
Njia hii imetumiwa na watawala anuwai duniani. Mtake msitake atatwaa alimradi ana nyenzo za mabavu ambazo ni watu wanaomuunga mkono, silaha na utawala dhaifu.
Njia hii haifui dafu kama hivi vitatu havipo. Ni wehu kuijaribu njia hii ikiwa haya hayapo. Moja ya nchi ambayo haya hayapo ni Tanzania.
Unaweza kukataa lakini tuliza akili utauona ukweli. Ni ngumu mtu kutwaa utawala kimabavu Tanzania.
Try at your own peril. Kuna nchi za wenzetu pia zimefikia hali hii ya kuwa na 'immunity'. Huwezi kutwaa madaraka kwa nguvu mfano US, UK, Japan! Hakuna nafasi!
Kama kuna jambo Mwalimu anapaswa kuenziwa ni hili! Alilisuka Taifa hadi likapata hii immunity. Mimi naiita IMMUNITY AGAINST FORCED ENTRY INTO POWER.
Unaweza kudai unavyotaka au akili yako inavyokutuma! Ukweli utabaki ukweli. Kuingia kwa mabavu Tanzania haiwezekaniki.
Njia ya tatu ni ya sanduku la kura. Njia hii inakubalika kila kona duniani. Hii ni kwa kuwa historia imetufundisha kuwa sio kila mmoja ana uhodari wa kuongea hadi apewe utawala wa taifa.
Pia kuingia madarakani kwa nguvu kuna athari nyingi kuliko faida. Tizama Libya, Iraq, Afghanistan na Yemen. Watu wameingizwa kwa nguvu madarakani matokeo balaa tupu!
Hapo ndio wapinzani Tanzania walipopotea sana.
Njia ya kwanza imewatupa mkono. Hawana karama ya maongezi! Hata wangepewa nafasi ya kuongea kutwa kucha bado njia hii isingewaingiza madarakani.
Ni njia wasiyoiweza kabisa. Nyerere licha ya kufungwa, kushitakiwa, kudhihakiwa, kusumbuliwa na mkoloni hakuwahi kuwatusi au kupinga mipango yao ya maendeleo japo maendeleo yalikuwa yanalenga UK!
Akiongea nao kwa staha. Alijenga hoja. Hebu fikiria kauli za wapinzani wetu? Hebu fikiri wanavyosherehekea ndege kukamatwa? Hebu fikiria wanavyopinga ujenzi wa reli au bandari? Ni tofauti mno. Njia ya mazungumzo haiwafai!
Ukitizama njia ya mabavu ndio kabisaa! Hawana nyenzo hata moja kati ya zile 3 ili waweze kutumia mabavu.
Lakini utasikia "TUSILAUMIANE", "NGUVU YA UMMA" Kichekesho! Njia hii wala wasiiote! Hawana uwezo.
Kwao njia iliyosalia ilikuwa ya sanduku la kura! Sasa kituko wameitupa mkono.Sawa na masikini ana hela ndogo anaichezea kamari!
Sasa hivi wapinzani wamekosa njia yoyote ya kutafutia utawala wa nchi. Njia zote tatu kwao zimekwama.
Na wasipojirekebisha wakaamua kutumia njia pekee ambayo walau wanaweza kufurukuta yaani njia ya sanduku la kura mwaka 2020 watajuta milele.
Huwezi kuwa mkulima ukatae kutayarisha shamba! Au ukatae kulima udai mwenzako aliyelima atakutambua!
Njia ya kwanza ni ya mazungumzo. Njia hii mfano mzuri ni Mwalimu Nyerere. Aliitumia akatwaa uongozi wa Taifa.
Ni njia ngumu mno inayohitaji kipaji cha kupanga hoja (power of thinking and analyzing), kuongea (power of oratory), ushawishi (convincing power), uadilifu (integrity) na uhamasushaji umma (mass mobilization).
Mwalimu alikuwa gwiji wa yote haya. Njia hii mpumbavu au mjinga akiitumia hafanikiwi ng'o!
Njia ya pili ni ya kutumia mabavu. Museveni ni mfano mzuri. Unatwaa utawala kwa mabavu.
Njia hii imetumiwa na watawala anuwai duniani. Mtake msitake atatwaa alimradi ana nyenzo za mabavu ambazo ni watu wanaomuunga mkono, silaha na utawala dhaifu.
Njia hii haifui dafu kama hivi vitatu havipo. Ni wehu kuijaribu njia hii ikiwa haya hayapo. Moja ya nchi ambayo haya hayapo ni Tanzania.
Unaweza kukataa lakini tuliza akili utauona ukweli. Ni ngumu mtu kutwaa utawala kimabavu Tanzania.
Try at your own peril. Kuna nchi za wenzetu pia zimefikia hali hii ya kuwa na 'immunity'. Huwezi kutwaa madaraka kwa nguvu mfano US, UK, Japan! Hakuna nafasi!
Kama kuna jambo Mwalimu anapaswa kuenziwa ni hili! Alilisuka Taifa hadi likapata hii immunity. Mimi naiita IMMUNITY AGAINST FORCED ENTRY INTO POWER.
Unaweza kudai unavyotaka au akili yako inavyokutuma! Ukweli utabaki ukweli. Kuingia kwa mabavu Tanzania haiwezekaniki.
Njia ya tatu ni ya sanduku la kura. Njia hii inakubalika kila kona duniani. Hii ni kwa kuwa historia imetufundisha kuwa sio kila mmoja ana uhodari wa kuongea hadi apewe utawala wa taifa.
Pia kuingia madarakani kwa nguvu kuna athari nyingi kuliko faida. Tizama Libya, Iraq, Afghanistan na Yemen. Watu wameingizwa kwa nguvu madarakani matokeo balaa tupu!
Hapo ndio wapinzani Tanzania walipopotea sana.
Njia ya kwanza imewatupa mkono. Hawana karama ya maongezi! Hata wangepewa nafasi ya kuongea kutwa kucha bado njia hii isingewaingiza madarakani.
Ni njia wasiyoiweza kabisa. Nyerere licha ya kufungwa, kushitakiwa, kudhihakiwa, kusumbuliwa na mkoloni hakuwahi kuwatusi au kupinga mipango yao ya maendeleo japo maendeleo yalikuwa yanalenga UK!
Akiongea nao kwa staha. Alijenga hoja. Hebu fikiria kauli za wapinzani wetu? Hebu fikiri wanavyosherehekea ndege kukamatwa? Hebu fikiria wanavyopinga ujenzi wa reli au bandari? Ni tofauti mno. Njia ya mazungumzo haiwafai!
Ukitizama njia ya mabavu ndio kabisaa! Hawana nyenzo hata moja kati ya zile 3 ili waweze kutumia mabavu.
Lakini utasikia "TUSILAUMIANE", "NGUVU YA UMMA" Kichekesho! Njia hii wala wasiiote! Hawana uwezo.
Kwao njia iliyosalia ilikuwa ya sanduku la kura! Sasa kituko wameitupa mkono.Sawa na masikini ana hela ndogo anaichezea kamari!
Sasa hivi wapinzani wamekosa njia yoyote ya kutafutia utawala wa nchi. Njia zote tatu kwao zimekwama.
Na wasipojirekebisha wakaamua kutumia njia pekee ambayo walau wanaweza kufurukuta yaani njia ya sanduku la kura mwaka 2020 watajuta milele.
Huwezi kuwa mkulima ukatae kutayarisha shamba! Au ukatae kulima udai mwenzako aliyelima atakutambua!