Pole sana bwana Kibanga Ampiga Mkoloni,watanzania ndivyo tulivyo

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,014
144,372
Kibanga Ampiga Mkoloni leo ameleta uzi wenye ushauri mzuri sana kwa serikali ulioandikwa na mkazi mmoja wa Dar-es-salaa ukiwa katika lugha ya kingereza.

Hata hivyo, huwezi amini kuwa uzi ule umepata wachangiaji wawili tu licha ya ukweli kuwa uzi husika umebeba mawazo ambayo naweza kuyaita ni "constructive criticism" kwa wataalamu wetu pamoja na wanasiasa wetu(watawala).

Nashauri uongozi wa JF ifike mahali watumie mamlaka yao ku-select baadhi ya thread ambazo kwa mtazamo wao(na bila shaka utakuwa mtazamo wa wengi) wanaona thread husika ina manufaa kwa nchi na hivyo waiweke "sticky" ili ujumbe uwafikie watawala au wahusika wengine bila kujali kama member wa JF wana-interest na uzi huo au laa.

Hali hii ni ushahidi tosha ni kwanini magazeti ya udaku yanauzika sana hapa Bongo kuliko magazeti yanayoandika habari za kisiasa,kiuchumi na kijamii.

Pia huh ni ushahidi mwingine ni kwanini watanzania wengi hawapendi kuangali taarifa za habari na badala yake ni wapenzi zaidi wa vipindi vya michezo na maigizo.
 
Last edited:
Topic nyingi zisiso na maana ndo zinahit, nadhan watu wana id nyingi wanazipromote wenyew, humu saiv tunaenda kisiasa, tija imepungua.
 
Sasa kwa nini na yeye auweke kwa kiingereza...kuna mtu humu huwa anauliza "alitusomesha"
Tatizo wala sio kingereza bali tatizo ni kuwa uzi husika hauipondi CHADEMA,CCM n.k na wala hauongelea habari za Lowassa,JK,Mbowe na wengineo.

Hii ndio shida yetu kubwa hapa JF.
 
Embu weka link mkuu wangu ila kiinglish sametimu kigumuuu...
 
Tatizo ni mtizamo wa wengi ni kujadili watu badala ya hoja.
Pia sishangai maana siku hizi watu wanachora Zombie kwenye mitihani Pro. Mchome anashauri wapewa Division 5 mwisho wa siku tunaambulia vilaza watupu.
 
Back
Top Bottom