Poland yamvimbia Russia, huu ujasiri wanautoa wapi?

Poland yamvimbia Russia, huu ujasiri wanautoa wapi?

kyagata

JF-Expert Member
Joined
Oct 18, 2016
Posts
13,960
Reaction score
26,135
Poland wamedungua Drones za Urusi zilizoingia kwenye anga yake kimakosa.

Hawa jamaa huu ujasiri wa kumvimbia Russia wanatoa wapi?

Screenshot_20250910_080647_Instagram.jpg
 
Poland wamedungua Drones za Urusi zilizoingia kwenye anga yake kimakosa.

Hawa jamaa huu ujasiri wa kumvimbia Russia wanatoa wapi?

View attachment 3468965
Polish huwa ni watu wabishi, hata Soviet Union walipata shida Papa alipochaguliwa John Paul II raia wa Poland, mchakamchaka waliupata maana walizoea kuonea Wakristo na ndio sababu walimpiga risasi bahati nzuri alipona.

Poland ilipigana na Ukraine mwaka 1918 ikashinda, mwaka 1919 ikachokozwa na USSR ya Vladimir Lenin ambayo iliiteka Ukraine kuiunganisha kwenye Soviet Union. Poland ikawafuata kuanzia Kiev ikaenda mpaka Belarus ikawapiga Warusi. Kasome Miracle on the Vistula ambapo dunia ilidhani Poland watapigwa kumbe wapi.

Wakasaini mkataba wa kutambua mpaka ambao Poland walitaka ingawa pia hawakuwa wanataka USSR ikue iunganishe Belarus na Ukraine (waliona changamoto za baadae).

Mwaka 1939 Hitler aliivamia Austria peke yake, Ufaransa peke yake, Belgium peke yake ila kwa Poland aliomba msaada wa USSR nusu Ujerumani ikaivamia na nusu USSR ikaivamia. Ila ingekuwa ni Poland avamiwe na USSR peke yake au Nazi Germany peke yake wangepotezewa sana muda ingawa wangeshinda. Wasovieti walipoteka nusu yao wakawinda kila anayevaa miwani (that time almost kila anayevaa miwani alisoma sana maana walikuwa wanasoma kwenye low light usiku wanapata madhara ya macho, kwahiyo kafika chuo), wakaua wanajeshi, maofisa usalama na watumishi wa umma. Katyn Massacre Wasovieti waliua Wapolish over 20,000. Baadhi walitoroka mmojawapo ni Marian Rejewski aliyegundua njia ya ku-decode Enigma machine vita ile. Mwingine ni General Stanislaw Sosabowski aliongoza majeshi ya Poland yaliyofanikiwa kutoroka kupigana kutokea Uingereza kukomboa nchi yao, alishiriki Operation Market Garden.

Turudi 1939, upande wa Ujerumani walianza kuvamia Danzig kamji ka pwani kanakojitegemea kiutawala sio mamlaka kamili ya Poland ila hiyo vita Polish walivyoivaa utadhani umevamiwa mji mkuu. Ilizuka battle of Westerplatte, Ujerumani ilikuja na ndege 60, melivita mbili na wanajeshi zaidi ya 3,000 ikatumia wiki kupigana na wanajeshi chini ya 300 wa Poland wasio na ndege wala melivita na hawana supply.

Kila wakitumia kitu kinapungua idadi, kila anayejeruhiwa au kufa anapunguza idadi ya wapiganaji, huwezi enda hospitali, huwezi letewa chakula wala dawa, walijichimbia wiki nzima wanapigana na hapo command kutoka makao makuu imekatika wanapigana kichwakichwa.
Na hapo walipigana na ile Ujerumani ya mwanzoni kabisa ambayo ina kila kitu na ina jeshi bora zaidi duniani.

Poland sio watu wazembe vitani hata kidogo, alafu hawatishiwi. Na miaka hii ya 2020s wana massive rearmament wanaunda silaha, kununua kutoka South Korea na Marekani na washirika wengine. Na wameongeza idadi ya active troops kwa sasa ndio nchi ya NATO inayotumia GDP kubwa jeshini.

Sababu kwanini wako hivi? Kipindi ni wanyonge walionewa kila jirani alikuwa mkorofi wakaipoteza Fisrt Polish Republic. Poland mwaka 1025 walikuwa na Ufalme na jina lao hili, baada ya hapo uvamizi, kuungana, kutengana vilifuata.
 
Polish huwa ni watu wabishi, hata Soviet Union walipata shida Papa alipochaguliwa John Paul II raia wa Poland, mchakamchaka waliupata maana walizoea kuonea Wakristo na ndio sababu walimpiga risasi bahati nzuri alipona.

Poland ilipigana na Ukraine mwaka 1918 ikashinda, mwaka 1919 ikachokozwa na USSR ya Vladimir Lenin ambayo iliiteka Ukraine kuiunganisha kwenye Soviet Union. Poland ikawafuata kuanzia Kiev ikaenda mpaka Belarus ikawapiga Warusi. Kasome Miracle on the Vistula ambapo dunia ilidhani Poland watapigwa kumbe wapi.

Wakasaini mkataba wa kutambua mpaka ambao Poland walitaka ingawa pia hawakuwa wanataka USSR ikue iunganishe Belarus na Ukraine (waliona changamoto za baadae).

Mwaka 1939 Hitler aliivamia Austria peke yake, Ufaransa peke yake, Belgium peke yake ila kwa Poland aliomba msaada wa USSR nusu Ujerumani ikaivamia na nusu USSR ikaivamia. Ila ingekuwa ni Poland avamiwe na USSR peke yake au Nazi Germany peke yake wangepotezewa sana muda ingawa wangeshinda. Wasovieti walipoteka nusu yao wakawinda kila anayevaa miwani (that time almost kila anayevaa miwani alisoma sana maana walikuwa wanasoma kwenye low light usiku wanapata madhara ya macho, kwahiyo kafika chuo), wakaua wanajeshi, maofisa usalama na watumishi wa umma. Katyn Massacre Wasovieti waliua Wapolish over 20,000. Baadhi walitoroka mmojawapo ni Marian Rejewski aliyegundua njia ya ku-decode Enigma machine vita ile. Mwingine ni General Stanislaw Sosabowski aliongoza majeshi ya Poland yaliyofanikiwa kutoroka kupigana kutokea Uingereza kukomboa nchi yao, alishiriki Operation Market Garden.

Turudi 1939, upande wa Ujerumani walianza kuvamia Danzig kamji ka pwani kanakojitegemea kiutawala sio mamlaka kamili ya Poland ila hiyo vita Polish walivyoivaa utadhani umevamiwa mji mkuu. Ilizuka battle of Westerplatte, Ujerumani ilikuja na ndege 60, melivita mbili na wanajeshi zaidi ya 3,000 ikatumia wiki kupigana na wanajeshi chini ya 300 wa Poland wasio na ndege wala melivita na hawana supply.

Kila wakitumia kitu kinapungua idadi, kila anayejeruhiwa au kufa anapunguza idadi ya wapiganaji, huwezi enda hospitali, huwezi letewa chakula wala dawa, walijichimbia wiki nzima wanapigana na hapo command kutoka makao makuu imekatika wanapigana kichwakichwa.
Na hapo walipigana na ile Ujerumani ya mwanzoni kabisa ambayo ina kila kitu na ina jeshi bora zaidi duniani.

Poland sio watu wazembe vitani hata kidogo, alafu hawatishiwi. Na miaka hii ya 2020s wana massive rearmament wanaunda silaha, kununua kutoka South Korea na Marekani na washirika wengine. Na wameongeza idadi ya active troops kwa sasa ndio nchi ya NATO inayotumia GDP kubwa jeshini.

Sababu kwanini wako hivi? Kipindi ni wanyonge walionewa kila jirani alikuwa mkorofi wakaipoteza Fisrt Polish Republic. Poland mwaka 1025 walikuwa na Ufalme na jina lao hili, baada ya hapo uvamizi, kuungana, kutengana vilifuata.
Nilijua utasema wa Poland walivyo wabishi watarusha drone kwenda Russia
Kumbe umekuja na ngojera zako za kila siku,
Bora urudi shambani ujiandae na kilimo cha mwakani sidhani kama kuna mtu humu atakuelewa na uchambuzi wako ulisha jivua credit zote ulizo kuwa unapewa na member wa humu sasa hivi huna tofauti na kipanya
 
Nyuma ya Ukraine kuna NATO yote

Mpaka sasa S.O ina miaka 3. Unajua gharama ya kugharamia vita miaka 3?

Russia iko ndani ya mipaka ya Ukraine, 20% ya ardhi ya Ukraine iko chini ya Russia.

Kuna wakati ni vyema mkawa mnashirikisha ubongo kucomment
Kwani Urusi mbona nae anapewa misaada na Kiduku na Iran na China
 
Poland wamedungua Drones za Urusi zilizoingia kwenye anga yake kimakosa.

Hawa jamaa huu ujasiri wa kumvimbia Russia wanatoa wapi?

View attachment 3468965
Poland ni NATO. Kuna majeshi ya Marekani sasa hivi huko.

Russia akiipiga Poland kaanzisha vita na NATO yote. Article 4 ya NATO. Ukimpiga mwanachama mmoja wa NATO ni kama umewapiga wote.

Kuna jamaa yangu yuko huko kama sehemu ya majeshi ya US.

Poland wamesha invoke article 4.

 
Nilijua utasema wa Poland walivyo wabishi watarusha drone kwenda Russia
Kumbe umekuja na ngojera zako za kila siku,
Bora urudi shambani ujiandae na kilimo cha mwakani sidhani kama kuna mtu humu atakuelewa na uchambuzi wako ulisha jivua credit zote ulizo kuwa unapewa na member wa humu sasa hivi huna tofauti na kipanya
Unanifuatilia? Huna kazi za kufanya mbona sikujui mimi.
 
Poland ni NATO. Kuna majeshi ya Marekani sasa hivi huko.

Russia akiipiga Poland kaanzisha vita na NATO yote. Article 4 ya NATO. Ukimpiga mwanachama mmoja wa NATO ni kama umewapiga wote.

Kuna jamaa yangu yuko huko kama sehemu ya majeshi ya US.

Poland wamesha invoke article 4.

Mkuu, ni Article 5 ndo inosema mwanachama mmoja akivamiwa kijeshi basi NATO yote ndo wataingia vitani.

Article 4 yaipa nafasi nchi ilojibu mashambulizi yoyote kuita mkutano wa NATO na kujadili kilotokea na kama hayo yalikuwa ni mashambulizi ya kupanga lqkini hakuna ile twaita trigger of military action kama ilivyo Article 5 ambayo ina "collective defense element which triggers military action.

Article 4 yasema hivi: "NATO's Article 4 states: "The parties will consult together whenever, in the opinion of any of them, the territorial integrity, political independence or security of any of the parties is threatened."

Russia tiyari imesema haina nia ya kuishambulia Poland na ilikuwa ikishambulia mji wa Lviv ambao upo karibu na Poland ambayo ililazimika kuzidungua hivyo UAVs zilokuwa enroute kwa Lviv lakini zikaingia kwa bahati mbaya sehemu ndogo tu ya anga la Poland.

Lakini ukisoma statements zao utagundua kuwa wanasema hawakuwa na nia ya kushambulia anga la Poland na kwamba hakuna ushahidi kwamba hizo UAVs ni za Russia.

Ila kwa wafuatiliaji twaona kuwa Russia iko kazini ikizijaribu ADSs za NATO members. kupima uhimilivu au resillience.
 
Back
Top Bottom