Points 10 za ujenzi: Unyevu/damp katika jengo

Nashukuru sana mkuu,itakuwa na msaada mkubwa kwangu. Kuna muda Hadi huwa namwambia jamaa yangu kuwa najuta Sana kujenga bila ya kufanya upembuzi yakinifu.
well,ni kwasababu ya kukosa elimu husika
 

Hapo Unyevu unatoka kwenye mfumo wa Paa...
  • Umeteremka hadi kwenye Dari..
  • Ukuta ulikuwa bado haujapigwa rangi
  • Huo upande wa ukuta haupigwi na jua,ndiyo mana ukijani a.k.a fungi unatanaradi
 

Hapa kuna Unyevu kupanda na Unyevu Penyezi...
  • Jirani ya ukuta kuna miti mikubwa mitatu ya Mwarobaini
  • Inazuia mwanga wa jua kutofikia ukuta na kukausha huo unyevu
 
greater than kuna majengo ya ghorofa 1 nimeona hawaweki jamvi yaan boma linaanzia tu baada ya mkanda wa chini as if ni nyumba isiyo ya ghorofa na wanaweka tu rough floor then tiles ingawa yana nguzo, mikanda na base kawa kawaida ya ghorofa zinavyojengwa hii kitaalam ni sahihi? je haiwezi pelekea jengo kutitia au kuanguka?
 
Kama haujajenga juu ya mwamba
Kutitia kwa jengo huwa ni lazima...ila kinachoangaliwa kiwango cha utitiaji...huwa initial settlement

Kwenye hilo Jengo....
Uzito wa jengo unapelekea kwenye nguzo, kwahiyo hapo ili lisititie,kwa kasi kubwa.
  • Uhimilivu wa udongo
  • Uzito wa jengo husika
  • Sanifu ya mfumo wa nguzo
  • Mazingira ya kiwanja
 
Kwa hiyo inawezekana kudesign then kujenga ghorofa moja bila jamvi na kusiwe na madhara au jamvi ni lazima no option?
 
Kwa hiyo inawezekana kudesign then kujenga ghorofa moja bila jamvi na kusiwe na madhara au jamvi ni lazima no option?
Inawezekana....
Huwa kuna suspended floor,,,yani sakafu isiyoegemea ardhi...

Lakini kwa mfumo kama waliotumia wao wa kugemeza sakafu kwenye udongo huku wakiwa na hawajaweka jamvi, shida kubwa itakuja kwenye.
  • Udhibiti wa mgandamizo wa udongo
  • Kupanda kwa unyevu na maji
  • Sakafu kutitia kwa kiwango tofauti na Jengo.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…