PM Pinda is Too Weak For Negotiation?

PM Pinda is Too Weak For Negotiation?

Wakuu naona hata ile batuka yake kule bagamoyo haijawakosha kabisa. Au tuseme nako alitumwa tu?
 
statement yako iko too general! Lowasa alikuwa hatetereki kwenye maamuzi yake na sio kigeugeu kama mizengo pinda! Tatizo la pinda ni kutokuwa na ujasiri! Kiongozi mwingine ambaye alikuwa hatetereki na maamuzi yake ni nyerere! Wakati wa vita na idi amini dada kamuzu banda aliivamia tanzania kwa kuleta manowari na ndege za kijeshi na kudai kuwa sehemu yote ya kyela mpaka milima ya livingstone ni sehemu ya malawi! Lakini manowari zile na ndege zilitunguliwa na jwtz! Hakumwonea mtu aibu, alianzisha uhusiano mzuri sana na zambia, zimbabwe na msumbiji kiasi kwamba malawi ilijikuta isolated!

hapo mheshimiwa nikumbushe na unipe data kamili lini tanzania ilipigana na malawi, maana kumbukumbu zangu zinaniambia vita ilipiganwa na tanzania ni ile ya uganda kumpiga iddi amini dada na msumbiji (iliisaidia msumbiji kupigania uhuru na kwenye vita ya renamo )
pia ilitoa msaada kwa angola na zimbabwe.

Kuhusu waziri mkuu pinda namuona anajua kazi kuliko wengine waliomtangulia.
Kama anakwenda malawi kutatua mgogoro ni kwamba anakwenda kupresent hoja ya tanzania au kwa maana nyingine ametumwa na raisi wetu sio anakwenda na hoja yake kwahiyo sioni tatizo hapo atasimamia hoja ya raisi na baraza la mawaziri.
Na kama kutakuwa na badiliko lazima amtaarifu jk ili aidhinishe au la.
Mheshimiwa lowasa alisimamia hoja na mapendekezo ya rais wetu ben mkapa, kama unavyojua ben mkapa hataki mchezo wala masihara kwenye kutetea mambo ya kitaifa
hivyo hivyo na rais wetu jk natumaini atakuwa makini katika hili suala la malawi isitoshe jk amekuwa msaidizi wa mkapa miaka 10 kwahiyo anajua principles za mkapa na anazitumia katika kazi zake.
Na ben mkapa naye amekuwa msaidizi wa baba wa taifa kwaio alifuata principles zake.
Kwaio mambo ni kuridhishana!
 
hapo mheshimiwa nikumbushe na unipe data kamili lini tanzania ilipigana na malawi

Hii haikuwa vita hasa, ilikuwa ni chokochoko tu ambazo zilizimwa mara baada ya muda mfupi na JWTZ. Nilipata habari hizi nilipoongea na Mkuu wa Kikosi cha Anga cha JWTZ mpakani na Malawi!
 
Kuhusu waziri mkuu pinda namuona anajua kazi kuliko wengine waliomtangulia.
Kama anakwenda malawi kutatua mgogoro ni kwamba anakwenda kupresent hoja ya tanzania au kwa maana nyingine ametumwa na raisi wetu sio anakwenda na hoja yake kwahiyo sioni tatizo hapo atasimamia hoja ya raisi na baraza la mawaziri.
Na kama kutakuwa na badiliko lazima amtaarifu jk ili aidhinishe au la.

Ni kwa namna gani basi wanaojadili kuhusu mikataba ya madini na mingineyo huwa wanaingizwa mkenge? Wake up please! It is not simple like that!
 
Hilo suala linahitaji waziri wa mambo ya nje na kamatiu ndogo ya washauri wa mambo ya nje na sheria za kimataifa
 
Back
Top Bottom