jamani umeharibu kabisa j3 na nafikir wk nzima jamani lol........................ee mungu tuhurumie. siku nyingine ukieka picha mbaya kama hii unatualert jamani wengine ni wepesi wa kulia na huwa muda wote tutakaa kuaza hili tu.
jamani umeharibu kabisa j3 na nafikir wk nzima jamani lol........................ee mungu tuhurumie. siku nyingine ukieka picha mbaya kama hii unatualert jamani wengine ni wepesi wa kulia na huwa muda wote tutakaa kuaza hili tu.
Kuna kijana mmoja ambaye alifanyiwa kitendo kama hiki na mama yake miaka takriban 18 iliyopita,kwa bahati akaokotwa na wasamaria wema na kupelekwa katika kituo cha kulelea watoto yatima,aliishi pale muda mfupi akaja kupata wazazi wakufikia ambao walikuwa na na matatizo ya uzazi.Baba alikuwa raia wa ujerumani na mama raia wa Tanzania,bahati mbaya zaidi yule baba alifariki kijana akiwa bado mdogo,kilichofuatia ilikuwa wanasheria kumtafuta huyo mtoto,maana ukiacha majumba aliyoachiwa mtoto kulikuwa na makampuni yanayomiliki meli yote yakiwa kwa jina la mtoto huyo ambayo yako Ujerumani.Kwa hiyo hawa dada zetu wanaofanya vitendo kama hivi wakumbuke kuwa kuna mungu ambaye anawaangalia waja wake na kuwalipisha watendao maovu
Dah kwenye miti hakuna wajenzi. Wakati kuna watu wanatafuta watoto wengine wanawatupa. MUNGU atusaidie akina mama. Lakini inabidi ifike mahali tujadili kwa kina nini hasa sababu ya mama uliyebeba mimba kwa miezi 9 na ukajifungua kwa uchungu alafu mwisho wa siku unafikia maamuzi ya kutupa mtoto. Ewe mama/dada usibebe mimba kama haujawa tayari kuwa mama mbona kuzuia mimba iko ndani ya uwezo wetu tatizo ni nini? maana sifa kuu ya MAMA ni kumlinda mtoto wake kwenye mazingira ya aina yoyote.
Eee Mungu, mwingi wa Rehema utusamehe waja wako kwakuwa tumekundea dhambi kubwa isiyomithilika...
Roho za marehemu wapate rehema kwa mungu...wapumzike kwa amani....AMINA!!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.