Zanika
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 1,316
- 752
Kizuri chajiuza kibaya chajitembeza!
Hivyo ndivyo unavyoweza kuwaita Wapinzani wa TZ ambao ni dhahiri sasahivi akili zao zimeshikiliwa na mafisadi na walowezi wa nchi jirani ambao na wao ni Puppets wa international middleman wanaoyatumia makampuni ya huko kwao kuiba rasilimali za mataifa masikini.
Hotuba ya Mkuu wa nchi leo imewaumbua kama si kuwavua nguo. Hii ni hasa pale ilipogusia baadhi ya kauli za Marehemu Baba wa Taifa na hatua alizochukua kulinda Rasilimali za Nchi na kufanya mapinguzi ya Viwanda humu nchini.
Ninanukuu:
Baada ya miaka michache ya kupata Uhuru, Mwalimu Nyerere alitambua kuwa huwezi kupata maendeleo kama njia kuu za uzalishaji zimeshikiliwa na watu binafsi peke yake, ni lazima serikali ishiriki kikamilifu na huo ndio ukweli wenyewe.
Nchi zote zilizofanikiwa duniani, serikali zao zilishiriki moja kwa moja katika shughuli za kiuchumi hivyo aliona upo umuhimu wa kujenga misingi itayowezesha seriakali kushiriki kikamilifu na ndipo azimio la Arusha lilipozaliwa mwaka 1967.
Mbali na azimio la Arusha kuweka miiko kuwabana viongozi kujilimbikizia mali, kulisaidia kuzuia mashirika na makampuni ambayo yalitumiwa na mabepari kutorosha rasilimali zetu kwenda nje ya nchi. Serikali ikajenga viwanda na mashirika, tulikuwa na viwanda vingi na kupunguza utegemezi kutoka nje, shirika la ndege pia lilikuwa na ndege 9. Lilianzishwa shirika la nyumbalililokuwa na nyumba zaidi ya 6,000
Pia namnukuu mwalimu, alisema 'Ni vyema madini yetu tukayaacha mpaka watanzania tutakapokuwa na ufahamu wa kutosha wataamua kuyachimba' mwisho wa kunukuu."
Haya ndiyo mafisadi na Chama chao pamoja na mabwana zao wa jirani na huko ughaibuni hawataki kuyasikia.
Wameajiri puppets zaidi ya 200 kukesha na kushinda mitandaoni wakiwa wamefundishwa ugaidi wa Habari( Information terrorism) ambako wanachofanya ni kuchafua na kupotosha kwa haraka kila jema liongewalo juu ya performance ya Serikali na hususani Hotuba za Mkuu wa Nchi.
Baada ya hayo inafata press ya either Msemaji wa Chama chao au kiongozi yeyote wakwao kulingana na walivyojipanga. Huyu naye atajibu kwa vipengele vyenye nia ya kuupotosha umma na ambavyo ni vile vile vilivyoandikwa na wale 200 puppets wao wa Mtandaoni ili uonekane ni hoja toka kwa wananchi.
Kinachofata baada ya wiki moja ama moja na nusu wataibuka na tukio la kupanga lenye nia ya kuuonyesha umma Serikali haitendi haki,inawaonea,wanatafutwa nk mradi wafikishe ujumbe kuchonganisha Serikali ichukiwe na Wananchi.
Huu mimi nauita ni ugaidi tena uhujumu mbaya sana kwa kundi kama hili linalotafuta madaraka kwa kila mbinu ovu na chafu.
Watanzania msighilibiwe na hawa. Waepukeni na muwaogope kama ukoma.
Kwenu ninyi vijana mnaotumika:
Mkae mkijua mnaharibikiwa na kibaya zaidi ni mnajenga kizazi kibovu chenye unafiki na roho mbaya zenye upofu wa majibu sahihi ya Utaifa wenu. Bomu mnalotengeneza leo litawagharimu ninyi wenyewe.
Amkeni usingizini mujitambue
Hivyo ndivyo unavyoweza kuwaita Wapinzani wa TZ ambao ni dhahiri sasahivi akili zao zimeshikiliwa na mafisadi na walowezi wa nchi jirani ambao na wao ni Puppets wa international middleman wanaoyatumia makampuni ya huko kwao kuiba rasilimali za mataifa masikini.
Hotuba ya Mkuu wa nchi leo imewaumbua kama si kuwavua nguo. Hii ni hasa pale ilipogusia baadhi ya kauli za Marehemu Baba wa Taifa na hatua alizochukua kulinda Rasilimali za Nchi na kufanya mapinguzi ya Viwanda humu nchini.
Ninanukuu:
Baada ya miaka michache ya kupata Uhuru, Mwalimu Nyerere alitambua kuwa huwezi kupata maendeleo kama njia kuu za uzalishaji zimeshikiliwa na watu binafsi peke yake, ni lazima serikali ishiriki kikamilifu na huo ndio ukweli wenyewe.
Nchi zote zilizofanikiwa duniani, serikali zao zilishiriki moja kwa moja katika shughuli za kiuchumi hivyo aliona upo umuhimu wa kujenga misingi itayowezesha seriakali kushiriki kikamilifu na ndipo azimio la Arusha lilipozaliwa mwaka 1967.
Mbali na azimio la Arusha kuweka miiko kuwabana viongozi kujilimbikizia mali, kulisaidia kuzuia mashirika na makampuni ambayo yalitumiwa na mabepari kutorosha rasilimali zetu kwenda nje ya nchi. Serikali ikajenga viwanda na mashirika, tulikuwa na viwanda vingi na kupunguza utegemezi kutoka nje, shirika la ndege pia lilikuwa na ndege 9. Lilianzishwa shirika la nyumbalililokuwa na nyumba zaidi ya 6,000
Pia namnukuu mwalimu, alisema 'Ni vyema madini yetu tukayaacha mpaka watanzania tutakapokuwa na ufahamu wa kutosha wataamua kuyachimba' mwisho wa kunukuu."
Haya ndiyo mafisadi na Chama chao pamoja na mabwana zao wa jirani na huko ughaibuni hawataki kuyasikia.
Wameajiri puppets zaidi ya 200 kukesha na kushinda mitandaoni wakiwa wamefundishwa ugaidi wa Habari( Information terrorism) ambako wanachofanya ni kuchafua na kupotosha kwa haraka kila jema liongewalo juu ya performance ya Serikali na hususani Hotuba za Mkuu wa Nchi.
Baada ya hayo inafata press ya either Msemaji wa Chama chao au kiongozi yeyote wakwao kulingana na walivyojipanga. Huyu naye atajibu kwa vipengele vyenye nia ya kuupotosha umma na ambavyo ni vile vile vilivyoandikwa na wale 200 puppets wao wa Mtandaoni ili uonekane ni hoja toka kwa wananchi.
Kinachofata baada ya wiki moja ama moja na nusu wataibuka na tukio la kupanga lenye nia ya kuuonyesha umma Serikali haitendi haki,inawaonea,wanatafutwa nk mradi wafikishe ujumbe kuchonganisha Serikali ichukiwe na Wananchi.
Huu mimi nauita ni ugaidi tena uhujumu mbaya sana kwa kundi kama hili linalotafuta madaraka kwa kila mbinu ovu na chafu.
Watanzania msighilibiwe na hawa. Waepukeni na muwaogope kama ukoma.
Kwenu ninyi vijana mnaotumika:
Mkae mkijua mnaharibikiwa na kibaya zaidi ni mnajenga kizazi kibovu chenye unafiki na roho mbaya zenye upofu wa majibu sahihi ya Utaifa wenu. Bomu mnalotengeneza leo litawagharimu ninyi wenyewe.
Amkeni usingizini mujitambue
