EMT
Platinum Member
- Jan 13, 2010
- 14,483
- 15,308
Serikali inakabiliwa na hali mbaya kutokana na uhaba mkubwa wa fedha za kuendesha shughuli zake. Kutokana na hali hiyo, serikali imeziagiza wizara na taasisi zake kufunga mkanda na kuhakikisha wanabana matumizi ili angalau fedha zilizopo ziweze kumaliza mwaka huu wa fedha wa 2011/2012.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alithibitisha kuwepo kwa hali hiyo bungeni jana wakati akijibu maswali ya papo kwa papo kutoka kwa wabunge. Pinda alitoa kauli hiyo wakati akimjibu Mbunge wa Ole (CUF), Rajab Mbarouk Mohamed, aliyetaka kujua serikali inafanaya nini kupunguza makali ya maisha kwa watanzania hasa kutokana na kupanda kwa kiwango cha mfumuko wa bei.
Mohamed alihoji kama serikali imefilisika kwa kuwa Wizara na idara zake zote zimekuwa zikilalamikia ukata. Mbunge huyo alisema hali ya maisha ya Watanzania inazidi kuwa mbaya kutokana na kupanda kwa bei ya bidhaa muhimu, lakini serikali haionyeshi jitihada za makusudi kukabiliana na hali hiyo. Katika majibu yake, Pinda alikiri kuwa hali ya maisha imepanda, lakini si kwa Watanzania tu kwani hata nchi zinazoizunguka nchi hali ni hivyo hivyo.
"Tumeagiza matumizi yasiyo ya lazima yasimamishwe, tubane matumizi kwelikweli ili shughuli za serikali ziendelee kama kawaida, kweli mfumuko wa bei unapanda sana ingawa tumejitahidi kutafuta kila mbinu, lakini haitusaidii," alisema Pinda na kuongeza: "Tumejitahidi kuondoa ushuru wa sukari inayotoka nje, lakini bado haitoshi, mafuta nayo yanapanda bei kila siku hivyo tunaomba wafanyabiashara waisaidie serikali wawe waaminifu wasipandishe bei bila sababu."
Hata hivyo, Pinda alisema kuwa serikali haijafilisika. "Pamoja na hayo serikali haijafilisika kwani ingekuwa hivyo wewe usingekuwa hapa bungeni?" alihoji.
CHANZO: NIPASHE
Mijadala ya awali:
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alithibitisha kuwepo kwa hali hiyo bungeni jana wakati akijibu maswali ya papo kwa papo kutoka kwa wabunge. Pinda alitoa kauli hiyo wakati akimjibu Mbunge wa Ole (CUF), Rajab Mbarouk Mohamed, aliyetaka kujua serikali inafanaya nini kupunguza makali ya maisha kwa watanzania hasa kutokana na kupanda kwa kiwango cha mfumuko wa bei.
Mohamed alihoji kama serikali imefilisika kwa kuwa Wizara na idara zake zote zimekuwa zikilalamikia ukata. Mbunge huyo alisema hali ya maisha ya Watanzania inazidi kuwa mbaya kutokana na kupanda kwa bei ya bidhaa muhimu, lakini serikali haionyeshi jitihada za makusudi kukabiliana na hali hiyo. Katika majibu yake, Pinda alikiri kuwa hali ya maisha imepanda, lakini si kwa Watanzania tu kwani hata nchi zinazoizunguka nchi hali ni hivyo hivyo.
"Tumeagiza matumizi yasiyo ya lazima yasimamishwe, tubane matumizi kwelikweli ili shughuli za serikali ziendelee kama kawaida, kweli mfumuko wa bei unapanda sana ingawa tumejitahidi kutafuta kila mbinu, lakini haitusaidii," alisema Pinda na kuongeza: "Tumejitahidi kuondoa ushuru wa sukari inayotoka nje, lakini bado haitoshi, mafuta nayo yanapanda bei kila siku hivyo tunaomba wafanyabiashara waisaidie serikali wawe waaminifu wasipandishe bei bila sababu."
Hata hivyo, Pinda alisema kuwa serikali haijafilisika. "Pamoja na hayo serikali haijafilisika kwani ingekuwa hivyo wewe usingekuwa hapa bungeni?" alihoji.
CHANZO: NIPASHE
Mijadala ya awali: