Pinda ni zaidi ya Cleopa David Msuya

Tatizo sio Bw.Pinda au sijui Bw.Nyerere, tatizo ni jamii yetu jinsi ilivyo na jinsi inavyoangalia mambo, wewe unaweza kuwa umeona hilo ni tatizo lakini Watanzania wengi wasione tatizo liko wapi, na ndio maana wachangiaji kwenye hii mada ni wachache ikilinganishwa na kama ungeleta mada kama fulani kafumaniwa gesti, au Bw.Rizwani anunua Magomeni yote, kurasa zote zingejaa wachangiaji hasa kwenye mambo ya Ngono, lakini jambo kama hilo wengi humu hawaoni tatizo na wala haliwashtui, hivyo anayoyafanya Bw. Pinda au sijui Bw.Msuya yangefanywa na Mtanzania yoyote au Watanzania walio wengi pindi wangepata hiyo nafasi, hata Kardinali Pengo alilisema hilo, anayelia ufisadi katika jamii yetu ni kwamba hajapata hiyo nafasi, lakini akiipata atafanya yaleyale, alikuwa sahihi kabisa na hii ndio tafsiri yake!

Kwa hiyo tuendelee na lao mpaka lini? Acha kupoteza matumaini mkubwa katika kutatua matatizo. Lazima matatizo tuyatatue bila kujali gharama zate au ukubwa wake.
 
Tatizo sio Bw.Pinda au sijui Bw.Nyerere, tatizo ni jamii yetu jinsi ilivyo na jinsi inavyoangalia mambo, wewe unaweza kuwa umeona hilo ni tatizo lakini Watanzania wengi wasione tatizo liko wapi, na ndio maana wachangiaji kwenye hii mada ni wachache ikilinganishwa na kama ungeleta mada kama fulani kafumaniwa gesti, au Bw.Rizwani anunua Magomeni yote, kurasa zote zingejaa wachangiaji hasa kwenye mambo ya Ngono, lakini jambo kama hilo wengi humu hawaoni tatizo na wala haliwashtui, hivyo anayoyafanya Bw. Pinda au sijui Bw.Msuya yangefanywa na Mtanzania yoyote au Watanzania walio wengi pindi wangepata hiyo nafasi, hata Kardinali Pengo alilisema hilo, anayelia ufisadi katika jamii yetu ni kwamba hajapata hiyo nafasi, lakini akiipata atafanya yaleyale, alikuwa sahihi kabisa na hii ndio tafsiri yake!

Watu wengi hawajui kwa nini wilaya na mikoa inaanzishwa. Na pia hawa jui athari za uanzishwaji huo kiuchumi, kijamii na kisiasa.

Kiuchumi, mikoa na wilaya hizo mpya zinahitaji ofice, nyumba za wafanyakazi, magari, mawasiliano nk

Kisiasa, huo ni mpenyo wa kutafutiana ulaji wa marafiki ndugu, vimada wa wakubwa ili kushika nafasi mpya. Pia, ni njama za kuongeza viti vya kisiasa bungeni nk.

Kijamii, huwa ni mzigo kwa maendeleo ya watu. Mikoa na wilaya zilizopo zimewashinda na bado wanaongeza nyingine.

Naunga mkono wazo la kumsupport Magufuli na Mwakyembe na Muhongo. Tutumie vilivyopo ipasavyo na sio tuongeze vingine.
 
kwa hiyo ulitaka kila waziri akiingia kazi iwe kuanzisha mikoa na wilaya tu.kwani wewe ulitaka tuwe na mikoa mingapi badala ya mingapi na kwa nini?
Tanzania inahitaji mikoa isiyozidi kumi na wilaya zisizozidi miamoja. Uchumi wa Taifa hili hauna uwezo wa kubeba mikoa yote hii tulionayo na ambayo kila utawala unaokuja unaiongeza kiholela na kwa maslahi binafsi na ukabila.
 
Kwa hiyo tuendelee na lao mpaka lini? Acha kupoteza matumaini mkubwa katika kutatua matatizo. Lazima matatizo tuyatatue bila kujali gharama zate au ukubwa wake.
Mimi nimetoa tu picha halisi ya jamii yetu, hayo mengine sijui ya kupoteza matumaini sio yangu, na wala sina haja hiyo,
 
Tanzania inahitaji mikoa isiyozidi kumi na wilaya zisizozidi miamoja. Uchumi wa Taifa hili hauna uwezo wa kubeba mikoa yote hii tulionayo na ambayo kila utawala unaokuja unaiongeza kiholela na kwa maslahi binafsi na ukabila.
kwanini tusiwe na mikoa mitano na wilaya 20 ili kuokoa fedha zaidi? kwani lengo la kuwa na wilaya na mikoa ni nini?
 
Kwa hiyo tuendelee na lao mpaka lini? Acha kupoteza matumaini mkubwa katika kutatua matatizo. Lazima matatizo tuyatatue bila kujali gharama zate au ukubwa wake.
Hatutatui matatizo kwa kuongeza mikoa na wilaya wala kwa kuongeza wizara na manaibu waziri. Ndio maana unaona sasa, kuliko wakati mwingine wowote tangu tupate uhuru huduma za jamii zimeelemewa sana. Angalia huduma za elimu, afya, utoaji haki zilivyodorora. Kisa mapesa yote tumeyaelekeza kwenye huduma za kiutawala na SIASA!
 
Hatutatui matatizo kwa kuongeza mikoa na wilaya wala kwa kuongeza wizara na manaibu waziri. Ndio maana unaona sasa, kuliko wakati mwingine wowote tangu tupate uhuru huduma za jamii zimeelemewa sana. Angalia huduma za elimu, afya, utoaji haki zilivyodorora. Kisa mapesa yote tumeyaelekeza kwenye huduma za kiutawala na SIASA!

Naamanisha tupambane tu na viongozi wabinafsi bila kujali kwamba hiyo ni hulka ya kila mtu kama mchangia mmoja aliposema hapo juu kwa kutoa mfano wa maneno ya Pengo " hata Kardinali Pengo alilisema hilo, anayelia ufisadi katika jamii yetu ni kwamba hajapata hiyo nafasi, lakini akiipata atafanya yaleyale, alikuwa sahihi kabisa na hii ndio tafsiri yake!". Sikubaliani naye kwa sababu hata Manzese ambako watu hukambwa sana hakukumbwa vile. Ni tabia ya watu kuruhusu na kuzoea tabia/matukio fulani na kuyafanya ya kawaida hata kama ni ya kiovu. Tupende tusipende, ufisadi haukuwa mkubwa kiasi hiki kipindi cha Mwl. JK. Nyerere. Tukiendekeza kauli hizi basi tunakoendelea ni kubaya zaidi.
 
Zitto,
Ulikusanya sahihi kutaka huyu jamaa aondolewe Uwaziri Mkuu kwa makosa ya watu wengine. Kusanya kura zingine kumwondoa kwa namna alivyosimamia yeye mwenyewe ugawaji wa mikoa na wilaya. Marekani pamoja na ukubwa wake wote kwa kila kitu sijasikia wakiwaza kuongeza majimbo nchini mwao. Baadhi ya majimbo kule ni makubwa kuliko hata Tanzania.
 
Pamoja na mambo mengine wanarukwa tunalia mgawanyo usiosawa wa rasilimalia ardhi baina ya katavi na rukwa(mkoa mama).
Mkoa wa rukwa umegawanywa kupata katavi na utabaki na km za mraba 27,765 na wilaya 3,majimbo 4,tarafa 16,kata 64,vijiji 316,mitaa 196 na vitongoji 1658.
Katavi(mkoa mpya) una km za mraba 47,485 ikiwa na mara mbili ya rukwa,majombo 3,tarafa 10,kata 42,vijiji 124,mitaa 14 na vitongoji 671.
Ni dhahiri kuwa kuna upendeleo mkubwa wa rasilimali ardhi kwa mkoa wa katavi huku maeneo yote potentials na ya kimkakati wakichukua wao.

Niliwahi kutoa uzi hapa kuhusiana na huu upendeleo wajinga wakaubeza. kimsingi nimeshawahi kuuzunguka mkoa wa Rukwa mara kadhaa, nakujua laela, swanga, nkasi, kirando mpanda nk. huu mkoa ulikuwa nyuma sana kimaendeleo, ukiangalia tatizo kuu ilikuwa barabara, juzi tu ilikuwa unapiga vumbi toka tunduma, swanga mpaka mpanda ghafla uwanja wa ndege, mkoa, wilaya nk. ni mkoa wa rukwa mpya ambao uko choka mbaya, hapo swanga mjini ni pabaya kuliko mpanda, mpanda kuna madini kuna reli, hebu nenda Nkasi ushangae, 4 yrs ago nilienda na kukuta wilaya isiyo na umeme wala cm including mobile lkn kuna mahindi na kuna ziwa pale ni vp? Pinda badala ya kuweka mikakati ya kuokoa mkoa wake ye anapeleka mkoa kwa watu wake hasa, mara airport na sasa hadi ardhi kawabana au nyingine ndo ile kawapa wazungu wapande mibono? haya masiasa haya! that means RC, RAS, RPC, RMO nk hao wote magari, salary, malazi matibabu nk ndo pinda huyo mtoto wa mkulima mwenye mil 20 bank sijui leo anaweza kusema zimepanda au zimeshuka dah! Tz tz nakupenda kwa moyo woteee! imbaaaaa!
 
Tanzania inahitaji mikoa isiyozidi kumi na wilaya zisizozidi miamoja. Uchumi wa Taifa hili hauna uwezo wa kubeba mikoa yote hii tulionayo na ambayo kila utawala unaokuja unaiongeza kiholela na kwa maslahi binafsi na ukabila.
Mkuu, hebu rejea ahadi za Mkulu wakati wa Kampeni zake 2005 and 2010, then urudi hapa tuone kama Pinda kapinda au kapindishwa na system.
 
Mkuu, hebu rejea ahadi za Mkulu wakati wa Kampeni zake 2005 and 2010, then urudi hapa tuone kama Pinda kapinda au kapindishwa na system.
Pinda katumia UDHAIFU wa mkuu wake wa kazi na ahadi zake nyingi kufanya aliyoyafanya sasa. WaziriMkuu makini hawezi kujigawia mkoa, akajigawia wilaya na halmashauri mbili kwa mpigo. Nashukuru sijamsikia akiutaka Urais. Maajabu na miujiza ingekuwa mingi zaidi.
 
Ukweli cioni utendaji kazi wa PINDA,ni kama serikali yetu haina waziri mkuu!
 
Pinda katumia UDHAIFU wa mkuu wake wa kazi na ahadi zake nyingi kufanya aliyoyafanya sasa. WaziriMkuu makini hawezi kujigawia mkoa, akajigawia wilaya na halmashauri mbili kwa mpigo. Nashukuru sijamsikia akiutaka Urais. Maajabu na miujiza ingekuwa mingi zaidi.
Mkuu, hili swala la kugawa wilaya kijanjajanja ni mbaya sana.....Nyamagana na Ilemela ----nimekutana na watumishi wa Ilemela ambao hawana ofisi, kwahiyo wanafanya shughuli zao tu, wakiitwa kwenye mikutano na warsha na semina wanakwenda. wakirudi wanaendelea na shughuli zao za binafsi.
 
Pamoja na mambo mengine wanarukwa tunalia mgawanyo usiosawa wa rasilimalia ardhi baina ya katavi na rukwa(mkoa mama).
Mkoa wa rukwa umegawanywa kupata katavi na utabaki na km za mraba 27,765 na wilaya 3,majimbo 4,tarafa 16,kata 64,vijiji 316,mitaa 196 na vitongoji 1658.
Katavi(mkoa mpya) una km za mraba 47,485 ikiwa na mara mbili ya rukwa,majombo 3,tarafa 10,kata 42,vijiji 124,mitaa 14 na vitongoji 671.
Ni dhahiri kuwa kuna upendeleo mkubwa wa rasilimali ardhi kwa mkoa wa katavi huku maeneo yote potentials na ya kimkakati wakichukua wao.

Hee!! isije ikawa ile dhambi ya ubaguzi inaanza kuwatafuna!! kama Katavi kuna upendeleo basi hamieni huko. Hata mimi wa kilimanjaro najiandaa kuhamia huko. kwani si nchi yangu hii?
 
Mkuu, hili swala la kugawa wilaya kijanjajanja ni mbaya sana.....Nyamagana na Ilemela ----nimekutana na watumishi wa Ilemela ambao hawana ofisi, kwahiyo wanafanya shughuli zao tu, wakiitwa kwenye mikutano na warsha na semina wanakwenda. wakirudi wanaendelea na shughuli zao za binafsi.
Kila kitu NCHI hii kinafanywa KISIASA. Hauwezi kuanzisha wilaya kama vile unaoa mke wa pili. Halafu unawalazimisha maDC na wasaidizi wakae huko! Uzoefu wa Pinda serikalini haujamsaidia lolote
 
Nakumbuka kulikuwa na move ya kanisa la Mennonite na friends wa Prof. Muhongo kuanzisha Chuo Kikuu Cha Kilimo Musoma (Nyerere University of Agriculture), ghafla tukasikia Mh. Mizengo Pinda pia akielekeza nguvu Rukwa kuanzishwa chuo kikuu cha Kilimo! Nikajiuliza, alikuwa wapi mpaka Mennonite waje na hiyo idea na yeye kuidakia???
 
Mbona hamsemi juu ya mikoa mengine iliyoanzishwa wakati wake kama Njombe, Geita nk. Je huko nako ni kwake? Acheni majungu.Watu wengine kazi yao ni kulaumu tu. Na si ajabu wengi wenu mkipewa nafasi kama hizo matafanya mabaya kuliko hata hayo mnayopigia kelele. Kama ni lawama basi iwe kwa serikali yote, kwasababau maamuzi ya kuanzisha mikoa na wilya hayafanywi na mtu mmoja.
 
Wakati ule Waziri Mkuu wa zamani Msuya anasimamia kwa nguvu zake zote kuanzishwa kwa wilaya mpya ya Mwanga wengi tulimwona ni mkabila, mtu anayependelea kwao.

Waziri Mkuu wa sasa, Mizengo KP Pinda ni zaidi ya Msuya. Katika kipindi hiki kifupi tu cha uwaziri mkuu wake kaanzisha mkoa wake, KATAVI, kaanzisha na wilaya yake, MLELE, na anataka wilaya hii iwe na halmashauri mbili!

Yote haya kwa gharama ya kodi zetu WATANZANIA. Kuna wa kumzuia?

je big 3 mikoa Tanzania ni ipi?
 
uwoya
sijui kama unatambua unyeti wa rasilimali ardhi ktk maendeleo ya watu.ni dhahiri kuwa 50 years to come rukwa kutakuwa na uhaba mkubwa wa rasilimali ardhi hasa ukizingatia kuwa kuna ukuaji wa wa kidemografia na kijamii,kiuchumi ktk mkoa huo.
Pia nakubaliana na ukweli kw itafikia kipindi (miaka ya usoni) wajukuu zetu watalazimika kuhamia katavi kutafuta rasilimali ardhi.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom