Pinda, Bilali na Sitta jipimeni wenyewe

Pinda, Bilali na Sitta jipimeni wenyewe

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
16,255
Reaction score
16,185
Sikuwahi kufikiria wala kudhani kuwa kamati ya maadili akiwemo rais Kikwete ingewaona Membe, January, Asha Migiro, Magufuli na Amina walioingia 5 bora ya CCM katika kinyang'anyilo cha kumsaka mgombea Urais kupitia tiketi ya CCM ni wasafi, wachapakazi, waadilifu na waaminifu kwa taifa letu kuwazidi hata Pinda, Bilali, Sitta, Wasira, Mwakyembe, Jaji Ramadhani na Mwingulu wasaidizi na washauri wakubwa wa rais.

Binafsi niliogopa sana kuona nchi inaongozwa na watu wasioaminika kiasi hiki, lakini niliogopa zaidi kuona rais anasaidiwa na watu asiowaamini kwa kiasi hiki. Kisiki cha watendaji wake wakuu hawa kingekuwa CC, NEC na mkutano mkuu na sio kwenye ngazi ya awali ya kamati ya maadili ambayo na rais ni mjumbe wake na mdau muhimu.

Kama wasaidizi wake hao walikuwa wana mafaili machafu kwanini hakuwaambia mapema kinagaubaga ili waache kutangaza nia ili kuwaepushia kupata aibu kama waliyoipata mbele ya wananchi ya kushindwa hata na mtoto mdogo kama January Makamba kwa uadilifu? Lakini ni kweli Asha Migiro ni mchapakazi na mwaminifu kuliko Pinda, Bilali, Mwakyembe, Sitta na Wasira? kwani kafanya nini kikubwa mno kwenye taifa hili kuwazidi Bilali, Pinda, Mwakyembe, Sitta na Wasira?

Huu ni udhalilishaji wa wazee wetu hawa wakuu ambao nao Kama mzee Kingunge hawana budi kutoa neno japo moja kwa wananchi ili kusafisha makoo yao. Kitaaluma kutoa dukuduku hadharani (mental ventilation) kunaongeza afya ya mtu kuliko kunyamaza na dukuduku moyoni. Wakikaa kimya namna hii ni dalili tosha za wazi kuwa kweli ni wachafu na wasioaminika kupewa urais kama kamati yao ya maadili ilivyoona, hivyo waondoke wapishe wengine waliosafi kwa taifa.
 
Naamini muda ndio factor pekee kwa hayo uliyoyazungumza,na sidhani pia kama wao wameridhika kwa Umafia na Udhalilishaji mkubwa waliofanyiwa hasa Pinda,Bilal na Jaji Ramadhani.

Kwa viwango na vipimo vyovyote vile haiwezekani wasaidizi na watendaji wakuu wa Rasi na Nchi wakaishia kwenye kamati ya maadili then wakaingizwa watu ambao hata hawapo kwenye system.
 
Mzee kingunge sio mnafiki. Mambo ya aibu sana, yaani January ambae ni naibu waziri ni bora kuliko makamu wa rais na waziri mkuu! Hayo maajabu ni ya kikwete tu
 
Bilali kilichompoza ni kuwa team lowasa pale alipoalikwa na kumtuma Lowasa amuwakilishe ndio maana wamemnyima kuendelea na umakamu wa rais wanahisi team lowasa wangeendelea kumtumia,Sita ni kigeugeu hana msimamo hata iweje asingefikiriwa maana ndio chanzo cha migogoro ccm.Pinda ni waziri mkuu dhaifu hata yeye anajijua hivyo hakuwa na nafasi.
 
Mzee kingunge sio mnafiki. Mambo ya aibu sana, yaani January ambae ni naibu waziri ni bora kuliko makamu wa rais na waziri mkuu! Hayo maajabu ni ya kikwete tu

Ni maoni yako tu, na wala huzuiwi kuchangia na huo ndo ukomo wako wa kufikiri!
 
Utashi wa kisiasa umekosekana na ndipo haya tunayoyaona yameota mizizi sasa. Pamoja na CCM kuwa na watu wazuri ambao wangeweza kuwa hazina kiuongozi kwa nchi hii kwa kipindi kirefu kijacho, watawala wanaendesha nchi kwa fitina, kiujanjajanja, makundi, kifamilia na chuki na hapo ndipo jahazi linazama pasipo wao kushtuka.
 
January aliwekwa pale tu mlengwa alikuwa membe na migiro. Ndio mnasema ccm kuna democracy wakati mwenyekiti wenu ndie anayechagua watu??
 
Mleta hoja nakubaliana na wewe 100 %!!

Kwa kweli hii ni aibu kwa nchi pia. Haiwezekani viongozi wakuu wa nchi, wachujwe na kamati ya maadili halafu tuendelee business as usual. Only in Tanzania. Ingeonekana ni kawaida kama wangeshindwa kwa kura ila hii ya kupigwa chini na kamati ya maadili is real questionable!! Jaji Mkuu mstaafu, Spika Mstaafu, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu wapigwa chini na kamati ya maadili!!? Ni AIBU kubwa. Hii imetupa picha halisi ya Viongozi wetu kuwa siyo waadilifu!! Ingekuwa kwa wenzetu, naamini Makamu na Waziri Mkuu wangeshaamua kuachia ngazi by now .... ila Bongo, hatoki mtu hapa mpaka utolewe!!

Kwa sasa Rais yuko nje ya nchi.... kwa nini kawaachia watu asiowaamini au wasio na maadili!!? Kwa sasa inabidi awachie watu kama akina Magufuli, January au Asha Rose ndiyo wa-act ikiwa nje ya nchi.

Kwa kweli hawa watu inabidi wajipime tena kama kweli bado wanastahili kurudi walau bungeni!!
 
Kingunge kasema maneno ya kweli kabisa watu wengi walishindwa kutafakari hayo sababu walishabikia kukatwa kwa lowasa ila kimsingi mchakato haukuwa wa haki ukichukulia mfano wa lowasa kutokuwemo kwenye kinyanganyiro je wangeendesha mchakato kwa uvunjifu huu wa taratibu?

Hapa hatubishanii kukatwa kwa lowasa tunatizama haki na utaratibu wa kupata mgombea je ulifuatwa? kwa kutizama maslai ya watu wachache na chuki na fitina kwa mtu mmoja chama kimejikuta kikivunja kanuni na kuendesha mchakato kinyamela.

Leo wataona sawa lakini njia hii hii ikija tumika tena kumkata mgombea mzuri siku nyingine nivyema tusije kulalamika maana leo tumeibariki.
 
Bilali kilichompoza ni kuwa team lowasa pale alipoalikwa na kumtuma Lowasa amuwakilishe ndio maana wamemnyima kuendelea na umakamu wa rais wanahisi team lowasa wangeendelea kumtumia,Sita ni kigeugeu hana msimamo hata iweje asingefikiriwa maana ndio chanzo cha migogoro ccm.Pinda ni waziri mkuu dhaifu hata yeye anajijua hivyo hakuwa na nafasi
Kama hayo unayosema ni ya kweli iweje rais amtumie Pinda kama waziri wake mkuu kwa miaka 8 yote pamoja na udhaifu wake wote huo? Kama Bilali hafai kuwa rais kwanini hakuonywa mapema asichukue fomu, kuhangaika kutafuta wadhamini na hatimaye kurejesha fomu? walikuwa hawakutani ofisini? alipokuwa anasafiri nchi alikuwa anamuachiaje mtu asiyeaminika kiasi hiki? Pima maneno yako mkuu
 
Mleta hoja nakubaliana na wewe 100 %!!

Kwa kweli hii ni aibu kwa nchi pia. Haiwezekani viongozi wakuu wa nchi, wachujwe na kamati ya maadili halafu tuendelee business as usual. Only in Tanzania. Ingeonekana ni kawaida kama wangeshindwa kwa kura ila hii ya kupigwa chini na kamati ya maadili is real questionable!! Jaji Mkuu mstaafu, Spika Mstaafu, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu wapigwa chini na kamati ya maadili!!? Ni AIBU kubwa. Hii imetupa picha halisi ya Viongozi wetu kuwa siyo waadilifu!! Ingekuwa kwa wenzetu, naamini Makamu na Waziri Mkuu wangeshaamua kuachia ngazi by now .... ila Bongo, hatoki mtu hapa mpaka utolewe!!

Kwa sasa Rais yuko nje ya nchi.... kwa nini kawaachia watu asiowaamini au wasio na maadili!!? Kwa sasa inabidi awachie watu kama akina Magufuli, January au Asha Rose ndiyo wa-act ikiwa nje ya nchi.

Kwa kweli hawa watu inabidi wajipime tena kama kweli bado wanastahili kurudi walau bungeni!!
Tatizo letu hapa hata urais ni ajira, hawawezi kuacha ajira zao, kwa nchi nyingine uongozi ni huduma tu sio ajira
 
kwa nini wawe makam na wazir mkuu kama hayo uliyoyasema ndo uharisia wao mbona kikwete asingewatimua au asingewashaur waache kugombea
 
inasaidia kuondoa maumivu. nadhani nyie mmeumia zaidi kuliko hao wazee. kwa idadi yao, lazima vigogo wangekatwa tu. hamna namna wala chuki mnazojaribu kuzipandikiza hazilisaidii Taifa hili wala kizazi hichi wala kizazi kijacho. Asiyeridhika ahame chama.
 
Hicho "KITENGO" Tume ya maadili ni tranparent kiasi gani?Hawa King maker ni wasafi kiasi gani.Labda ni malaika yaani watu wasio hai au watoto wadogo! Au ni matakwa ya Malkia CLEOPATRA?
 
inasaidia kuondoa maumivu. nadhani nyie mmeumia zaidi kuliko hao wazee. kwa idadi yao, lazima vigogo wangekatwa tu. hamna namna wala chuki mnazojaribu kuzipandikiza hazilisaidii Taifa hili wala kizazi hichi wala kizazi kijacho. Asiyeridhika ahame chama.
Huna hoja kaa chini wewe, kwani hiyo kazi ya kuwakata ingefanywa na wajumbe kwenye ngazi za CC, NEC na mkutano mkuu kusingekuwa na chembe ya ubishi wala hoja na wala uzi huu usingeletwa hapa. Tatizo ni pale mwenyekiti kucheka na kunywa na watu asiokuwa na imani nao kwa miaka 5, 8 na wengine hadi 10 bila kuwatonya madhaifu yao na kusubiri hadi wakati huu wa kumsaka mgombea urais mpya. It is too late to the entire nation
 
Jamani lazima tutambue ili kuwa Rais ni zaidi ya uadilifu tu.
Ni kweli uadiiifu wa Pinda, Bilali na hao wengine hauna shaka. Lakini Je kama CCM ikiwasimamisha hao nini nafasi yao ya ushindi?

kwa mtazamo wangu CCM ina nafasi kubwa kupitia Magufuli kuliko kupitia Pinda au Bilali.

Pia ukiangaia utendaji wao katika nafasi zao leo, are they Presidential materials? To me NO

Rais must be a tough and aggressive guy like Magufuli and not too soft character.
 
Jamani lazima tutambue ili kuwa Rais ni zaidi ya uadilifu tu.
Ni kweli uadiiifu wa Pinda, Bilali na hao wengine hauna shaka. Lakini Je kama CCM ikiwasimamisha hao nini nafasi yao ya ushindi?

kwa mtazamo wangu CCM ina nafasi kubwa kupitia Magufuli kuliko kupitia Pinda au Bilali.

Pia ukiangaia utendaji wao katika nafasi zao leo, are they Presidential materials? To me NO

Rais must be a tough and aggressive guy like Magufuli and not too soft character.

Soma mada vizuri afu rudia kucoment
 
Jamani lazima tutambue ili kuwa Rais ni zaidi ya uadilifu tu.
Ni kweli uadiiifu wa Pinda, Bilali na hao wengine hauna shaka. Lakini Je kama CCM ikiwasimamisha hao nini nafasi yao ya ushindi?

kwa mtazamo wangu CCM ina nafasi kubwa kupitia Magufuli kuliko kupitia Pinda au Bilali.

Pia ukiangaia utendaji wao katika nafasi zao leo, are they Presidential materials? To me NO

Rais must be a tough and aggressive guy like Magufuli and not too soft character.

Sawa, lakini nchi hii ni yetu wote, wananchi ndio wanayemjua aina ya rais wanayemtaka awaongoze, na wananchi wanaongea kupitia wajumbe wao wa vikao waliowachagua wao, hivyo wawakilishi wa wananchi ni wale wajumbe wote wa cc, nec na mkutano mkuu na sio kamati ya maadili, maana hii kamati haijawekwa na wanachama wala wananchi pale kwa njia ya kura, hivyo kuwaamulia wananchi mtu safi sio sawa.
 
Back
Top Bottom