dosama
JF-Expert Member
- Dec 25, 2010
- 912
- 957
ZIARA iliyofanywa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda katika Wilaya ya Maswa mkoani Simiyu, imezua tafrani jana baada ya Mbunge wa Viti Maalum, Rose Kamili (CHADEMA), kudai kuwa Mkuu wa Wilaya hiyo aliwakamata na kuwaweka ndani watendaji wa vijiji kwa kushindwa kutoa mbuzi kama zawadi kwa waziri huyo.
Wakati akiuliza swali bungeni, bila kutaja jina, Kamili alisema mkuu huyo wa wilaya alifanya hivyo, baada ya watendaji hao kushindwa kuchangia mbuzi tisa kwa Waziri Mkuu, aliyefanya ziara mkoani humo Februari 23, mwaka huu.
Hata hivyo, aliyekuwa mkuu wa wilaya wakati huo, ni Kapteni mstaafu, James Yamungu ambaye kwa sasa amehamishiwa Wilaya ya Serengeti, mkoani Mara.
Swali la mbunge huyo lilimfanya Waziri Pinda, kuduwaa huku akiwa ameshika tama, na kuzua minong'ono na miguno kutoka kwa wabunge wengi.
"Mheshimiwa Spika, ninahitaji ufafanuzi wa kisheria kwa hili la baadhi ya ma-DC, ambapo huwaagiza watendaji kufanya mambo kinyume cha sheria na pindi wasipofanya huwaweka ndani kwa muda wa siku saba.
"Na mfano halisi ni hili lililotokea wilayani Maswa, katika ziara ya Waziri Mkuu Februari mwaka huu, katika Mkoa wa Shinyanga, ambapo mkuu huyo wa wilaya aliwaweka ndani watendaji wa kata kwa kushindwa kukusanya mbuzi tisa kwa ajili ya zawadi kwa Waziri Mkuu."
Swali hili lilimfanya Spika wa Bunge, Anne Makinda, kumtaka mbunge huyo kuthibitisha kwa ushahidi kutokana na jambo hilo kugusa hisia kali kwa Bunge na taifa kwa ujumla, hivyo kutaka kuleta ushahidi.
Mbunge huyo alisema kuwa anao ushahidi, na kwamba hata jambo hilo lilitangazwa na baadhi ya runinga hapa nchini, hoja ambayo hata hivyo ilionekana kuwa nyepesi kiasi cha Spika Makinda, kuwataka wabunge kuwa makini katika maswali na hoja wanazozitoa bungeni.
Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa TAMISEMI, Aggrey Mwanri, alisema serikali haijawahi kumwagiza mtendaji yeyote wa serikali kuchangisha wananchi kwa nguvu katika ziara za viongozi wa juu wa serikali.
Hata hivyo, alisema hoja ya mbunge huyo si ngeni kwani iliwahi kuibuliwa na ikamlazimu aliyekuwa Waziri wa Tamisemi, George Mkuchika, kwenda hadi Maswa kuzungumza na wananchi ili kupata maelezo ya kina.
"Baada ya kufanya mkutano na wananchi hao, ilibainika kwamba si la kweli. Lakini kama mbunge ana ushahidi mpya tunamuomba atuletee na huyo DC tutamshughulikia kwa mujibu wa sheria," alisema Mwanri.
Alifafanua kuwa wakuu wa mikoa na wilaya wana haki ya kuingilia kati utendaji wa ngazi za chini, zikiwemo halmashauri, ikiwa tu kuna hatari ya usalama ama mali ya taifa, vinginevyo hawaruhusiwi kuzuia ama kutoa maelezo mengine nje ya maamuzi sahihi ya kisera na kikanuni yaliyoamriwa na mamlaka za halmashauri za miji ama vijiji.
"Majukumu ya Mkuu wa Wilaya yametajwa katika kifungu namba 14, 1 hadi 3 cha sheria za Serikali za Mikoa namba 19 ya mwaka 1997 kwamba yeye ndiye msimamizi mkuu wa serikali katika wilaya yake.
Concern
Hapo ni waziri mkuu je na rais huwa inakuwaje
Wakati akiuliza swali bungeni, bila kutaja jina, Kamili alisema mkuu huyo wa wilaya alifanya hivyo, baada ya watendaji hao kushindwa kuchangia mbuzi tisa kwa Waziri Mkuu, aliyefanya ziara mkoani humo Februari 23, mwaka huu.
Hata hivyo, aliyekuwa mkuu wa wilaya wakati huo, ni Kapteni mstaafu, James Yamungu ambaye kwa sasa amehamishiwa Wilaya ya Serengeti, mkoani Mara.
Swali la mbunge huyo lilimfanya Waziri Pinda, kuduwaa huku akiwa ameshika tama, na kuzua minong'ono na miguno kutoka kwa wabunge wengi.
"Mheshimiwa Spika, ninahitaji ufafanuzi wa kisheria kwa hili la baadhi ya ma-DC, ambapo huwaagiza watendaji kufanya mambo kinyume cha sheria na pindi wasipofanya huwaweka ndani kwa muda wa siku saba.
"Na mfano halisi ni hili lililotokea wilayani Maswa, katika ziara ya Waziri Mkuu Februari mwaka huu, katika Mkoa wa Shinyanga, ambapo mkuu huyo wa wilaya aliwaweka ndani watendaji wa kata kwa kushindwa kukusanya mbuzi tisa kwa ajili ya zawadi kwa Waziri Mkuu."
Swali hili lilimfanya Spika wa Bunge, Anne Makinda, kumtaka mbunge huyo kuthibitisha kwa ushahidi kutokana na jambo hilo kugusa hisia kali kwa Bunge na taifa kwa ujumla, hivyo kutaka kuleta ushahidi.
Mbunge huyo alisema kuwa anao ushahidi, na kwamba hata jambo hilo lilitangazwa na baadhi ya runinga hapa nchini, hoja ambayo hata hivyo ilionekana kuwa nyepesi kiasi cha Spika Makinda, kuwataka wabunge kuwa makini katika maswali na hoja wanazozitoa bungeni.
Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa TAMISEMI, Aggrey Mwanri, alisema serikali haijawahi kumwagiza mtendaji yeyote wa serikali kuchangisha wananchi kwa nguvu katika ziara za viongozi wa juu wa serikali.
Hata hivyo, alisema hoja ya mbunge huyo si ngeni kwani iliwahi kuibuliwa na ikamlazimu aliyekuwa Waziri wa Tamisemi, George Mkuchika, kwenda hadi Maswa kuzungumza na wananchi ili kupata maelezo ya kina.
"Baada ya kufanya mkutano na wananchi hao, ilibainika kwamba si la kweli. Lakini kama mbunge ana ushahidi mpya tunamuomba atuletee na huyo DC tutamshughulikia kwa mujibu wa sheria," alisema Mwanri.
Alifafanua kuwa wakuu wa mikoa na wilaya wana haki ya kuingilia kati utendaji wa ngazi za chini, zikiwemo halmashauri, ikiwa tu kuna hatari ya usalama ama mali ya taifa, vinginevyo hawaruhusiwi kuzuia ama kutoa maelezo mengine nje ya maamuzi sahihi ya kisera na kikanuni yaliyoamriwa na mamlaka za halmashauri za miji ama vijiji.
"Majukumu ya Mkuu wa Wilaya yametajwa katika kifungu namba 14, 1 hadi 3 cha sheria za Serikali za Mikoa namba 19 ya mwaka 1997 kwamba yeye ndiye msimamizi mkuu wa serikali katika wilaya yake.
Concern
Hapo ni waziri mkuu je na rais huwa inakuwaje