ktk nchi zenye mirengo ya kijamaa hio ni kawaida yao, ukitaka kuendelea lazima ushirikiane na nchi za kibepari hata huyo china ndiko anakotengenezea pesa, kama kuna mkataba kwanini asishitakiwe? ndio maana Trump hacheki naoWakati Pm hakukumbuka hilo. Yuko nyuma huyu mzee kuna bima za mazao kabisa. Benki zitafilisika zote. Utaratibu wa mashamba na kilimo chenyewe na hasa masoko lazima uzingatiwe.
Mimi ni mkulima sitosahau serikali ilipotangaza imepata soko kubwa la mihogo china ambalo hatuliwezi.
Tulipolima tu mchina kabadili mkataba akasema hanunui muhogo mibichi tena ila mikavu. Na hiyo mikavu iwe imekatwa silesi silesi na bei ikashuka toka 1,060/= kwa kg 1 mpaka tshs 280/= kwa kilo mkavu. Ni ktk awamu ya 5 hii. Hizo habari sio mara ya kwanza kusikia.
Alichosaidia ni kuufuata mzigo shambani.
Hiyo ilikuwa ni mwaka 2018. Hatusikii tena soko la mihogo la china.
Labda wawakopeshe watu wa korosho huko wamezoea kukopeshana.