Wakudadavuwa
JF-Expert Member
- Feb 17, 2016
- 17,506
- 15,997
Ndugu zangu,
Wenye kumbukukumbu sawa mtakumbuka siku Lowassa anachukua fomu kugombea urais kwa tiketi ya Chadema kwa kuzidiwa na furaha ndugu Freeman Mbowe alizimia/ alipoteza fahamu na kulazwa hospitali ya Muhimbili, alipozinduka alikiri kuwa Lowassa ni ''mwanamabadiliko'' wa kweli. Siku za karibuni baada ya Edward Lowassa kuondoka CHADEMA anasema alikuwa mzigo.
Tundu Lissu, ghafla aliongoza wafuasi wa CHADEMA kutoa matusi kwa aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chadema na mwalimu wake wa siasa Dr.Wilbroad Slaa. Zaidi, akajimilikisha ''utunzi wa orodha ya mafisadi'' akaenda mbali zaidi akasema kwa mujibu ujuzi wake kisheria kajiridhisha pasi na shaka kuwa EL alisingiziwa,alitegwa na hivyo akatangaza msamaha.
Ili kutilia mkazo hoja yake akasema kwa mujibu wa ripoti za utafiti wa ''wazungu'' EL ndiye anapendwa zaidi, hivyo wao hawaangalii tena maadili,uchapa kazi n.k wanazingatia taarifa za wazungu.
Siku za hivi karibuni kumekuwa na vijembe na kejeli nyingi kwa wanaoondokka CHADEMA pasipo na kukiri makosa na kutubu kwa wananchi.
Wananchi si wajinga, wengi ukiwauliza sasa hivi wanakwambia ''hao wote ni CCM tu, ulaghai umezidi.
Kama mtapuuza kutoa tamko rasmi la kuomba msamaha wananchi kwa ulaghai mliofanya mwaka 2015 anguko liko palepale. Niwakumbushe tu, hata Mrema alikuwa na wafuasi wengi sana kiasi cha kusukuma gari lake lakini leo hana ushawishi.
Wenye kumbukukumbu sawa mtakumbuka siku Lowassa anachukua fomu kugombea urais kwa tiketi ya Chadema kwa kuzidiwa na furaha ndugu Freeman Mbowe alizimia/ alipoteza fahamu na kulazwa hospitali ya Muhimbili, alipozinduka alikiri kuwa Lowassa ni ''mwanamabadiliko'' wa kweli. Siku za karibuni baada ya Edward Lowassa kuondoka CHADEMA anasema alikuwa mzigo.
Tundu Lissu, ghafla aliongoza wafuasi wa CHADEMA kutoa matusi kwa aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chadema na mwalimu wake wa siasa Dr.Wilbroad Slaa. Zaidi, akajimilikisha ''utunzi wa orodha ya mafisadi'' akaenda mbali zaidi akasema kwa mujibu ujuzi wake kisheria kajiridhisha pasi na shaka kuwa EL alisingiziwa,alitegwa na hivyo akatangaza msamaha.
Ili kutilia mkazo hoja yake akasema kwa mujibu wa ripoti za utafiti wa ''wazungu'' EL ndiye anapendwa zaidi, hivyo wao hawaangalii tena maadili,uchapa kazi n.k wanazingatia taarifa za wazungu.
Siku za hivi karibuni kumekuwa na vijembe na kejeli nyingi kwa wanaoondokka CHADEMA pasipo na kukiri makosa na kutubu kwa wananchi.
Wananchi si wajinga, wengi ukiwauliza sasa hivi wanakwambia ''hao wote ni CCM tu, ulaghai umezidi.
Kama mtapuuza kutoa tamko rasmi la kuomba msamaha wananchi kwa ulaghai mliofanya mwaka 2015 anguko liko palepale. Niwakumbushe tu, hata Mrema alikuwa na wafuasi wengi sana kiasi cha kusukuma gari lake lakini leo hana ushawishi.