Picha zinatisha: Mlinzi wa Hifadhi ya Taifa ya Tarangire avamiwa na kujeruhiwa na simba

chakii

JF-Expert Member
Sep 15, 2013
19,696
22,729
index.jpeg

IMG-20170427-WA0023.jpg
IMG-20170427-WA0011.jpg

Mwenyezi Mungu msaidie apone mapema.

=======
Mmiliki wa kambi amzungumzia simba aliyejeruhi

Kwa ufupi

Loyani amejeruhiwa maeneo mbalimbali ya mwili ikiwa ni pamoja na kunyofolewa sikio na kuvunjwa taya.

Mmiliki wa Kambi ya Utalii ya Maramboi, Wilbard Chambulo amezungumzia mkasa wa mfanyakazi wake Kilopa Loyani (46) kushambuliwa na simba na kujeruhiwa.

Loyani amejeruhiwa maeneo mbalimbali ya mwili ikiwa ni pamoja na kunyofolewa sikio na kuvunjwa taya.

Akizungumza na gazeti hili jana, Chambulo alisema Aprili 22 saa tisa usiku, akiwa amelala kwenye hema kambini hapo aliamshwa na sauti ya kelele za kuomba msaada kutoka kwa Loyani ambaye ni mlinzi.

“Nilishtuka nikawasha taa kabla ya kuzima kwa sababu ya usalama, baadaye niliitwa kwa radio call na askari wa Tarangire. Mlinzi huyo alikuwa kwenye korido ya nyumba ya wageni iitwayo Simba, ndipo alipovamiwa na alipiga kelele kuomba msaada,” alisema.

“Kwenye korido alikuwa na mwenzake ambaye alimsaidia kupiga kelele, tulifika kumuokoa tukawaona simba watatu, mmoja dume na majike mawili. Hatukuweza kuwafanya chochote kutokana na sheria, badala yake nilichukua gari na kumpeleka mgonjwa hospitali.”

Alisema mlinzi huyo amejeruhiwa upande mmoja wa uso na sikio la kushoto lilinyofolewa na pia alivunjwa taya.

Chambulo alisema walimfikisha Loyani katika Hospitali ya Karatu alikopatiwa huduma ya kwanza ikiwa ni pamoja na kuongezwa damu na baadaye alipelekwa Hospitali ya Rufaa ya KCMC mkoani Kilimanjaro.

“Amelazwa KCMC na amefanyiwa upasuaji mara mbili kwenye taya. Nashukuru hali yake inaendelea vyema kwa sababu kuna wakati anazungumza,” alisema mmiliki huyo wa kambi ya utalii.

Chambulo alisema tukio hilo ni la kwanza kutokea kwenye kambi hiyo na aliziomba mamlaka husika kuchukua hatua ya kuzuia madhara kwa watu kwa kudhibiti wanyama wakali wakiwamo simba.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Minjingu ilipo kambi hiyo, Bariki Kisiri alisema hilo ni tukio la kwanza kijijini hapo lakini ana taarifa kuwa kuna mtu aliuawa na simba mwezi uliopita kwenye Kijiji cha Vilima Vitatu kilichopo jirani.

“Shambulio hilo ni la kwanza kutokea katika kijiji changu, lakini nina taarifa kuwa kijiji cha jirani kuna mtu aliuawa mwezi uliopita, tumetoa taarifa kwenye Idara ya Wanyamapori bado hatua hazijachukuliwa,” alisema.

Chanzo: Mwananchi
 
Weka Picha Weka Kivuli Sehemu yenye damu mkubwa tupate uhalisia kidogo....Nina Mashaka kidogo akiwa na mwanafunzi wake,kwani field ameenda na mwanafunzi mmoja tu? Halafu ukiwa na mawazo ya kufanya mambo flani akili huwa zinapotea haujali porini kuna simba au lah,ebu weka picha tuone jinsia zao kwanza tusije bashiri hovyo.
 
Weka Picha Weka Kivuli Sehemu yenye damu mkubwa tupate uhalisia kidogo....Nina Mashaka kidogo akiwa na mwanafunzi wake,kwani field ameenda na mwanafunzi mmoja tu? Halafu ukiwa na mawazo ya kufanya mambo flani akili huwa zinapotea haujali porini kuna simba au lah,ebu weka picha tuone jinsia zao kwanza tusije bashiri hovyo.
Mkuu ungetulia kidogo kuisoma habari vizuri! kwanini aongope na hakusema alikwenda na mwanafunzi bali wanafunzi.
 
Weka Picha Weka Kivuli Sehemu yenye damu mkubwa tupate uhalisia kidogo....Nina Mashaka kidogo akiwa na mwanafunzi wake,kwani field ameenda na mwanafunzi mmoja tu? Halafu ukiwa na mawazo ya kufanya mambo flani akili huwa zinapotea haujali porini kuna simba au lah,ebu weka picha tuone jinsia zao kwanza tusije bashiri hovyo.
3b4ce6a79ccd9cb34d3316f68d69d134.jpg
 
Back
Top Bottom