Picha zikionesha stesheni za reli ya kisasa - SGR zikiwa mbioni kukamilika

Tanzania Railways Corp

JF-Expert Member
Mar 23, 2018
251
595
Picha hizi zinaonesha Maendeleo ya Ujenzi wa Stesheni za Dar es Salaam, Pugu na Soga. Katika kipande cha kwanza cha Mradi wa Ujenzi wa Reli ya Kisasa - SGR ambao utakuwa na jumla ya Stesheni Sita ikiwemo Stesheni kuu mbili ambazo ni Dar es Salaam na Morogoro huku Stesheni ndogo (za kati) zikiwa ni Pugu, Soga, Ruvu na Ngerengere. Wastani wa Jumla wa Maendeleo ya Mradi Dar es Salaam - Morogoro ni zaidi ya 73%

DSC_0274 (2).JPG


Jengo la Stesheni ya Reli ya Kisasa ya Dar es Salaam likiwa limeanza kuwekwa vioo.
Jengo la Stesheni ya Dar es Salaam limejengwa kwa muonekano wa Madini ya Tanzanite ambayo upatikanaji wake ni adimu, madini haya hupatikana Tanzania pekee.

DSC_0283.JPG
DSC_0288.JPG

Muonekano wa Jengo la Stesheni ya Reli ya Kisasa ya Pugu, ambayo ujenzi wake umefika 80%

DSC_0334.JPG

Moja kati ya Vituo vya kupokea, kupoza na kusambaza umeme utakaoendesha treni za Umeme eneo la Mpiji, kikiwa katika hatua za mwisho kuweza kukamilika.
DSC_0357 (2).JPG
DSC_0355.JPG
DSC_0447.JPG
DSC_0434.JPG
DSC_0380.JPG
DSC_0387.JPG
DSC_0378.JPG

PICHA; Muonekano tofauti wa Stesheni ya Pugu ambayo ujenzi wake umekamilika kwa 90%.
Majengo ya Stesheni za Pugu, Soga, Ruvu, Ngerengere ni ya kufanana yakiwa yamejengwa kiusanifu kuakisi Vazi la Kilemba ambalo ni maarufu kwa wanawake hapa Tanzania.
 
Inavutia kweli kweli, naona kama Coat of Arm kwa hiyo stesheni ndogo hivi.

Haya ndio matunda na juhudi za wananchi katika kufanya kazi.
 
[@Tanzania Railways Corp,
hizi images zinanikumbusha mbali sana enzi hizo wakati TAZARA inajengwa. ilikuwa na muonekano wa hivi hivi. sijui TAZARA sasa imeishia wapi masikini?

nachomaanisha hapa ni kuwa hii si mara ya kwanza kwa Tanzania kujenga reli ya SGR kwa kiwango hiki cha sasa. kwa sisi tuliozaliwa before 60s huko tulishuhudia kwa macho yetu.

swali ni je, tumejifunza makosa tuliyoyafanya kwa TAZARA? kwa matumaini tuliyokuwa nayo kwa TAZARA na kile tulichokipata, my verdict is "TAZARA is one big white elephant". should we now brace ourselves up for another (this time TRC's championed) white elephant?

your guess is as good as anyone's!!
 
Kazi nzuri , lakini sasa kama reli itaachwa wazi hivo bila kuzungushia chochote kuzuia watu wasifike relini kirahisi , basi tujiandae pia kwa misibia isiyokwisha .

Kweli kabisa kama tumeamua hela ziongezwe kuweka fences za kuzuia mifugo na watu pia katika maeneo ya makazi
Hiyo inasaidia hata uhujumu pia


Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Tukipongeza pokea pongezi kiroho safi, ikitokea mkaonyeshwa madhaifu baadhi ya viongozi wasikurupuke eti ni uhalifu. Nchi hii ni yetu sote, tushiriki kuijenga. Hongera TRC.
 
Tukipongeza pokea pongezi kiroho safi, ikitokea mkaonyeshwa madhaifu baadhi ya viongozi wasikurupuke eti ni uhalifu. Nchi hii ni yetu sote, tushiriki kuijenga. Hongera TRC.
 
M-mbabe,
ukishanyanyua silaha na kuingia vitani haipaswi kusema tena tumeingia hii vita kimakosa hapanaaa.. hapo ni mapambano kwa kwenda mbele mpaka tushinde. i love my tanzania
 
M-mbabe, Tazara inakufa kwa sababu inaendeshwa na nchi mbili, na hilo lilikuwa kosa toka mwanzo, na nadhani hizi nchi mbili zimejikuta zikiwa na mawazo tofauti kuhusu uendeshaji wa tazara.

Ili tazara ifanikiwe, kwa mawazo yangu, inatakiwa kila nchi ibaki kumanage kipande chake, tukifanya hivyo tunaweza kuwa na bonge la dry port tunduma na wakongo, wazambia wamalawi wkaja kuchukulia mizigo yao hapo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom