warumi
R I P
- May 6, 2013
- 16,213
- 18,455
Staa wa sinema za Kibongo, Jacqueline Wolper Massawe ameibua maswali kwa mashuhuda walimuona live akiingia kwenye hekalu la watu wa Jamii ya Siri (Secret Society ) ya Freemasons yenye nguvu duniani inayohusishwa na imani za kishetani .
TUJIUNGE MTAA WA SOKOINE
Tukio hilo lililoibua kizaazaa kwa mashuhuda waliomuona Wolper , lilijiri juzikati, mishale ya jioni kwenye hekalu hilo lililopo Mtaa wa Sokoine mkabala na Hoteli ya Hyatt Regency , The Kilimanjaro jijini Dar jirani na Benki Kuu ya Tanzania ( BoT).
SIMU ZAMIMINIKA
Likiwa kwenye majukumu ya kusaka habari kama kawaida yake , gazeti hili lilipokea simu kadhaa kutoka kwa mashuhuda hao wakiwataka wanahabari wetu kuwahi eneo la tukio .
Kufuatia umbali waliokuwa mapaparazi wetu , ilibidi kuwaomba mashuhuda hao kumfotoa picha ambapo mmoja wao alifanya hivyo na kuziwasilisha kwenye meza ya gazeti hili.
. ..akitoka .
ALINASWAJE?
Akidadavua mazingira aliyonaswa Wolper , shuhuda huyo alikuwa na haya ya kusema :
Kwanza mwanzoni hatukumjua kama ni Wolper lakini kuna dada ambaye anamjua vizuri na ni shabiki wake mkubwa ndiye aliyetuhakikishia kuwa ni Jacqueline (Wolper ).
Kuna waliomuona akiingia . Nilipofika mimi nilimkuta getini anatoka . Walisema hakukaa muda mrefu kwani alitumia dakika kadhaa kisha akatoka na kwenda kwenye gari lake aina ya Prado (Toyota ) alilopaki mbali kidogo na lango hilo , alisema shuhuda huyo kwa sharti la kutotajwa jina na kuongeza :
Baada ya hapo alitoka nduki maana nzi ( watu) walikuwa wameanza kumjalia na kulizingira gari lake.
WOLPER AJITETEA
Baada ya kuzikagua picha za Wolper akiwa katika mazingira hayo na kujiridhisha kuwa ni yeye, gazeti hili lilimbana mwigizaji huyo ambapo alijitetea :
... a kiwa getini .
Jamani nilikuwa sina hili wala lile . Kuna jengo nilikuwa nalitafuta ndiyo nikajikuta nimetokea maeneo hayo .
Mimi mwenyewe nilishtuka kuona watu wananiangalia sana kumbe ndiyo nikagundua nipo kwenye lango la Freemasons.
Risasi Jumamosi : Mbona kuna mashuhuda walikuona wakati unaingia na wakati unatoka ?
Wolper : Unajua mimi sikuona kibao chao lakini sikuingia kabisa hadi kule ndani .
Risasi Jumamosi : Lakini kuna madai kwamba wewe ni mwanachama . Unasemaje?
Wolper : Mimi siyo Freemasons, nakumbuka kuna siku watu walinifuata wakaniambia nijiunge Freemasons nitakuwa na mafanikio lakini sijakubaliana nao .
TUJIUNGE MTAA WA SOKOINE
Tukio hilo lililoibua kizaazaa kwa mashuhuda waliomuona Wolper , lilijiri juzikati, mishale ya jioni kwenye hekalu hilo lililopo Mtaa wa Sokoine mkabala na Hoteli ya Hyatt Regency , The Kilimanjaro jijini Dar jirani na Benki Kuu ya Tanzania ( BoT).
SIMU ZAMIMINIKA
Likiwa kwenye majukumu ya kusaka habari kama kawaida yake , gazeti hili lilipokea simu kadhaa kutoka kwa mashuhuda hao wakiwataka wanahabari wetu kuwahi eneo la tukio .
Kufuatia umbali waliokuwa mapaparazi wetu , ilibidi kuwaomba mashuhuda hao kumfotoa picha ambapo mmoja wao alifanya hivyo na kuziwasilisha kwenye meza ya gazeti hili.
. ..akitoka .
ALINASWAJE?
Akidadavua mazingira aliyonaswa Wolper , shuhuda huyo alikuwa na haya ya kusema :
Kwanza mwanzoni hatukumjua kama ni Wolper lakini kuna dada ambaye anamjua vizuri na ni shabiki wake mkubwa ndiye aliyetuhakikishia kuwa ni Jacqueline (Wolper ).
Kuna waliomuona akiingia . Nilipofika mimi nilimkuta getini anatoka . Walisema hakukaa muda mrefu kwani alitumia dakika kadhaa kisha akatoka na kwenda kwenye gari lake aina ya Prado (Toyota ) alilopaki mbali kidogo na lango hilo , alisema shuhuda huyo kwa sharti la kutotajwa jina na kuongeza :
Baada ya hapo alitoka nduki maana nzi ( watu) walikuwa wameanza kumjalia na kulizingira gari lake.
WOLPER AJITETEA
Baada ya kuzikagua picha za Wolper akiwa katika mazingira hayo na kujiridhisha kuwa ni yeye, gazeti hili lilimbana mwigizaji huyo ambapo alijitetea :
... a kiwa getini .
Jamani nilikuwa sina hili wala lile . Kuna jengo nilikuwa nalitafuta ndiyo nikajikuta nimetokea maeneo hayo .
Mimi mwenyewe nilishtuka kuona watu wananiangalia sana kumbe ndiyo nikagundua nipo kwenye lango la Freemasons.
Risasi Jumamosi : Mbona kuna mashuhuda walikuona wakati unaingia na wakati unatoka ?
Wolper : Unajua mimi sikuona kibao chao lakini sikuingia kabisa hadi kule ndani .
Risasi Jumamosi : Lakini kuna madai kwamba wewe ni mwanachama . Unasemaje?
Wolper : Mimi siyo Freemasons, nakumbuka kuna siku watu walinifuata wakaniambia nijiunge Freemasons nitakuwa na mafanikio lakini sijakubaliana nao .