Nakubaliana na wewe lakini nataka watanzania wajue yeye nu mmoja hawezi peke take ututoa tulipo kwenda anapotaka twende, nashauri tumuunge mkono kwa kufanya nae kazi,MATARAJIO YANGU KWA JOHN POMBE MAGUFULI
Baada ya kuapisha kuwa Rais wa awamu ya tano ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 05.11.2015 (10:49 A.M), mimi kama raia wa Tanzania nina matarajio yafuatayo kwa Mh. Dr.John Pombe Magufuli.
? Kutatua haraka tatizo la Zanzibar lililotokana na ZEC kufuta uchaguzi pasipo na sababu za Kimsingi.Hii ni hatari kwa mustakabali wa Taifa na Wananchi wake.
? Kuwaunganisha Watanzania ambao wametofautiana kutokana na Vyama vya siasa kuwagawa kwa misingi ya itikadi za vyama,dini,makabila na ukanda wakati wa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba,25,2015.Makovu haya ni mengi na kwa watu wote sehemu zote.
? Kuinua ari ya uwajibikaji na uchapakazi Serikalini na watu binafsi na Viongozi wote watakaozembea wawajibishwe mara moja.
? Kuboresha huduma za afya katika Hospitali zote nchini na Zahanati na kuepuka Viongozi kwenda kutibiwa nje ya nchi.
? Kuhakikisha kila anayepaswa kupata elimu anaipata na hatimaye kufuta ujinga ambao umekithiri sana hivi karibuni.(Rejea kura nyingi kuharibika)
? Kuwashughulikia wote waliohusika na watakaohusika na rushwa (Matumizi mabaya ya Ofisi na mali za Umma kwa manufaa yao binafsi)
? Kuboresha Viwanda vilivyokuwepo kwa kuvipatia ruzuku na kuondoa mlolongo wa kodi na michango ambayo badala ya kuviendeleza huviumiza zaidi.
? Utatuzi wa matatizo ya wakulima uwe wa kweli na wenye tija.Matatizo kama pembejeo,masoko,mitaji n.k huwarudisha nyumba sana wakulima na hatimaye Taifa.
? Ajira kwa Vijana ambao wanamaliza shule na vyuo. Kuiunua viwanda,kufufua kilimo,kukomesha rushwa,uwajibikaji na elimu za ufundi kwa pamoja zitatoa ajira kwa vijana.
? Kutokomeza umaskini wa kipato kwa wananchi wa hali ya chini kwa kufufua kilimo,kutoa ajira,kukomesha rushwa na kutoa huduma safi za afya.
? Kupunguza pengo kati ya wenye nacho na wasionacho (Tajiri na Maskini) kwa kupunguza mianya ya unyonywaji kwa wasionacho.
Ni matumaini yangu kila Mtendaji atatoa ushirikiano mkubwa katika kufanikisha haya na JPM atafuatilia kwa ukaribu watendaji wasio na tija wenye nia ya kuendekeza ulaji na upigaji wa madili badala ya kuleta maendeleo.