Picha: Mwigulu Nchemba afunga mafunzo ya UVCCM - Ruvuma

Picha: Mwigulu Nchemba afunga mafunzo ya UVCCM - Ruvuma

Unamuuliza nani ili iweje.

CCM haina siasa za kilaghai na kikubwa kabisa, CCM haina vibaraka wanaotumikia makafiri kupata mtaji wa matumbo yao.

CCM haichakachui katiba yake bali inafanya kazi zake kupitia vikao halali.

CCM haijengwi na viongozi bali wanachama ndiyo wajenzi wake.

Utamhadaa nani dunia ya sasa? ccm inajengwa na mafisadi wauza ya sembe.
 
Ni kweli wanaoumia ni walalahoi kwenye maandamano kwa sababu huwezi kuwa na nyumba South Africa, United Kingdom, USA, Dubai and Nairobi usiweze kuweka pesa za kificho kwenye mabenki ya Seychelles, Mauritius, Malta, Gibraltar, Channel Islands Luxembourg n.k

Huyu ndiye Mwenyekiti tajiri wa Chama Cha Siasa Tanzania ambaye hatosheki mpaka anachakachua katiba ya chama na kuairisha uchaguzi wa ndani ya chama ili aendeleze ulafi wa madaraka na pesa.

Hivi huyu Mwenyekiti tajiri alirudisha gari ya KUB kama alivyodai?.

Niambie chama gani Duniani zaidi ya CCM Tanzani na CCCP China ndio vinavyofanya uchaguzi wa VIONGOZI wao KICHAMA?

Hii ni propaganda kwanini hamuwaulizi CUF au NCCR? Mnajua mtapandikiza vinara ndani ya chama kinachowapa taabu Usiku na Mchana hamuwezi hata kulala

Kwahiyo ni hela za RUZUKU tu zinazomtajirisha? Ni nini kinachokuuma wewe? Pesa za RADA ziko wapi? Tuelezee basi?
 

Kama ni ZIARA ya KICHAMA ni lazima awatembelee MKUU wa MKOA na MKUU wa WILAYA? wakati ziara yake ilikuwa NAMTUMBO??

Kwahiyo ina Maana vyama vya Upinzani pia wakifanya ziara zao huwa wanapewa nafasi ya kuonana na Mkuu wa Mkoa wanoutembelea na kupewa CHAI ya MOTO na MAZIWA? na TV Pembeni? halafu Kukutana na Mkuu wa WILAYA?

Ni nani anayelipia hizo GHARAMA? ni PESA za RUZUKU????

Huwa ni lazima awatembelee hao kwa kuwa Mkuu wa Mkoa au Mkuu wa Wilaya sifa mama ya wao kuteuliwa ni kuwa kada wa chama ambaye mchango wake katika chama unajulikana. Kinyume na hivyo hawezi kuteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa au Mkuu wa Wilaya. Kwa hiyo amewatembelea makada wenzake wa chama.

Hebu angalieni kofia aliyovaa Mwigulu Mchemba. Mbona inanipa kumbukumbu ya Adolf Hitler wa Ujerumani? Nakosea kweli kuwa naiona taswira ya dikteta yule aliyewaua Wayahudi kwa mamilioni?
 
CCM ilithubutu, ikaweza na kwa sasa inasonga mbele huku ikilipa mkopo wa kura iliopewa na wananchi wapenda amani, umoja na maendeleo kupitia sanduku la kura kwa mamilioni nchini 2010.

CCM haina muda wa kurumbana na wapinzaji wanaoongoza nchi ya kufikirika kwa sababu ulaghai wao ulikataliwa na wananchi kwa mamilioni kupitia sanduku la kura kuanzia mwaka 1995.

Kwa sasa wamebaki kuzodoana na kurumbana kutokana na ulaghai wao siyo kwa wananchi peke yao bali hata wao kwa wao wamelaghaiana kwa kubadilisha vipengele kinyemela bila kuambizana kupitia vikao vyao vya kinafiki vya kinafikia na kizandiki.

Yako wapi makambi ya Red Brigades ambao yalitangazwa na viongozi wa kilaghai.

CCM inaongoza na vyama vya upinzani vitaendelea kufuata kwa nyuma,

Like it or not. Huu ndiyo ukweli halisia.

Kama hutaki, kick the wall and die.

pole sana kumbe bado hujajitambua daa.....
 
Mwigulu ni jembe na hizo ndio siasa sio kuandamana. Kwa taarifa tu kuna zaidi ya wilaya 92 zimeanza fanya mambo Kama hayo ya Namtumbo!

Hii inasaidia sana kukijenga chama kuliko kuropoka Kama wafanyavyo Chamdomo!

Sasa ni vitendo hakuna maneno, wenzao CUF wanahangaika na uchaguzi sasa hadi 2014 CCM wanahangaika na maandalizi ya uchaguzi wa serikali za mitaa! CDM wao bado wanaogopa kufanya uchaguzi wanajua kitakachotokea!

Chukua hatua chukia Chamdomo
 
Back
Top Bottom