Watu wa JF, ni wa ajabu sana. Wanatagiana kuja kuona maumbile ya mgonjwa. Si kwa lengo la kujifunza, bali kukejeli.
Anyway, turudi kwenye uzi.
Kwanza, pole sana Mkuu. Ni tatizo la kawaida, hivyo comments za wanaJamii zisikutishe sana.
Pili, ni ngumu kidogo kutabiri ni ugonjwa gani. Kwa sababu magonjwa ya zinaa yana dalili kadhaa zinashoshabihiana. Lakini pia, sijapata maelezo yako. Je, tatizo lilianza lini? Je, kwenye muoto huo kunauma? Dalili zinazoambatana na hali hiyo ni zipi? Ukikojoa unaumia?
Tatu, kwa makisio ya kawaida kwa kutumia macho, inaonyesha ni genital warts. Siyo herpes. Kwa asiyefahamu, anaweza dhani ni moja. Ila herpes zinakuwa vijipele wakati warts inaoteana kama kinyama. Ni ugonjwa unaoambukizwa kwa kushiriki ngono isiyo salama.
Hakuna dawa ya kutibu magonjwa tajwa, kinga yako ya mwili inaweza kusambaratisha na kupotea baada ya muda.
Hata hivyo, kuna dawa zinazoweza kupunguza maumivu (endapo yapo). Si busara kuzitaja bila ya kuthibitisha ugonjwa husika.
Nne, yakupasa ufike katika kituo cha afya karibu yako kwa ajili ya uchunguzi zaidi. Mtaalamu wa afya atakupa dawa kulingana na matokeo ya vipimo.
Tano, nakutakia uponyaji mwema. Zingatia ngono salama na matumizi ya dawa na ushauri wa daktari.