Moja ya desturi nisiyoikubali kabisa kwa kizazi kijacho Kilimanjaro ama Moshi hai na rombo itakuwa eneo la makaburi kubwa kabisa katika uso wa tz NI nadra sana ukute nyumba haina kaburi au shamba Halina kaburi na wanayaweka karibu kabisa na makazi yao..huweki kuta MTU anazikwa katikati ya shamba...kabla ya hapo Kuna jamii (ukoo)ulikuwa unazika ndani ya nyumba zile misonge ya makuti...baada ya miaka miwili wanafukua kwa nje na kwenda kuitupa mifupa sehemu Fulani iliyotengwa kwa ajili hio(story behind)NI kuwa katika kipindi hicho Cha miaka miwili endapo watafukua mwili na kukuta haujamalizika kuoza wanajua aliuwawa kwa nguvu za kishirikina....miaka ya 50 ukristo ulipoingia ndio ukaanza taratibu za kuzika kwenye maeneo ya kanisa nayo yakajaa watu wakaanza kuzikia makwao...kwao baada ya muda ukiendelea huu utaratibu wa kuzika kila mtu mgombani kutakuwa grave yard Wala hakutakuwa na kahawa Wala mgomba...