Mgirik
JF-Expert Member
- Apr 27, 2013
- 13,258
- 13,367
Natumai wote mu buheri wa afya.
Napenda kurejea kwenye maada husika.
Katika social network nyingi hivi karibuni kumetokea na hili jambo la kuwarusha askari wetu wakiwa kwenye matukio mbalimbali ambayo hayaendani na maadili ya kazi au maadili ya jamii.
Binafsi kama raia sijapendezewa na mambo wanayoyafanya askari wetu, ni mambo ya kulidhalilisha jeshi letu la polisi na kuidhalilisha sare ya jeshi ambayo ni moja ya nembo ya taifa hili.
Lakin pamoja na udhaifu huo uliopo kwa hawa wenzetu, hatukupaswa kufanya kama hivi tulivyofanya. Kitendo cha kurusha picha hizi kwenye social network ni udhalilishaji mkubwa sana dhidi ya jeshi letu.
Nikweli yawezekana ikawa njia moja wapo ya kuwaamsha kuwa wawe makin katika utendaji wao na hasa wawapo maeneo ya kazi lakini kuna picha zingine zmevuka mpaka.
Tutambue kuwa askari naye ni binadamu kama tulivyo mimi na wewe na yeye ana mapungufu kama binadamu kwahyo ni bora tukatumia busara zaidi kuliko hivi tunavyofanya.
Inafikia hatua unampiga picha akiwa amesinzia bila kuangalia kuwa huyo askari na yeye anachoka kama ambavyo tunachoka mimi na wewe.
Tukumbuke kuwa kabla mimi na wewe hatujaamka kwenda kazini hawa jamaa wanakuwa wapo barabarani mpaka muda tunapokuwa kazini wao bado wanakuwa barabaran kwa ajili ya usalama wetu sasa kwa nini tufikie hatua ya kuwadhalilisha kias hcho?
Ni bora kama umemuona amekaa mahali kasinzia nenda kamwamshe hata yeye atakuona unamaana zaidi kuliko kumrusha kwenye mitandao.
Hebu fikiria angekuwa babayako,mama yako au dadayako au kaka yako ndio anarushwa vile na baadae anafukuzwa kaz kwa kosa dogo ambalo hata ww unauwezo wa kumsaidia.
Tukumbuke kuwa maisha yetu watanzania huwa walio wengi tunategemeana, unapomfukuzisha kazi mwenzako tayari unakuwa umewarudisha nyuma watu wengi sana wanao mtegemea.
Kama wabunge wenyewe pamoja na kuwa na viyoyozi ukumbin lakn bado wanasinzia sasa sembuse askari anayepigwa na jua masaa12?
Na tusisahau mfumo wa nchi yetu yule mwenye kosa dogo ndiyo anateketezwa lakn mwenye kosa kubwa ndiye analindwa.
.......(wanachuja mbu na kumeza ngamia)..........
Kama tunafanya hvyo eti kwa lengo la kuondoa uovu ulio ndani ya jeshi la polis tutakuwa tunakosea kabisa, . Watu wa kudeal nao ni viongoz wa juu , uongozi wa serikali ukiwa imara na thabit hata watendaji wake na wasimamia sheria watakuwa imara,.
Lakn haya tunayoyafanya huku ni kuwaonea tu hawa wenzetu.
Kumbuka hata polis wao sio wote ni wadhalim bali wanashindwa kufanya maamuzi sahihi ya haki kwa sababu ya kusaka tonge, wanaogopa wakienda tofauti na maelekezo watapoteza kazi zao kitu ambacho kitakuwa janga kwa familia zao na wategemezi wao..
....... Napenda niishie hapa.........
Napenda kurejea kwenye maada husika.
Katika social network nyingi hivi karibuni kumetokea na hili jambo la kuwarusha askari wetu wakiwa kwenye matukio mbalimbali ambayo hayaendani na maadili ya kazi au maadili ya jamii.
Binafsi kama raia sijapendezewa na mambo wanayoyafanya askari wetu, ni mambo ya kulidhalilisha jeshi letu la polisi na kuidhalilisha sare ya jeshi ambayo ni moja ya nembo ya taifa hili.
Lakin pamoja na udhaifu huo uliopo kwa hawa wenzetu, hatukupaswa kufanya kama hivi tulivyofanya. Kitendo cha kurusha picha hizi kwenye social network ni udhalilishaji mkubwa sana dhidi ya jeshi letu.
Nikweli yawezekana ikawa njia moja wapo ya kuwaamsha kuwa wawe makin katika utendaji wao na hasa wawapo maeneo ya kazi lakini kuna picha zingine zmevuka mpaka.
Tutambue kuwa askari naye ni binadamu kama tulivyo mimi na wewe na yeye ana mapungufu kama binadamu kwahyo ni bora tukatumia busara zaidi kuliko hivi tunavyofanya.
Inafikia hatua unampiga picha akiwa amesinzia bila kuangalia kuwa huyo askari na yeye anachoka kama ambavyo tunachoka mimi na wewe.
Tukumbuke kuwa kabla mimi na wewe hatujaamka kwenda kazini hawa jamaa wanakuwa wapo barabarani mpaka muda tunapokuwa kazini wao bado wanakuwa barabaran kwa ajili ya usalama wetu sasa kwa nini tufikie hatua ya kuwadhalilisha kias hcho?
Ni bora kama umemuona amekaa mahali kasinzia nenda kamwamshe hata yeye atakuona unamaana zaidi kuliko kumrusha kwenye mitandao.
Hebu fikiria angekuwa babayako,mama yako au dadayako au kaka yako ndio anarushwa vile na baadae anafukuzwa kaz kwa kosa dogo ambalo hata ww unauwezo wa kumsaidia.
Tukumbuke kuwa maisha yetu watanzania huwa walio wengi tunategemeana, unapomfukuzisha kazi mwenzako tayari unakuwa umewarudisha nyuma watu wengi sana wanao mtegemea.
Kama wabunge wenyewe pamoja na kuwa na viyoyozi ukumbin lakn bado wanasinzia sasa sembuse askari anayepigwa na jua masaa12?
Na tusisahau mfumo wa nchi yetu yule mwenye kosa dogo ndiyo anateketezwa lakn mwenye kosa kubwa ndiye analindwa.
.......(wanachuja mbu na kumeza ngamia)..........
Kama tunafanya hvyo eti kwa lengo la kuondoa uovu ulio ndani ya jeshi la polis tutakuwa tunakosea kabisa, . Watu wa kudeal nao ni viongoz wa juu , uongozi wa serikali ukiwa imara na thabit hata watendaji wake na wasimamia sheria watakuwa imara,.
Lakn haya tunayoyafanya huku ni kuwaonea tu hawa wenzetu.
Kumbuka hata polis wao sio wote ni wadhalim bali wanashindwa kufanya maamuzi sahihi ya haki kwa sababu ya kusaka tonge, wanaogopa wakienda tofauti na maelekezo watapoteza kazi zao kitu ambacho kitakuwa janga kwa familia zao na wategemezi wao..
....... Napenda niishie hapa.........