+255
JF-Expert Member
- Jan 1, 2012
- 1,939
- 762
Hebu ona hizi picha hapa chini
Hiyo picha Komba kapiga akiwa bungeni?
Hebu ona hizi picha hapa chini
Nimefanikiwa kutembelea tovuti ya utoaji mikopo VICOBA ambayo ni www.vicobatanzania.wapka.mobi nimejiunga na kupatiwa mkopo nimechukua mil.10 mil.5 nahitaji kuwekeza ktk biashara ya duka la jumla la vinywaji mil.5 nyingine nataka kununua kiwanja.
Wana JF kwa mwenye wazo lolote au ushaur kuhusu biashara ya duka la jumla anisaidie nawaomba.
Nakubaliana kabisa kwamba maadili yameporomoka sana. Ikumbukwe kuwa jeshi la Polisi pamoja na mabaya yote , ni mali ya wananchi.
Tabia inayoendelea siku hizi ya kupa-publish maswala ya kipolisi kwenye mitandao ni kosa kubwa kwani ikumbukwe kwamba polisi mmoja ama wawili wanapofanya kosa hawaliwakilishi jeshi la Polisi. Ni matendo ya watu binafsi kama binadamu wengine.
Lakini kwa upande mwingine jeshi la polisi nao wajiangalie na kujichuja wenyewe. Hivi, kwa mfano karatasi ya simu ambayo hivi karibuni imezagaa kwenye mitandao ikiwa ni amri ya Trafic hq kubadilisha kazi kwa ma-Wp wawili waliofanya kazi kizembe ilitokaje kwenye mafaili ya Polisi hadi mitandaoni? Je,huko siyo kufanya kitendo kibaya kinyume na sheria za polisi?
Hii maana yake kuna watu waliopewa dhamana za utunzaji wa nyaraka hawajatimiza wajibu wao.
Polisi na nyie safisheni nyumba yenu kwanza. Mu hodari wa kupeleleza makosa ya wengine, munashindwaje kupeleleza kwenu?
Jamii ielewe kwamba pamoja na makosa wanayoyafanya polisi, pamoja na kutowapenda kote , pamoja na kuwaita majina yote ya kifedhuli kama vile policcm na mengineyo, bado tunalihitaji jeshi la polisi kwa kiasi kikubwa.
Fikiria jeshi la polisi lisimame kufanya kazi kwa saa moja tu, madhara yatakuwaje!
Ni kweli polisi mmoja akifanya kosa haimaanishi ni wote na ndio maana hata waliofukuzwa kazi ni hao tu waliofanya kosa sio polisi wote,lakini jambo kuangalia ni wapi walipojikwaa sio walipoangukia na hii ndio nafasi ya kujirudi na wakae kwenye mstari vinginevyo katika hiki kipindi cha utandawazi wataumbuliwa mpaka wakose pa kupita. Hivi kama ushahidi wa picha kwenye mitandao umetosha kuwafukuzisha kazi hao wa chini vipi kuhusu zile picha za mauaji ya Mwangosi kule Nyololo na yule kamanda alipelekwa wapi?
Mimi na declare siwapendi polisi, ktk maisha yangu sijaona msaada wao zaidi ya kero kwangu na jamii. Sitegemei kuwa na rafiki polisi
Si bure utakuwa umetokea kwenye familia ya vibaka..huwezi kuwapenda polisi wakati una damu ya kihalifu.
Hao watu walikupeje mkopo? Yani huwezi rudisha kabisa! Dah elimu ya hela inahitajika sana TZ. Sasa hio 5 ya kiwanja unampango wa kurudisha na 5 uliyo invest kwenye duka la jumla ambalo hujawahi hata kuanza!
Halafu mbona unaharibu thread?
Natumai wote mu buheri wa afya.
Napenda kurejea kwenye maada husika.
Katika social network nyingi hivi karibuni kumetokea na hili jambo la kuwarusha askari wetu wakiwa kwenye matukio mbalimbali ambayo hayaendani na maadili ya kazi au maadili ya jamii.
Binafsi kama raia sijapendezewa na mambo wanayoyafanya askari wetu, ni mambo ya kulidhalilisha jeshi letu la polisi na kuidhalilisha sare ya jeshi ambayo ni moja ya nembo ya taifa hili.
Lakin pamoja na udhaifu huo uliopo kwa hawa wenzetu, hatukupaswa kufanya kama hivi tulivyofanya. Kitendo cha kurusha picha hizi kwenye social network ni udhalilishaji mkubwa sana dhidi ya jeshi letu.
Nikweli yawezekana ikawa njia moja wapo ya kuwaamsha kuwa wawe makin katika utendaji wao na hasa wawapo maeneo ya kazi lakini kuna picha zingine zmevuka mpaka.
Tutambue kuwa askari naye ni binadamu kama tulivyo mimi na wewe na yeye ana mapungufu kama binadamu kwahyo ni bora tukatumia busara zaidi kuliko hivi tunavyofanya.
Inafikia hatua unampiga picha akiwa amesinzia bila kuangalia kuwa huyo askari na yeye anachoka kama ambavyo tunachoka mimi na wewe.
Tukumbuke kuwa kabla mimi na wewe hatujaamka kwenda kazini hawa jamaa wanakuwa wapo barabarani mpaka muda tunapokuwa kazini wao bado wanakuwa barabaran kwa ajili ya usalama wetu sasa kwa nini tufikie hatua ya kuwadhalilisha kias hcho?
Ni bora kama umemuona amekaa mahali kasinzia nenda kamwamshe hata yeye atakuona unamaana zaidi kuliko kumrusha kwenye mitandao.
Hebu fikiria angekuwa babayako,mama yako au dadayako au kaka yako ndio anarushwa vile na baadae anafukuzwa kaz kwa kosa dogo ambalo hata ww unauwezo wa kumsaidia.
Tukumbuke kuwa maisha yetu watanzania huwa walio wengi tunategemeana, unapomfukuzisha kazi mwenzako tayari unakuwa umewarudisha nyuma watu wengi sana wanao mtegemea.
Kama wabunge wenyewe pamoja na kuwa na viyoyozi ukumbin lakn bado wanasinzia sasa sembuse askari anayepigwa na jua masaa12?
Na tusisahau mfumo wa nchi yetu yule mwenye kosa dogo ndiyo anateketezwa lakn mwenye kosa kubwa ndiye analindwa.
.......(wanachuja mbu na kumeza ngamia)..........
Kama tunafanya hvyo eti kwa lengo la kuondoa uovu ulio ndani ya jeshi la polis tutakuwa tunakosea kabisa, . Watu wa kudeal nao ni viongoz wa juu , uongozi wa serikali ukiwa imara na thabit hata watendaji wake na wasimamia sheria watakuwa imara,.
Lakn haya tunayoyafanya huku ni kuwaonea tu hawa wenzetu.
Kumbuka hata polis wao sio wote ni wadhalim bali wanashindwa kufanya maamuzi sahihi ya haki kwa sababu ya kusaka tonge, wanaogopa wakienda tofauti na maelekezo watapoteza kazi zao kitu ambacho kitakuwa janga kwa familia zao na wategemezi wao..
....... Napenda niishie hapa.........
Duuh! Thank you, nadhani wewe unanufaika na uozo wa mapolisi, Niwe mhalifu au sio siwezi badilisha msimamo wangu. Na popote wakiniletea za kuleta nawanyoosha. Nawajua hao watu kuliko unavyonidhania
huku mitandaoni nnajua sana kuongea ila mtaani kimya na mnanyooshwa vilivyo na watu kama wewe ndo wale wamenyong'onyea kama kuku aliyenyeshewa