Philip Mangula ateuliwa kugombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa CCM

Hii cinema nyingine mpya ndani ya CCM. Mzee Mangula (wakati huo akiwa Katibu Mkuu wa CCM) aliyemkataa JK waziwazi asipitishwe kugombea urais mwaka 2005 maana hakuwa safi na report za sekretariati za mikoa nyingi zilikuwa chafu juu yake. Baada ya JK kushika hatamu za chama akampiga chini ukatibu mkuu. Mzee Mangula akagombea uenyekiti wa chama Mkoa wa Iringa, mara mbili mfululizo JK anampiga chini. Leo JK huyo huyo anageuka na kumkumbuka hasimu wake mkubwa. Kuna nini nyuma ya pazia? Unahitaji akili ya ziada (sio ya binadamu wa kawaida) kuendelea kuwa mwana CCM na kushuhudia haya maajabu huku ukipiga makofi na kuimba nyimbo ambazo moyoni mwako huziamini. Sina uhakika hata kama ukichanganya na za mbayuwayu unaweza kuwaelewa hawa jamaa.
 
Kamati kuu ya CCM iliyo kaa hapa dodoma imempendekeza Philip Mangula apigiwe kura na Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM,Mangula amewahi kua Katibu Mkuu wa CCM na ameshika nafasi mbali mbali ndani ya Chama. Kwa sasa Philip Mangula ni Mashauri wa mambo ya siasa kwa Chama tawala cha Afrika ya Kusini ANC,nafasi ambayo ameanza kuitumikia tangu mwaka 2008,ana sifika kuwa ni mtu mwenye mbinu nyingi za kisiasa hasa kwenye masuala ya uchaguzi na mikakati ya kueneza siasa.
Vijana mpo? stand up and say something munahitaji maelezo marefu, huyu ndiye aliyesema kikwete hafai wakati amechukua fomu kugombea uraisi....leo tena anakuwa makamu mwenyekiti? there must be something wrong somewhere.
 
kawa abused kama makinda..Sijui this time hawajapata mwanamke wa ku abuse tena?
 
Mchambuzi;5006705]Nguruvi3,
Umetoa hoja za msingi sana kwenye bandiko namba 144, Kwanza kuhusu Dawa ya Matatizo ya Sasa ya CCM baina ya Vijana na Wazee , na Pili kuhusu Majukumu ya Makamu Mwenyekiti; Tukianza na suala la Ujana vis a vis Uzee kama ndio Dawa ya matatizo ya CCM ya leo, kwa mtazamo wako, mabadiliko haya ya ujana/uzee yataikumba na sekretarieti kwa kiasi gani? Na je ni muhimu wazee warudi katika nafasi hizi?
Mchambuzi, mabadiliko ya ujana vs uzee hayatokei naturally, it's all about circumstances around which compell the changes.
Siku zote nimekuwa nasema watu tusiangalie umri kama kigezo bali busara hekima na uadilifu.

Tatizo kubwa si ujana au uzee, ni mfumo unaopelekea upatikanaji wa viongozi ndani ya CCM.
JK alifanya kosa kubwa sana, kwanza kulipa visasi vya kisiasa na pili kuendeshwa na kundi lililojivika kofia ya ujana huku tukielewa kuwa hiyo haikuwa agenda yao. Nadhani umeona safu ya uongozi wa vijana uliopo. Utakubaliana nami kuwa hakukuwa na vetting ya kutosha na ndio maana vijana wenye uwezo wa kukiendeleza chama wameachwa nje, simply because majina yao haya link.

JK alipoingia alibadili chama 360 degree akiwatupa wazee nje. Kwa vile vijana hao hawakupatikana kwa njia sahihi sasa analazimika kuwaangukia wazee. Mtu kama Mangula akikubali nafasi hiyo atakuwa amejivika mzigo mzito sana.
Hatakuwa na nguvu za kujenga chama ambacho msingi tayari umeharibika. Kila atakachokifanya atakumbana na makundi ya ''vijana'' huko NEC na atakwama tu. Ndivyo kijana Nape Nnauye Jr alivyokwama.

Kuhusu sekretariati hata kama wazee watarudi bado equation inarudi pale pale, watafanya nini katika NEC iliyopo ku-transform chama? Lakini pia vijana wameshaonja tamu ya sekretariati hivyo sidhani kama wazee watarudi. Kutakuwa na sintofahamu kubwa sana.

Tatizo lipo katika uongozi wa kitaifa, kwamba mwenyekiti ameshindwa kutumia nguvu alizopewa na chama kurudisha nidhamu, na sasa ni too late.
Kwa mtazamo wake, Je hili pia limechangia Msekwa kushindwa kuimudu nafasi hiyo au hilo lilichangiwa zaidi na uwezo wake kuwa mdogo wa kuongoza katika siasa za kisasa? Kwa Mujibu wa katiba ya CCM, ibara ya 120, sehemu ya (4):Makamu wa Mwenyekiti watakuwa ndiyo wasaidizi wakuu wa Mwenyekiti wa CCM na watafanya kazi zote za CCM watakazopewa na Mwenyekiti wa CCM; Pengine hii inaweza kutoa mwanga kidogo kuhusu wapi ndio kuna tatizo;
Hapa tatizo lipo kwa Mwenyekiti. Ukitazama katiba kwa undani, makamu mwenyekiti ni msaidizi wa Mwenyekiti na hakuna maamuzi yoyote yatakayofanywa na makamu bila ridhaa ya Mwenyekiti kama yupo katika uwezo wa kifikra na kiafya.

Mwenyekiti wa CCM anaogopa kukabiliana na majukumu na kazi zake. Anachagua kazi za kufanya na za kumtupia Makamu. Tunakumbuka uteuzi wa Msekwa ulilenga kuleta nidhamu. Kilichotokea ni kuwa kupanga safu ya uongozi hilo alilifanya Mwenyekiti. Kukabiliana na maamuzi magumu ya kichama alimtupia Makamu. Wakati akimtupia makamu, Mwenyekiti alikimbia upande wa pili. Inaonekana kana kwamba Mwenyekiti anamshakizia ''ubaya'' makamu.Hilo ndilo Msekwa anataka kulikwepa hasa ukizingatia historia yake nzuri ndani ya chama. Nani atabeba zigo, pengine Mangula!

Kimsingi, nakubaliana na hoja yako kwamba busara hapa ni Mangula kukataa kutumikia nafasi hiyo, lakini mimi naongezea kwamba - unless kunakuwa na mabadiliko makubwa ya Kikatiba, na pia yeye ashirikishwe kwa nguvu zote kutengeneza safu mpya ya sekretarieti mpya na Kamati Kuu, na Katiba ifanye mabadiliko fulani fulani kuondoa baadhi ya majukumu ya NEC na yahamie kwenye Kamati Kuu ili kuanzia sasa tuwe tunajua wanaoboronga kimaamuzi ni kina nani; Ni kama vile Supreme Court nchini marekani, wapo majaji tisa nadhani kama sio saba, na kila mmoja maamuzi yake yanaenda on record; Kamati Kuu ichukue majukumu muhimu ya NEC na ifuate mfumo huu; Najua kamati kuu kwa sasa ndio yenye maamuzi lakini NEC bado ni supreme to CC in practice;
Katika siku za nyuma, maamuzi ya kamati kuu yaliheshimiwa sana.Uwepo wa kamati kuu ni njia ya kuwa na kikundi kidogo effective na responsible.

Kwa vile hilo limeonekana ni kikwazo, zimetumika njia nyingi kuipa NEC nguvu ya ziada. Huko ndiko tatizo lililopo hasa.
Nakubaliana nawe kabisa kuwa kama mfumo uliopo hautafanyiwa reform, ikiwa ni pamoja na Mwenyekiti kubanwa katika uwajibikaji, hakuna chochote kipya na hapo ndipo chama kinapokuwa safarini kuungana na KANU au UNIP
 
Fisadi fisadi tu, hata huyu yupo kwenye orodha ya Halima Mdee ya wanyang'anyi ya ardhi ya watanzania pale wame dakawa Mvomero. Karibu uone M4C
 
Kikwete wanamwondoa? Mangula na Kikwete wanawezaje kufanya kazi pamoja? Uwezo na Mangula na Kikwete ni sawa na kulinganisha mlima kilimanjaro na Kichuguu. Sasa utawawekaje pamoja hawa? Lakini pia ikumbukwe kwamba Kikwete alimtosa vibaya sana Mangula, baada ya Mangula kueleza wazi kwamba Kikwete hana uwezo wa kuongoza nchi. Sasa leo watakaeje tena kujadili masuala ya mstakabali wa taifa ilihali ni mahasimu?
kwa nini kikwete ni kama kichuguu na mangula ni mlima?kikwete alimtosa mangula wapi na lini?lini mangula alisema kikwete hafai kuwa kiongozi?ni nani aliemchagua kikwete kuwa mwenyekiti wa chama na sasa ni nani anaemchagua magula kuwa naibu mwenyekiti?
 
ni nchi gani duniani yenye rushwa kwa asilimia 0.00?

Haipo, lakini hatuwezi kukubali standards za mataifa mengine hata kwenye mambo ya kishenzi kama rushwa. Rushwa ni ushenzi na ni upumbavu, rushwa ni adui wa haki na inaondoa thamani ya utu. Lazima tujenge institutions za kuongoza maisha yetu ambazo haziendeswi kwa misingi ya rushwa. au unataka kujenga hoja gani?
 
Kiamsingi bwana mkubwa mwaka 2005 alitaka kuweka watu wake akiamini kuwa he is the best to the post na kuumaliza mtangulizi wake ili aonekane yeye ndio mzuri. Leo hii anagundua kuwa aliowaamini ndio wamemuangusha wanagombea madaraka kama machangudoa wanavyogombea mwanaume mwenye hela. It is a good move but i think too late.
 
Kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi hii, makundi ya wazi kwenye mbio za uongozi yalianza kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 1995. Makundi haya, yalidhihiri ndani ya CCM. Hata hivyo, tofauti na chaguzi za kabla ya (1995) hapo, mazingira ya kisiasa nchini yalikuwa ni moja ya chanzo cha uasisi wa makundi ya wazi kwenye uchaguzi wa mwaka 1995.Kwenye kutafutwa mwakilishi wa CCM, kulikuwa na makundi kadhaa yaliyokuwa yanawaunga mkono watu wao...makundi hayo ni pamoja na yale yaliyokuwa yanamuunga mkono Lowassa, Kikwete, pamoja na Mwandosya.
BAADA YA UCHAGUZI MKUU WA 1995.
Tofauti na baada ya uchaguzi wa mwaka 2005(ambapo makundi bado yalikuwapo), mara baada ya uchaguzi mkuu( wa 1995) ambao ulimwingiza madarakani Mkapa, makundi yote niliyoyataja hapo juu yalikufa. Kundi kubwa kuliko yote lilikuwa la Kikwete. Kundi la Kikwete lilikua zaidi baada ya kuongezewa nguvu na kundi lililokua linamuunga mkono Lowasa. Kwavile Lowasa alipigwa kumbo(na Nyerere) mapema, ikatokea kwamba wafuasi wake wengi kama sio wote waliingia kwenye kambi ya Kikwete. Lowasa na Kikwete walikuwa na maswahiba!
Hata hivyo, kufa kwa makundi hayo hakukutokea kwa bahati mbaya ingawaje vile vile Phillip Mangula hakuwa mchango mkubwa wa kuondosha makundi hayo.

SABABU AMBAZO ZILIUA MAKUNDI!
1. DHAMIRA YA DHATI YA JAKAYA KIKWETE

Waswahili wanasema kwamba, Mnyonge mnyongeni, haki yake mpeni! Sababu kubwa ambayo ilifanya makundi ya mwaka 1995 ni dhamira ya dhati ya Kikwete pale alipotangaza(baada ya kutochaguliwa kuwakilisha chama 1995) kuvunja kwa mtandao wake. Baada ya mizengwe ya Mwalimu kumpitisha Mkapa, Kikwete alitangaza wazi kwamba anavunja rasmi mtandao wake na wote wajikite kwenye uchaguzi mkuu ambao hasimu wao mkubwa alikuwa Mrema wa NCCR. Na hata baada ya Mkapa kuingia Ikulu, mtandao wa KIkwete ulimwacha Mkapa aongoze nchi kwa amani tofauti na mitandao ya sasa. Ingawaje ni kweli pia kwamba, kwa namna fulani mtandao wa Kikwete ulikuwa unajipanga kwa ajili ya uchaguzi wa 2005, lakini kujipanga huko hakukua kwa wazi wazi kama ilivyo sasa. Na sana sana, Kikwete alikuwa anajipanga kwa kutumia magazeti zaidi kuliko kuleta makundi kwenye chama. Magazeti yote, hususani ya Habari Corporation yalikuwa yanamchora Kikwete kama mtu bora kabisa pengine kuliko uhaliisa wake! Magazeti yalimpamba kwa nyimbo na mapambio kwa mambo yote mazuri kiasi kwamba kila mmoja alifahamu hakuna ambae angeweza kushindana na Kikwete 2005. Hapa tusidanganyane, hadi 2005 inaingia, hakukua na mtu ambae alikuwa na ubavu wa kuchuana na Kikwete kwani huyu bwana alifanikiwa sana kuyatumia magazeti na ndio maana haikushangaza pale alipoibuka na usindi wa 80%! Huku Uswahilini kulikuwa na simulizi kibao kuhusu Kikwete huku zote zikionesha ni jinsi gani alikuwa extra-ordunary person! Simulizi ambayo hadi leo hii sijaisahau ni ile iliyohusu ushiriki wake wa Vita vya Kagera!! Huyu jamaa (JK), alikuwa hapigiki risasi!!! LOL!

2. USWAHIBA WA LOWASA NA KIKWETE.

Sababu nyingine ambayo ilichangia kufa kwa makundi ya 1995 ni uswahiba wa Lowasa na Kikwete. Pamoja na kwamba kuelekea 2005 Kikwete alikuwa ndie mgombea mwenye nguvu zaidi lakini bado Lowasa nae alikuwa na nguvu ingawaje alishachafuliwa na Nyerere! Na kwavile KIkwete alikuwa na nguvu zaidi huku Lowasa akiachwa majeruhi wa kashfa, basi bila shaka hapo KIkwete na LOwasa wakaamua kuunda "alliance." Alliance hii ni kwamba, ifikapo 2005, Lowasa asigombee bali amuunge mkono swahiba wake KIkwete na hivyo kuondosha kabisa misuguano kati ya wanachama hawa wawili ambao wote walikuwa na nguvu!

3. UUNGWANA WA MARK MWANDOSYA NA SALIMU AHMED SALIMU.
Kwa namna fulani, katika vipindi tofauti tofauti; baadhi ya magazeti, hususani ya Habari Corporation yalikuwa yanafanya kazi ya kumjenga KIkwete na wakati huo huo kuwachafua Mark Mwandosya na Salimu Ahmed Salimu. Hawa walikuwa ndio tishio pekee(hata kama hawakuwa na mabavu makubwa kama JK) kwa Kikwete kwenye uchaguzi wa 2005. Kama si chuki za kihistoria ( za ASP, ZPP na HIZBU), huenda tishio kubwa zaidi kwa Kikwete angekuwa ni Salim Ahmed Salim lakini kwa bahati mbaya Salim aliangushwa zaidi na Wazanzibari wenzake(waliokuwa against HIZBU) kuliko kuangushwa na uchafuzi uliokuwa unafanywa na magazeti.

Hivyo basi, ingawaje baadhi ya magazeti yalitumika kumchafua Salim na Mwandosya, lakini waheshimiwa hawa walijizuia kuingia kwenye mnyukano huo na hivyo kuacha magazeti yakimpamba zaidi Kikwete kuliko uwepo wa habari za mnyukano ndani ya magazeti. Hii ni tofauti na sasa!

4. UKALI WA MKAPA!
Kwangu mimi, Mkapa ni one of the most corrupt leaders ever happened in Tanzanian History! Hata hivyo, kwangu mimi huyu atabaki ndio kiongozi pekee(ukimwacha Nyerere) ambae alikuwa na msimamo na ambae hakupenda upuuzi (hususani, upuuzi dhidi yake)!Siamini kabisa kwamba Mkapa angeweza kuvumilia upuuzi wa minyukano unaendelea hivi sasa CCM! Hii ni tofauti kabisa na Mwenyekiti wa sasa.

Hivyo basi, ukiangalia ukweli huo, ndipo utaona kwamba mchango wa Katibu Mkuu(Phillip Mangula) ulikuwa mdogo sana katika kufanya kutokuwapo kwa makundi baada ya uchaguzi wa 1995.

KWANINI MAKUNDI YALIENDELEA HATA BAADA YA UCHAGUZI WA 2005.
Tofauti na kufa kwa makundi baada ya uchaguzi wa 1995, makundi ya 2005 bado yanaendelea kukitafuna chama! Ukisha-negate(ukishaangalia kinyume) sababu za kutoendelea kwa makundi baada ya 1995, utakuja kupata sababu za kuendelea kwa makundi baada ya 2005. Hata hivyo, sababu kubwa kuliko zote ni kuvunjika kwa Uswahiba wa dhati kati ya Loawasa na Kikwete! Hata kama wanataka tuwaone kwamba bado ni marafiki, lakini ukweli ni kwamba, watu hawa hivi sasa ni mahasimu wakubwa hata kama hawakukutana bararani. Wakati Lowasa alikuwa tayari kutofanya kampeni za mapema kwa ajili ya 2005 ili amuunge mkono swahiba wake (JK), hivi sasa Lowasa huyo huyo hana sababu za kukaa kimya na kumwacha "swahiba" aongoze kwa amani kwavile tayari yeye Loawasa alishachinjiwa baharini na "swahiba" wake huyo huyo! Lowasa na wafuasi wake bado wanaamini KIkwete kama Rais bado alikuwa na uwezo wa kuzima anguko la Lowasa kupitia Richmond! Badala yake, Kikwete akamtosa(akamsaliti) Lowasa na hivyo Lowasa anaona heri nae amsaliti tu Kikwete! Huku Uswahilini, tunasema "kama mbwai, mbwai tu!"


MWENYE UWEZO WA KUVUNJA MAKUNDI CCM!!
Kama nilivyotangulia kusema hapo awali; Phillip Mangula hana ubavu wa kuvunja makundi yaliyopo CCM hivi sasa! Hata hivyo, watu wawili wana ubavu wa kuvunja makundi hayo.

1. MWENYEKITI WA CCM.

Huyu ndie mtu wa kwanza kabisa mwenye uwezo wa kuyavunja makundi yaliyopo hivi sasa kwa kuchukua maamuzi yanayostahili ambayo hivi sasa tumegeuza kuyaita "eti maamuzi magumu!" Kwa kumuheshimu Rais wangu, ningependa kutumia maneno kwamba tatizo la Kikwete ni silika yake ya ustahimilivu na subira. Lakini ukweli ulio wazi ni kwamba, ustahimilivu ukivuka mipaka unabadilika na kuwa udhaifu! Ustahimilivu wa Kikwete dhidi ya wahalifu mbalimbali umevuka mipaka na hivi sasa kugeuka kuwa si tena ustahimilivui bali ni udhaifu!! KIkwete akiamua kondokana na udhaifu wa kuchukua maamuzi basi makundi ndani ya CCM yatakaufa na kama yataendelea kuwapo, kamwe hayataweza kuwa ya wazi wazi kama sasa!

2. MKUTANO MKUU WA CCM.

Mkutano Mkuu unaoendelea hivi sasa una uwezo kabisa wa kuvunja nguvu za makundi yaliyopo CCM! Hapa panatakiwa awepo mtu mwenye ujasiri wa kumfunga paka kengele na kuibua hoja ambayo IN THE SHORT RUN itakiathiri chama lakini In the LONG RUN itakijenga chama!! Mkutano Mkuu wa CCM unatakiwa kuifahamu na kuitumia barabara saikolojia ya Watanzania! Watanzania walio wengi ni mashabiki wa TIMUA TIMUA! Watanzania wa leo hakuna lugha wanayopenda kuisikia kama ile ya "fulani ametimuliwa!" Hata mimi nilifurahi ile mbaya niliposikia Lyord Nchunga na wenzake wametimuliwa pale Jangwani! Hata wana-CHADEMA nao huwa wanahamasika ile mbaya wakiskia "madiwani wao" fulani wametimuliwa! Hii ni cheap political opportunity ambayo Mkutano Mkuu wa CCM inaweza kuitumia na kukifanya chama chao kupata kurejesha taswira ya chama!

Hivyo basi, wanachotakiwa Mkutano Mkuu wa CCM kufanya ni kuwataja wote wanaoonekana wanakidhoofisha chama na kupitisha azimio la kuwatimua!! Kuweka matumaini kwa Phillip Mangula ni kumwonea na katu HATAWEZA! Ikiwa rais mwenyewe ameshindwa, how come wamtarajie Phillip Mangula?! Kama alivyoshindwa Mkama, Mangula nae hataweza!! Mwenye uwezo huo ni yule mwenye extra-ordinary power ambae ni Mwenyekiti Rais pamoja na Mkutano Mkuu! Lakini kwavile Mwenyekiti Rais amesha-prove failure, basi mwenye uwezo huo kwa sasa ni Mkutano Mkuu unaoendelea!
 

NB: AWALI ya yote, niwatake radhi wasomaji kwa kuchanganya majina....nimetaja ni Pius Mangula badala ya Phillip Mangula!!! NI bahati mbaya sana nimeshindwa ku-edit heading!!!
 
Back
Top Bottom