Ni vigumu sana kuuza mradi unaozalisha.Bahati mbaya ni kuwa kuna watu wanaopiga hela kwenye biashara nyingine na wamedhani kwenye biashara ya dawa anaweza kupiga hela zaidi.Hali inakuwa tofauti sana mtu anapoingia kwenye biashara yenyewe.
Kwanza unalazimika kupata chumba/vyumba angalau 2 vizuri ambavyo malipo yake hayawezi kuwa kidogo.
Unatakiwa kumlipa mfamasia kwa ajili ya kuweka cheti ili upate kibali.Gharama ya kulipa ni kati ya 1M-1.6M kwa mwezi.Huyu anaweka tu cheti hauzi dawa!Inabidi utafute nesi wa kuuza dawa hizo ambaye naye utamlipa kila mwezi.
Changamoto kubwa ni kupata wateja.Unaweza kuta una dawa nyingi ambazo hazinunuliwi na zinaanza kuisha muda,wakati pengine una madeni,biashara ngumu,TRA wanaangalia vioo tu unakamuliwa!Kwa usalama wa roho akili na mwili,inabidi uuze pharmacy ukawekeze angalau kwenye biashara ya misumari.