Peter Msechu: Ninatukanwa sana sababu ya unene wangu

Bilionea Asigwa

JF-Expert Member
Sep 21, 2011
16,510
28,416
mSECHU%20_0.jpg


Msanii wa muziki wa bongo fleva Peter Msechu amefunguka na kusema kuwa amekuwa akitukanwa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu unene wake na kusema kuwa wapo baadhi ya watu walimfuata na kutaka kumpa dawa ili apunguze mwili wake.

Amesema licha ya kushawishiwa kwa hilo, yeye hataki kwa kuwa ameridhika na mwili huo.

Akiwa katika kipindi cha Planet Bongo Peter Msechu amesema mwanzo alidhani kuwa ni yeye tu anatukanwa kwa sababu ya mwili wake lakini akagundua kuwa si yeye tu kwani hata msanii AT naye alikuwa anazungumzwa vibaya kutokana na wembamba wake.

"Unajua nilikuwa natukanwa sana kwenye mitandao ya jamii juu ya unene wangu, wengine walikuwa wananishauri hata nitumie dawa kupunguza mwili lakini nikagoma kwa sababu mimi nimeridhika na mwili wangu, sema nikawa najiuliza hawa watu wanataka nini maana hata watu wembamba wanasemwa kuwa wana UKIMWI na mambo mengine mengi tu' Alisema Msechu

Mbali hilo, Msechu amesema alipokuwa kwenye kituo kimoja cha Radio alimchana AT kuhusu wembamba wake, lakini AT hakupenda jambo hilo na kwamba hiyo ndiyo ilikuwa sababu ya AT kuandika ujumbe kwenye mitandao kumchamba Msechu, na kuongeza kuwa walipoona jambo hilo limekuwa kubwa ilibidi waligeuze kama fursa kwao ili wafanye kazi ya pamoja kuhusu miili yao.

"Kuna siku nilimchana AT kwenye kituo cha Radio kumbe yeye hakupenda ndiyo akaandika ujumbe ule, mambo yakawa makubwa sana tukaona bora tuifanye fursa kwa kufanya wimbo wa pamoja' alisema Peter Msechu.

Source: Eatv.
 
Msechu anafuga maradhi.Mwili ule ni balaa.
Afanye mazoezi aache bia afanye diet.Yeye ni kioo cha jamii.
 
Itafika hata huko kucheza mziki jukwaani atashindwa atabaki kupunga mikono hewani. Yeye anaona sifa
 
Back
Top Bottom