pete wapendazo wadada na mabinti.

pete wapendazo wadada na mabinti.

nataka kumvisha pete mpenzi wangu, nimeaanda 20,000/=. Je ni pete rangi gani ambazo mabinti wanazipenda zaidi? Msaada wenu wanajamvi. Asanteni!

20,000? Majanga hayo.....hii inaonesha hujawahi kumgharamia zaidi ya 350,000? Mthamini mwenzio, Ukiwa kijana mfanye
afurahi, pete siyo swala la ghafla mpatie dhahabu nzuri , najua utapata nzuri mkuu at least kuanzia 100,000 hadi 1,000,000 hivi vitu havijirudiagi bana, vikipita vimepita. MAKE IT HAPPEN.
 
wadau nami ninashida hiyohiyo ya pete ya uchumba.
Uwezo wangu hauzidi laki na nusu. Je naweza pata pete nzuri? Na kwa dar, ni maduka gani naweza kupata?
Vp kuhusu size ya kidole, nitahakikisha vp haiwi over size ntakapoenda kununua?

Natanguliza shukrani.
 
Kwa hilo dau utapata ilosokota na yale makaratasi ya dani ya pakti. Za sigara full silver,
 
Mwaya wasikudanganye,
Hiyo hiyo elfu 20 yako pita hapo
mitaa ya kwa mangi nunua pete ya
rangi ya blue kamvishe mchumba wako.

Pengine ndo penzi litadumu hata kuliko
wale wengine wa malaki na mamilioni.
 
ninachoona hapa wengi hawanunui pete ila wananunua madini....ila naamini kwa elfu 20 unapata pete nzuri tu....
unless unasema unataka kumtafutia pete ya madini fulani.
 
kuna wale wauza urembo kwenye vikapu huwa wanapita mitaani, wasubiri hao mkuu utapata ya buku nadhani. haya mambo nadhani huyawezi mweleze tu mchumba kuwa huna uwezo asubiri pete ya ndoa ambayo na kwa 70,000 hutapata.

hahahahahahahahHa...
 
Hapo unapata Pete 3 za ndoa, kwa machinga na unabaki na cheji ya tshs 5000.

yaan ww siasa hadi kwenye haya mambo kumbee! dooh acha izooo.

na we mleta mada pete gan siku iz sijui elf 20 au 60?? me naona kama ujipange tena usije kumchosha buree bride to be looolz!
 
Back
Top Bottom