DOGofGOD
JF-Expert Member
- Feb 15, 2015
- 1,341
- 481
Amani kwenu wadau,
Unakutana na wanandoa ambao siku ya harusi yao walifanya shehere ya harusi ya gharama kubwa sana.Na mamilioni ya shilingi yalikatika kwa ajili ya gharama za kukodi ukumbi,usafiri,chakula vinywaji na mbwembwe nyingine.
Lakini ukichunguza maisha ya wanandoa hao baada ya kumaliza shehere ya harusi kusema kweli inatia huruma.Unakuta wanaendelea kuishi maisha ya kuungaunga.
Nadhani muda umefika sasa hizi kamati za shehere.Ziangalie upya bajeti zao kiasi ambacho badala ya kutumia kiasi chote kinachokusanywa kukodi kumbi za kifahari na kuintateini waalikwa.Angalau wajitahidi kutumia nusu ya bajeti yao katika mambo ya sherehe na nusu inayobaki wapewe wanandoa ili ziwasaidie kupata mitaji ya kuanzia maisha.
Sababu mojawapo ya ndoa nyingi kuvunjika ni ukata uliopo katika familia.cause ukata ndio chanzo cha migogoro mingi inayopelekea ndoa nyingi kuvunjika.Kwahiyo kama wanandoa watapewa mitaji itasaidia kupunguza migogoro ambayo ndio chanzo cha tatizo la ndoa kuvunjika.
Kiepe a.k.a Baba Prosper
Unakutana na wanandoa ambao siku ya harusi yao walifanya shehere ya harusi ya gharama kubwa sana.Na mamilioni ya shilingi yalikatika kwa ajili ya gharama za kukodi ukumbi,usafiri,chakula vinywaji na mbwembwe nyingine.
Lakini ukichunguza maisha ya wanandoa hao baada ya kumaliza shehere ya harusi kusema kweli inatia huruma.Unakuta wanaendelea kuishi maisha ya kuungaunga.
Nadhani muda umefika sasa hizi kamati za shehere.Ziangalie upya bajeti zao kiasi ambacho badala ya kutumia kiasi chote kinachokusanywa kukodi kumbi za kifahari na kuintateini waalikwa.Angalau wajitahidi kutumia nusu ya bajeti yao katika mambo ya sherehe na nusu inayobaki wapewe wanandoa ili ziwasaidie kupata mitaji ya kuanzia maisha.
Sababu mojawapo ya ndoa nyingi kuvunjika ni ukata uliopo katika familia.cause ukata ndio chanzo cha migogoro mingi inayopelekea ndoa nyingi kuvunjika.Kwahiyo kama wanandoa watapewa mitaji itasaidia kupunguza migogoro ambayo ndio chanzo cha tatizo la ndoa kuvunjika.
Kiepe a.k.a Baba Prosper