Mapenzi ni kitu cha Ajabu sana. Mapenzi yaweza kumea mahala popote bila kujali lolote.
Compaund ambayo nakaa ina Nyumba 4 zote ni za kupangisha. Tumepanga watu tofauti kila mmoja na shughuli yake kama unavyojua mambo ya mjini.
Jirani yangu kuna Dada anakaa. Ila sina mazoea nae. Zaidi ya kusalimiana tuu na vile mini sio mtu wa kukaa sana nyumbani hivyo huwa hatuonani sana.
Last week night moja nilisikia mlango wangu unagongwa mida ya saa 3 usiku. Nilikuwa jikoni nakaangiza kidogo nile. Alikuwa huyo jirani mrembo. Mkononi alikuwa Ameshi Ki Remote cha mita ya LUKU.
Nikamkaribisha akaingia Sebuleni kisha nikamwita hadi jiko. Nika mkaribisha, tukasalimiana, akaniambia umeme kwake umeisha hivyo amekuja kwangu ili aweze kuingiza. Nikamwambia endelea. Akawa yupo kwenye Extension ya TV anaweka luku yake.
Nikapunguza moto jikoni nikamfuata nikamsaidia akafanikiwa.
Nikaongea ki utani tuu kwamba chakula kipo tayari aje kula, akasema ana njaa lakini anajisikia uvivu kupika ndo kwanza anafika nyumbani ngoja akaoge kwanza.
Akaenda akaoga. Baada ya nusu saa hivi akawa amekuja na Track suit yake basi nikamkaribisha tukawa tunakula Ugali, Mayai na matunda. Tumekula tukawa tunapiga story za kawaida, nikamuomba na mm nikaoge kwanza nikaoga tukawa tupo Sebuleni tunachek mechi ya Afcon
Mida ya saa 6 hivi akawa anataka kulala, nikamwambie nikusindikize kwako basi for first time ndo naingia kwake, nikapiga porojo mbili tatu nikamuuliza nakuagaje sasa.?? Akasema vyovyote. Basi nikamkumbatia akawa kafumba macho akasema asante nikaondoka.
Nikaingia ndani nikalala. Mida ya saa 8 hivi nasikia Geti linagongwa, nikasogea nikauliza we nani? ( Mimi jakiiiii) basi nikafungua mlango nikamuuliza vipi mbona usiku vipi?
Akasema unajua sina namba yako ya simu,? Nikamuuliza ndo usiku huu sasa mbona hukusena saa ile. Nikaona dalili fulani sizielewi. Basi nikafungua Geti akaingia. Tukaelekea chumbani tukalala
Asubuhi akaamka akaenda kwake. Akajiandaa akaenda kwenye mishe zake.
Sasa hivi ndo umekuwa mchezo. Hakuna siku nalala peke yangu. Tunaamua tu tulale wapi. Tukipika kwangu tunalala kwangu. Tukipika kwake tunalala hapo hapo.
Design sasa amekuwa kama mke. Japo kila mtu ana maisha yake