Pengine Zitto hana kosa....

Pengine Zitto hana kosa....

Highlander

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2012
Posts
3,093
Reaction score
1,077
Nimewiwa kumtetea Zitto Kabwe na Freeman Mbowe na Dk. Wilbrod Slaa. Nina mashaka sana hakuna mwenye makosa, na kwamba tunachokiona kama machafuko katika CHADEMA katika hizi siku mbili tatu unaweza uwe ni mgongano tu wa taaluma mbili ndani ya Chama.

Kama Zitto Kabwe alipata Elimu ya Political Economy pale Chuo Kikuu Mlimani au kwingineko, yeye ni Mwanasiasa wa Kusomea. Sifa za Wanasiasa duniani zinajulikana. Ni watu wa kutafuta sifa, kujikweza na kutaka dunia nzima isikie na kujua kwa uhakika ni kipi hasa walichofanya.

Kwa hiyo Siwezi kushangaa kama nitasikia Zitto Kabwe akijisifia kupandisha bendera ya CHADEMA akiwa na umri wa miaka 16. Huyu ni mwanasiasa wa kusomea, na hapo atakuwa anafanya siasa kadri ya mafunzo yake.

Nasita kumzungumzia sana Dk. Kitila Mkumbo kwa kuwa hakuna ninachokijua zaidi ya kwamba ni Mwalimu wa Chuo Kikuu. Lakini wote tunajua huwezi kumtenga sana mwalimu na siasa kwa kuwa hii ni taaluma inayohusu kujieleza, na mwanasiasa sharti ajue kujieleza. Kwa hiyo naomba nimwite Dk, Kitila Mkumbo kuwa na yeye ni mwanasiasa wa kusomea.

Nitamjadili zaidi Zitto Kabwe hapa kwa sababu mzozo unaoonekana kuwapo katika CHADEMA leo unaonekana kuwahusu zaidi watu wawili hata kama wengine wameingizwa humo: huu mgogoro unamhusu Zitto Kabwe na Freeman Mbowe.

Freeman Mbowe ni Mfanyabiashara kama mimi, japokuwa tunapishana viwango kwa mbali kama ardhi na nyota. Lakini ndege ni ndege tu—awe analala katika banda au kwenye mti; watakuwa na mambo yanafanana.

Sisi wafanyabiashara huwa tahupendi urasimu. We are doers. Kikao cha familia kikishakubaliana kuwa tunataka duka lijengwe hivi mahali, lipakwe rangi hii, tuweke nondo kwenye madirisha. Kitu cha muhimu ambacho huwa kinabakia hapo huwa ni results! Siyo Nani katoa hela, zilitoka saa ngapi, mkono gani ulizishika wakati zinatoka na upuuzi mwingine wa kuchelewesha results.

Nimeamka mapema sana leo kuandika mawazo haya kwa sababu sitaki kuona ugomvi katika CHAMA tegemeo la wananchi baada ya “CHAMA kaka” kuharibiwa. Pengine ni kweli Mbowe kafanya unilateral decisions katika mambo yanahusu fedha. Naamini hilo litakuwa lilifanywa kuharakisha results. Urasimu una desturi ya kuchelewesha sana results. Nionavyo mimi Chama kimefanya mambo mengi sana mazuri na kuna mafanikio makubwa yamefikiwa na yanaonekana hadi hapa tulipo chini ya uongozi wa Mbowe.

Tatizo ni kwamba mambo yanayofanywa na fedha za chama hayajapeleka sifa kwa kila mwanasiasa ambaye angependa fedha za CHAMA zitumike kumpa sifa na yeye pia. Hapa kuna tatizo la sifa!

Naamini Mbowe hajaiba fedha CHADEMA kama kambi ya Zitto inavyotuhumu. Naamini kinachoelezwa kuwa udikteta wa Freeman Mbowe katika CHADEMA ni mgongano wa mitizamo ya utendaji unaojitokeza kutokana na taaluma mbili kugongana. Zitto Kabwe angependa kila kinachotendeka kilete sifa kwake pia. KInachotendeka pale katika chama kinaleta sifa kwa mtu mmoja tu anayeamua kipi kifanyike.

Inawezekana kabisa ni kweli Mbowe anafanya maamuzi ya kiimla. Wafanyabiashara wengi wapo hivyo mara nyingi kwa sababu ya kuwahi kukamilisha lengo. Tupo Goal Oriented. Na ni rahisi sana kuwakwaza watu katika mazingira hayo kutokana na sifa za manunuzi say ya pikipiki zinunuliwe wapi kutokumpatia sifa na Zitto Kabwe. Maswali ambayo napenda kusikia wanaCHADEMA wakiuliza ni haya: Mbowe kaiba Sh. Ngapi? La pili likiwa hili: kwamba ni kitu gani katika manunuzi ya CHAMA kilipangwa kufanywa ili kufaidisha chama hakijafanywa na kufaidisha chama?

Hoja ya Umamluki wa Zitto nayo inaweza kupata maelezo: kwamba taaluma ya upelelezi tangu mwanzo wa historia ya binadamu imehusu neno moja tu katika lugha ya Kiingereza--neo EMBED.

Ku-embed ni kupandikiza mtu miongoni mwa jamii inayopelelezwa kwa namna ya kumwezesha kuonekana ni mmoja wao. Mpelelezi anayefaulu katika kazi yake ni yule anayemudu ku-embed mwenyewe, au kwa kuwezeshwa. Kwa maana hiyo, mpelelezi mzuri atazungumza lugha ya wenyeji, atavaa mavazi ya wenyeji, atakula chakula cha wenyeji, atafanya biashara kama wenyeji, hata atazaa na wenyeji, atakuwa mmoja wao, ataishi kama wao. Kumtambua mpelelezi aliye-embed vizuri ni ngumu sana. Unaweza usijue milele yote. Kwa wale waliosoma Biblia mifano ni mingi mule, mzuri kuliko yote ukiwa mfano wa Mpelelezi Delila, ambaye alitumia mbinu inayoitwa “honey trap” kumpeleleza Samsoni kwa niaba ya Wafilisti.

Waliobobea katika taalum ya upelelezi watasema njia pekee ya kumtambua mpelelezi miongoni mwenu ni kusoma “associations zake” nje yenu. Associations za nje ni mahusiano yake na watu waliopo nje ya kundi lenu. Kwa hiyo mtatizama mahusiano yake na watu kitaaluma, kidini, kimapenzi, kibiashara, kimichezo kwa namna iwayo yote itayoweza kutoa picha ya associations za suspect.

Mkipata undani wa hizo associations zake sasa mtasikiliza huwa anasema nini anapokutana na hao watu katika associations zake kwa siri. Mtamsikiliza kwa kutumia njia halali au njia haramu; au vyote kwa pamoja ikibidi. Kujua sana ilani za chama, na katiba zake, na sera zake, na historia yake, SI sababu tosha kumtoa mtu kwenye list ya mapandikizi. Pandikizi anatakiwa kuvijua vyote katika chama anachokipeleleza, sawasawa kabisa na shetani anavyojua vifungu katika Biblia.

Ili kujua kama Zitto ni Jasusi wa CCM, labda sasa CHADEMA watuambie waliupata wapi huu waraka unaoitwa mpango wa hujuma. Je waliupata kwenye Kambi ya CCM? Je waliupata kwenye associations zake nje ya chama?

Mwisho napenda kuwasihi WANACHADEMA kukubali kwamba pengine Zitto hana makosa. Na kama huu ndo ukweli, basi naomba Mbowe na Dk. Slaa watoe majibu ya haraka kuhusu kila alicholalamikia Zitto.
 
Zito angekubali kuitwa john Paulo angekubalika chadema ila na uzuberi wake unatarajia nini? Chadema inamsafisasha aliyekubali kutenda makosa wazi ambaye ni dr. Kitila na kumshambulia anayetuhumiwa. Double standard inayosababisha na nguvu ya kiimani. Ni mtazamo yangu.
 
Sasa hisia kwenye jambo hili zimekuwa nyingi...wengi tupo dilema kwamba nani mkweli..kwa kuwa kuna watu wameshika makali na wengine mpini kwenye suala hili. Labda maoni yako yatafanyiwa kazi.
 
Utofauti ni kuwa Mbowe ni mhafidhina na dictator ambaye anapata maelekezo ya chama kutoka kwa mkwe wake hivo basi mtazamo wake wa chama ni wa ukanda ndo maana nyuma yake kuna Lema,Nassari(ukanda mmoja),yuko too local na hana exposure na ZZK ni mwanamapinduzi wa kiuchumi na kisiasa mwenye vision ya kitaifa na ana international exposure
 
All in all huku mwisho ni good analysis,kama angekua ni spy wa CCM sidhani kama angekua karibu na associations za ccm ili akamilishe lengo!!kwa hilo dogo tu wafuata upepo wengi wameshindwa kung'amua!!
 
Sasa hisia kwenye jambo hili zimekuwa nyingi...wengi tupo dilema kwamba nani mkweli..kwa kuwa kuna watu wameshika makali na wengine mpini kwenye suala hili. Labda maoni yako yatafanyiwa kazi.

nakubaliana nawe kabisa. wanachama wengi wapo katika dilema. mimi nimeandika mawazo haya ikiwa tafakuri ya kutafuta a way out of the dilema. lakini pia naamini njia ambayo ni sahihi ni kutafuta compromise ya hizi kambi mbili. na harakaharaka nadhani compromise inawezekana kabisa kutafuta neutral group ipewe madaraka--tena haraka. Na sijui ni nani atayewezesha hili kutokea. kuleta neutral people kwenye safu ya uongozi itaondoa hisia ya either group kushinda. chadema ni chama kikubwa kuliko kinavyoonekana machoni pa watu. kwa hiyo hapatakuwepo shida kupata neutral group. tatizo nani awezeshe hilo?
 
Kamati kuu imeishanawa mikono na kilichobaki ni kupeleka mapendekezo ya kwenye vikao vya Baraza Kuu na Mkutano Mkuu kuridhia baraka zake.

Mh. Zitto na crew yake wamesema hawana makosa na kwa sababu hawana makosa, hawawezi kuondoka kwa hiari yao ndani ya CHADEMA labda wasukumwe kwa "hoja za nguvu" nje ya mlango wa CHADEMA.

Mh. Zitto hawezi kuomba msamaha kwa sababu anafahamu na kuamini hana kosa bali ni unsubstantiated claims na siasa za majitaka ndizo zimemuhukumu hata Dr. Kitila hakubaliani na maamuzi ya Kamati Kuu.

Kumuacha ndani ya CHADEMA utakuwa ni ushindi kwa Mh. Zitto kutokana na hoja zake na kwa kufanya hivyo, kutampa nguvu ya kisiasa ndani na nje ya CHADEMA.

Kumnyang'any'a uanachama ni kufungua mlango wa mapambano ya kisiasa kwenye majukwaa ya kisiasa nje ya CHADEMA mpaka uchaguzi mkuu kwa sababu kuna uwezekano mkubwa akakata rufaa mahakamani na serikali ya CCM ikachelewesha hukumu ili minyukano ya kisiasa ikidhoofishe CHADEMA kwanza kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa na pia upatikanaji wa Katiba mpya.

CHADEMA kwa sasa wamebeba bomu la kisiasa na kilichobaki ni hekima na busara kutumika katika ku-defuse.
 
Zito angekubali kuitwa john Paulo angekubalika chadema ila na uzuberi wake unatarajia nini? Chadema inamsafisasha aliyekubali kutenda makosa wazi ambaye ni dr. Kitila na kumshambulia anayetuhumiwa. Double standard inayosababisha na nguvu ya kiimani. Ni mtazamo yangu.

Ni mtazamo hafifu sana. Hivi David Kafulila ni dini gani? Karata ya kidini anayoishikilia Zitto haitamsaidia bali itamwangamiza! Nyerere aliwahi kusema kuwa ukiona mtu anatumia udini kutafuta umaarufu amafilisika kisiasa!
 
Kamati kuu imeishanawa mikono na kilichobaki ni kupeleka mapendekezo ya kwenye bikao vya Baraza Kuu na Mkutano Mkuu kuridhia baraka zake.

Mh. Zitto na crew yake wamesema hawana makosa na kwa sababu hawana makosa, hawawezi kuondoka kwa hiari yao ndani ya CHADEMA labda wasukumwe kwa "hoja za nguvu" nje ya mlango wa CHADEMA.

Mh. Zitto hawezi kuomba msamaha kwa sababu anafahamu na kuamini hana kosa bali ni unsubstantiated claims na siasa za majitaka ndizo zimemuhukumu hata Dr. Kitila hakubaliani na maamuzi ya Kamati Kuu.

Kumuacha ndani ya CHADEMA utakuwa ni ushindi kwa Mh. Zitto kutokana na hoja zake na kwa kufanya hivyo, kutampa nguvu ya kisiasa ndani na nje ya CHADEMA.

Kumnyang'any'a uanachama ni kufungua mlango wa mapambano ya kisiasa kwenye majukwaa ya kisiasa nje ya CHADEMA mpaka uchaguzi mkuu kwa sababu kuna uwezekano mkubwa akakata rufaa mahakamani na serikali ya CCM ikachelewesha hukumu ili minyukano ya kisiasa ikidhoofishe CHADEMA kwanza kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa na pia upatikanaji wa Katiba mpya.

CHADEMA kwa sasa wamebeba bomu la kisiasa na kilichobaki ni hekima na busara kutumika katika ku-defuse.

Nimeipenda sana sentensi yako hii: "CHADEMA kwa sasa wamebeba bomu la kisiasa na kilichobaki ni hekima na busara kutumika katika ku-defuse."

ku-defuse bomu hili ni kufanya uchanguzi haraka, na ije timu mpya ambayo itatumia busara za timu ya zamani zitazoonekana kufaa kutoka kwenye pande zote. CHADEMA siyo Zitto, Mkumbo, Mbowe na Slaa peke yao. Dawa ni kutoa wote tuokoe chama.

Ujue hii tiba ninayoipendekeza hapa hata kule CCM inawafaa kabisa. Dawa ya kuondoa yale makundi ni kufutilia mbali kambi zote zinazojulikana na kuweka watu neuetral kule na chama kingepona.

Watanzania na pengine binadamu kwa ujumla tunakuwa na fikra potofu kuwa watu maarufu ndiyo suluhisho la matatizo ya chama au niseme vyama. Tunasahau kuwa wale watu maarufu huwa wanatengezwa na chama. Hawajitengezi wenyewe. Kwa hiyo kutengeza watu maarufu wengine ni possibility kubwa kabisa.

Tupilia mbali wote wawili, Zitto na Mbowe tuokoe chama! Full stop. CCM wengeweza kufutilia mbali kina Mwandosya, Kikwete, Lowasa na kutafuta watu wapya kabsaaaa, na chama kingepona siku nyingi.

Na ninadhani wanachama ndio wenye rungu hili. Umaarufu kitu gani bana.... Bila Chama mbowe na zitto wangepata wapi huo umaarufu? To hell with names....

They should shape up, or ship out!
 
Mtoa mada unataka Dr Slaa na Mbowe waeleze walichoiba? Nijuavyo mimi aliyejenga dhana ya wizi ndie anayetakiwa athibitishe maneno yake, otherwise ataonekana muongo. Kama kibaraka wenu Zitto ana ushahidi wa wizi anajua wapi apeleke taarifa ili zifanyiwe kazi, sio majukwaani!
 
Last edited by a moderator:
Nimeipenda sana sentensi yako hii: "CHADEMA kwa sasa wamebeba bomu la kisiasa na kilichobaki ni hekima na busara kutumika katika ku-defuse."

ku-defuse bomu hili ni kufanya uchanguzi haraka, na ije timu mpya ambayo itatumia busara za timu ya zamani zitazoonekana kufaa kutoka kwenye pande zote. CHADEMA siyo Zitto, Mkumbo, Mbowe na Slaa peke yao. Dawa ni kutoa wote tuokoe chama.

Ujue hii tiba ninayoipendekeza hapa hata kule CCM inawafaa kabisa. Dawa ya kuondoa yale makundi ni kufutilia mbali kambi zote zinazojulikana na kuweka watu neuetral kule na chama kingepona.

Watanzania na pengine binadamu kwa ujumla tunakuwa na fikra potofu kuwa watu maarufu ndiyo suluhisho la matatizo ya chama au niseme vyama. Tunasahau kuwa wale watu maarufu huwa wanatengezwa na chama. Hawajitengezi wenyewe. Kwa hiyo kutengeza watu maarufu wengine ni possibility kubwa kabisa.

Tupilia mbali wote wawili, Zitto na Mbowe tuokoe chama! Full stop. CCM wengeweza kufutilia mbali kina Mwandosya, Kikwete, Lowasa na kutafuta watu wapya kabsaaaa, na chama kingepona siku nyingi.

Na ninadhani wanachama ndio wenye rungu hili. Umaarufu kitu gani bana.... Bila Chama mbowe na zitto wangepata wapi huo umaarufu? To hell with names....

They should shape up, or ship out!
Siasa za nchi za Kiafrika na nchi za Magharibi zitaendelea kuwa kama mbingu na dunia kwa sababu Waafrika hatuko tayari kuvaa nguo za demokrasia ya nchi za Magharibi pamoja na kuikubali na kujaribu kuisimika katika uendeshaji wa vyama vya siasa na nchi.

Kwa wenzetu kukitokea migogoro kama hii ya kiuongozi ndani ya vyama, huwa wanaitisha uchaguzi na kujua mbivu na mbichi lakini sisi ni kinyume chake ambapo huwa tuna ahirisha uchaguzi kwa madai ya machafuko ili kuwashughurikia kwanza wanaoleta chokochoko za kidemokrasia. Ndiyo maana matatizo hayaishi kwa sababu kinachofanyika ni kuyasogeza mbele.

CHADEMA walikuwa wameamua watafanya uchaguzi wa ndani kabla ya mwaka kikatiba ili kuepuka kigongano ya uchaguzi wa serikali za mitaa na mchakato wa katiba lakini kwa sasa nimeanza kuamini kuwa viongozi wa CHADEMA waliamua kutokufanya hivyo baada ya kupata mnuso kama kuna kikundi kinajiandaa katika harakati hizo. Kinachofanyika kwa sasa ni kuwashughulikia kwanza wanaoleta chokochoko za kidemokrasia ili njia iwe ni nyeupe.

Hata kama CCM wangekuwa wako upinzani tungeona sarakasi kama hizi za CHADEMA lakini kwa sasa wanasaidiwa na dola ndiyo maana wanaweza kuendelea kuonekana kama makundi hayaathiri chama kiutendaji.
 
Ni mtazamo hafifu sana. Hivi David Kafulila ni dini gani? Karata ya kidini anayoishikilia Zitto haitamsaidia bali itamwangamiza! Nyerere aliwahi kusema kuwa ukiona mtu anatumia udini kutafuta umaarufu amafilisika kisiasa!

Nyerere sio msahafu na ukweli hakuna kinamuangamiza zito zaidi ya dini, kabila lake na kanda atokayo. Yeye mwenyewe kaligusia hilo kuwa kama mtu ananyanyaswa bila makosa ya wazi je wale wanaodhani kuna udini, ukabila au ukanda si watasema au kupata nguvu katika madai yao? Na huo ndio ukweli kwani anachoogopa zito ni kusema wazi jambo hilo.
 
Nyerere sio msahafu na ukweli hakuna kinamuangamiza zito zaidi ya dini, kabila lake na kanda atokayo. Yeye mwenyewe kaligusia hilo kuwa kama mtu ananyanyaswa bila makosa ya wazi je wale wanaodhani kuna udini, ukabila au ukanda si watasema au kupata nguvu katika madai yao? Na huo ndio ukweli kwani anachoogopa zito ni kusema wazi jambo hilo.
CHAMVIGA hivi Mansour ni dini gani??


Mbona madai yake ni ya msingi na bado mmemtimua??

Hamkumkandamiza sababu ni Mzanzibar?
 
Last edited by a moderator:
CHAMVIGA hivi Mansour ni dini gani??


Mbona madai yake ni ya msingi na bado mmemtimua??

Hamkumkandamiza sababu ni Mzanzibar?

waliomfukuza Mansoor wamekosea na nilisema wazi msimamo wangu na yote hayo ni kuulinda muungano usiotakwa na watanzania.
 
Last edited by a moderator:
Ni mtazamo hafifu sana. Hivi David Kafulila ni dini gani? Karata ya kidini anayoishikilia Zitto haitamsaidia bali itamwangamiza! Nyerere aliwahi kusema kuwa ukiona mtu anatumia udini kutafuta umaarufu amafilisika kisiasa!

Ni vizuri ukajibu suali.Ni kweli Chama kinamsafisha Dkt.Mkumbo ambaye AMEKIRI makosa na kumhukumu Mh.Kabwe ANAYETUHUMIWA kufanya makosa.Ikiwa ni kweli jiulize inakuwaje anayekubali makosa anasafishwa na anayetuhumiwa anahukumiwa.Halafu uje sasa kwa huyo Nyerere wako.Hapa utakuwa umetenda haki nionavyo mimi.
 
Nyerere sio msahafu na ukweli hakuna kinamuangamiza zito zaidi ya dini, kabila lake na kanda atokayo. Yeye mwenyewe kaligusia hilo kuwa kama mtu ananyanyaswa bila makosa ya wazi je wale wanaodhani kuna udini, ukabila au ukanda si watasema au kupata nguvu katika madai yao? Na huo ndio ukweli kwani anachoogopa zito ni kusema wazi jambo hilo.

kwahiyo wewe umeamua kumsemea? wewe akili yote inagotea kwenye dini? think big!
 
CHAMVIGA hivi Mansour ni dini gani??


Mbona madai yake ni ya msingi na bado mmemtimua??

Hamkumkandamiza sababu ni Mzanzibar?

Kwani Mansour yuko Chadema.Hayo ni ya CCM.Hapa yanaongelewa mambo ya Chadema.Usitake kuvurugu mada vinginevyo kuna kitu kinafichwa.
 
Last edited by a moderator:
Utofauti ni kuwa Mbowe ni mhafidhina na dictator ambaye anapata maelekezo ya chama kutoka kwa mkwe wake hivo basi mtazamo wake wa chama ni wa ukanda ndo maana nyuma yake kuna Lema,Nassari(ukanda mmoja),yuko too local na hana exposure na ZZK ni mwanamapinduzi wa kiuchumi na kisiasa mwenye vision ya kitaifa na ana international exposure

Tunapokuwa tunaanza kutafakari hoja kwa kina, akina hawa wanajibwaga na mambo yasiyosaidia kufikisha hoja kwenye uelewa MPEVU. Angalia hata maneno ya huyu hapo juu. Sijui ni taswira gani itakuwa imekuwa-delivered. Unapoleta maneno kama haya, mlengwa anakuwa ni nani? Goal linakuwa ni nini? Kama nikutarajia kuwabadilisha wapenzi wa uliyemsema ili wamchukie huko si kuonyesha chongo huku wao wakiona ni kengeza? Huna na namna nyingine ya kuwasilisha hoja yako na ika-sink kuliko kuharibu muda wako. Tuseme na wewe ni great thinker? Unadhani kwa hivi uwezo wako utaendelea kuaminika? Be serious.
 
Ng'wamapalala, Umeliweka vizuri..... Kamati kuu imefanya a Political gamble! itakicost chama.... si zitto tu....na wote waliohusika katika sakata hili
 
Bwana Highlander,pamoja na mawazo yako mazuri ya kuelimisha,naomba nikuulize swali moja:
Wakati Zitto anaenda kujibu tuhuma pale Serena hotel;ukumbi ule ambao angeutumia Zitto kujibu mapigo,uliandaliwa na kupambwa na Stellah Mwampamba na baadhi ya vijana wa ccm;---- uhusiano gani hapo?
 
Back
Top Bottom