Pendekezo: Waziri anayeshughulikia Misaada ya Kigeni

Pendekezo: Waziri anayeshughulikia Misaada ya Kigeni

Nadhani kuna kitengo maalum cha "Aid management and external funding" ndani ya wizara ya fedha. Sidhani kama kuna haja ya kuwa na wizara kwaajili ya hili tu.
Ata huko kwao ivyo ivyo hao watu ni junior ministers (manaibu) sio mawaziri wanaondesha wizara kamili.
 
Kama biashara za ndani zinazidi kufa, hayo mapato yatatoka wapi tuweze kujiendesha bila misaada yao?

Ningetegemea kwanza muinue hali ya kipato ya mwananchi mmoja mmoja, pesa itakapokuwa nzuri kwenye mzunguko ndio uje na mpango kama huo, lakini kuja na mpango huo wakati huu bado tunaomba misaada ya kumalizia Nyerere Dam, na SGR, kwangu naona ni ndoto.
Umejuaje biashara za ndani "zinazidi kufa"?
 
Kwa nchi yenye miaka zaidi ya nusu karne toka ipate Uhuru ni fedheha kuwa na wizara ya kushughulikia misaada tunayopokea.

Hatuwezi kuwa ombaomba milele hivyo hakuna ulazima kuanzisha wizara ambayo inakinzani na malengo yetu ya kujitegemea.

Tunawahubiria raia wetu kuhusu kujijengea uwezo wa kujitegemea kama taifa alafu tunaanzisha wizara ya kuratibu upokeaji wa misaada huko ni kuwachanganya wananchi na siasa za kihuni hizo.
Hujaelewa mada.
 
Tujiandae kufunga mkanda. Wazungu hawawezi kutoa hela zao halafu CCM inacheza na Haki za raia. Hii miaka mitano ya magufuli itakua migumu katika historia ya nchi hii tangu tupate uhuru.
Ndio tupate akili. Kweli wangesitisha misaada
 
JPM kasema anaweza kuendesha nchi bila misaada nyie mnapiga ramli humu. Walimnyima pesa za barabara 4 yeye akaamua kujenga 8 na hadi leo hii hajakwama. Mwacheni JPM ainyooshe nchi nyinyi mlizoea kila duka mkiingia ma-generator yanawapigia kelele. Tanzania ni tajiri na ni kweli, hatuwezi kuwa makuwadi wa wale ambao wanaiba bila huruma rasilimali zetu. Watanzania badilikeni na hizi elimu za kitumwa we can make it so long as everyone understands what we want, and how we can reach there.

Miradi ya kimkakati, SGR, kufufuliwa kwa reli ya zamani, JNHPP pamoja na Bomba la mafuta kutoka Uganda ni kichocheo kikubwa kukuza uchumi wetu. Nani kabla ya JPM kuingia madarakani alifikiri Tanzania inaweza kuwa na import cover ya miezi 6?
 
Nayaona kwa macho yangu, leo nimeona hoteli ya Ngurdoto imekuwa hosteli!.
Hiyo ni biashara kama nyingine.

1606938509753.png


Debenhams set to close all stores with possible loss of 12,000 jobs (msn.com)
 
Napendekeza jina la wizara. Itaitwa wizara ya mabeberu.
 
Back
Top Bottom