Pendekezo: Wakuu wapya wa Mikoa na Wilaya

Pendekezo: Wakuu wapya wa Mikoa na Wilaya

fasiliteta

JF-Expert Member
Joined
Jul 2, 2014
Posts
2,598
Reaction score
4,472
Kwa jinsi ninavyoona muelekeo wa serikali baada ya kifo Cha JPM na kumpata Rais mpya Mama Samia Suluhu, ni wazi sasa panga pangua ya safi ya uongozi unaendelea ili mama apate cream yake ya kuliendesha gurudumu hili pamoja na kujarbu kurekebisha mapungufu madogo madogo ya mtangulizi wake yasijirudie.

Ameanza na wizara mbalimbali kaja makatibu wakuu na wakuu wa Taasisi za serikali. Ni wazi sasa wanaofata ni:
  • Wakuu wa mikoa
  • Wakuu wa wilaya
  • maDED
  • maDAS n.k.

Si vibaya pia kwa jicho la tatu kama wananchi tunaweza kutoa maoni yetu na pendekezo kwa nafasi hizi mbalimbali hasa wakuu wa mikoa na wilaya kama akipita humu aangalie sehemu ya wananchi wake Wana maoni gani kabla hajamalizia kufanyia kazi anayoendelea kuyapanga.

Binafsi namuona GODWIN GONDWE.

Apande cheo kutoka kua mkuu wa wilaya kua mkuu wa mkoa.

Jamaa ni mchapakazi sana na hana majivuno. Pamoja na umaarufu wake lakini anajishusha kwa wananchi. Ni mkuu wetu wa wilaya ya Temeke. Mimi kama raia nimemshuhudia Mara nyingi akitatua kero za watu na ukimsimamisha anasimama na kusikiliza kabisa na hata raia wengi wa Temeke ukiwauliza watakwambia hilo hilo.

Wananchi wengi tunatamani kesi zetu na shida zetu nyingi ziishie kwa wakuu wa wilaya au mikoa na si mpaka kwenda wizarani au Rais na kupata ufumbuzi na si majibu ya hovyo na nenda rudi kila siku Kama wakuu wengi wa wilaya wanavyosumbua wananchi wake.

Hakika GONDWE ni kiongozi haswaa.

Namuona pia Dada yetu JOKATE anavyopambana. Ni muda muafaka sasa akabiziwe mkoa wa Pwani ili aendelee kuutengeneza zaidi.

Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Mh. Kunenge aendelee huyu huyu maana hana papara kabisa. Huko mikoani pia tuangalie.

Nawasilisha
 
Makonda hatakiwi popoteee

Enz za jiwe alikuwa anafanya kaz kama Gestapo, si unawajua hawa Gestapoz, enzi za utawala wa Hitler, hawa walikuwa ni askar wa rank flan ya Kati tuh, wala hawakuwa wakubwa ila walikuwa wanareport direct kwa Hitler, na Hitler alikuwa anawaamin sana.

Sasa gestapo makonda bashite amebakia kama kifaranga yatima ambae kila muda mwenye wanaruka ruka juu yake Ili wamfanye kitoweo.
 
Mmeanza kupiga debe! It is Too early. Muiache mamlaka ya uteuzi itekeleze majukumu yake kikatiba, miluzi Hii kutoka kila upande ikizingatiwa mbwa atapotea mapema sana.
 
Msimchanganye Samia wa watu maacheni ateue kwa utulivu
 
Enz za jiwe alikuwa anafanya kaz kama Gestapo,si unawajua hawa Gestapoz,enz za utawala wa hitler,hawa walikuwa ni askar wa rank flan ya Kati tuh,wala hawakuwa wakubwa ila walikuwa wanareport direct kwa hitler,na hitler alikuwa anawaamin Sana,

Sasa gestapo makonda bashite amebakia kama kifaranga yatima ambae kila muda mwenye wanaruka ruka juu yake Ili wamfanye kitoweo
Huenda Making akapewa wilaya moja huko mkoani na hawa kina Sabaya wakaishia kubadilishiwa wilaya tu.
 
Kwahiyo kuzunguka zunguka kote huko kwenye uzi kumbe lengo ilikuwa nikumpigia tu upatu Godwin gondwe?

Haya tumekusikia mdogo wake Godwin.
Hata kunijua hanijui kabisaaa. Kama mwananchi namuona he deserves na kwenye kutatua keep anaskiliza pande zote bila kupendelea.

Mi nimuhanga pia kuna kesi yetu ilikua safari ya mahakamani,basi akaisolve kirahisi Sana Kila mtu akaridhika.

Na si hyo tu zipo nyingi sana.
 
Msimchanganye Samia wa watu maacheni ateue kwa utulivu
Freedom to speech, hatujamshinikiza ni maoni yetu,Mambo ya one man show so ndo hamtakagi mnataka ashaurike? Au nyi mmekua vinyonga hamna rangi halisi.
 
Huenda Making akapewa wilaya moja huko mkoani na hawa kina Sabaya wakaishia kubadilishiwa wilaya tu.
Thubutuuuu,labda ajiunge bongo movies Kama jambazi kuu. Na Kisha apeleke kazi zake Filamu zetu irushwe na Azam
 
Freedom to speach,hatujamshinikiza Ni maoni yetu,Mambo ya one man show so ndo hamtakagi mnataka ashaurike?au nyi mmekua vinyonga hamna rangi halisi.
Ndio hayohayo yamefanya utenguzi wa mkurugenzi wa TPDC sijui kwa kuwalazimisha watu wateuliwe wakati hawajawa tayari na qualified
 
Mmeanza kupiga debe! It is Too early. Muiache mamlaka ya uteuzi itekeleze majukumu yake kikatiba, miluzi Hii kutoka kila upande ikizingatiwa mbwa atapotea mapema sana.
Freedom to speech,mbona mnapenda hii kauli kuisema lakini hamuiishi?
 
Godwin Gondwe ni DC wa hovyo kuwahi kutokea. Hafai kabisa tuulize sisi wana Temeke.

Amekariri kuwa kiongozi ni kufokafoka tu bila kutumia akili.
 
Ndio hayohayo yamefanya utenguzi wa mkurugenzi wa TPDC sijui kwa kuwalazimisha watu wateuliwe wakati hawajawa tayari na qualified
Kama amequalified vigezo it's ok, acheni mawazo finyu, China Korea n.k Kuna maCEO vijana wengi wanaendesha Taasisi kubwa kwa uwezo na si kupitapita maofisi mbalimbali ndo CV, hebu acheni akili mbovu za mrundikano wa miCV ya kucopy na kupaste tu.
 
Namuomba Mama anikumbuke na mimi anipe ukuu wa wilaya. Naahidi sitawaangusha Watanzania. sio kila siku majina ni yale yale tu.
 
Back
Top Bottom