Pd Karugendo: Kwanini waliitaka sauti yangu?

Pd Karugendo: Kwanini waliitaka sauti yangu?

Hivi jamani naomba mnisaidie, haya maneno kama shenzi, pumbavu, mjinga, baradhuri na mengineyo mfano wa hayo hua hayana mahala stahili pa kutumika?

Kama hakuna kwa nini bado yanaitwa eti maneno sanifu na bado yamo kwenye kamusi?

Kama papo mahala sahihi mbona yakitumika watu wanakuja juu sana?

Mtazamo wangu
Tufute maneno yote ambayo wataalam wanadai hutakiwi kuyatamka eti kisa ni makali na badala yake tuunde tamathali za semi nyingi ili kuepusha vigugumizi.
 
Padri Privatus Karugendo

KWA siku tofauti ndani ya juma hili nimepata simu za wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine Mwanza wanaojifunza uandishi wa habari, wakiuliza swali lilelile kuhusu rushwa kwenye vyombo vya habari.

Walitaka kujua kama kuna rushwa kwenye vyombo vya habari vya Tanzania, na walitaka mifano na maelezo ya ziada.Sikushindwa kujibu maswali yao, bali niliwaomba wanitumie kwa njia ya barua pepe, ili niyajibu.Hawakutaka pendekezo la barua pepe! Walitaka sauti yangu!

Ni wazi nina mengi ya kuelezea juu ya rushwa kwenye vyombo vya habari, lakini nilisita na sikuweza kuwapatia wanafunzi hao jibu. Walisikitika, walinibembeleza na kuniomba niwasaidie.Najua kabisa inaweza kuwa ni sehemu ya mitihani yao au kazi za mazoezi wanazopewa na maprofesa wao.

Nilikataa, si kwa vile nina roho mbaya na siwatakii mema wanafunzi hao ila baada ya tukio la Wilfred Lwakatare, la watu wenye nia mbaya kutengeneza video bandia hadi mtu kuitwa gaidi na kuwekwa gerezani na kufikishwa mahakamani, na matukio mengine mengi ambayo yameondoa kuaminiana katika taifa letu, ni vigumu kumwamini mtu anayepiga simu na kujitambulisha kwamba yeye ni mwanafunzi wa chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine na angetaka mawazo yako juu ya mambo kadhaa.

Sote tunajua uongo wa simu za kiganjani; mtu anasema yuko Mwanza, wakati yuko Dar es Salaam. Mtu anajitambulisha kuwa yeye ni Juma wakati yeye ni Paulo na mengine mengi.

Kwenye simu anajitambulisha ni mwanafunzi, lakini huku ni mtu mwenye nia mbaya ambaye anataka kutengeneza video juu ya Karugendo. Kesho utasikia Karugendo amesema hivi na hivi juu ya serikali au viongozi wa serikali. Kwa sauti, na kuunganisha picha, kujitetea inakuwa vigumu, kama ilivyotokea kwa Lwakatare, hadi leo hii anasota gerezani.

Kwa kuandika, mtu unaweza kusimama kidete na kufa na maandishi yako, maana Walatini wanasema "kilichoandikwa kimeandikwa".

Binafsi nilikuwa tayari kuyajibu maswali ya vijana hawa wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine kwa maandishi kwa njia ya barua pepe. Wao hawakutaka hilo, bali waliitaka sauti yangu! Kwanini walitaka sauti? Nilijiuliza maswali mengi. Kila aliyepiga simu, aliitaka sauti yangu na wala hakukubaliana na pendekezo la kuandika barua pepe. Watanzania wamezoea ‘cut and paste'.

Kwa mtazamo wangu majibu ya barua pepe yangewasaidia zaidi ya sauti. Tuliona kwenye video ya Lwakatare jinsi sauti na picha vilivyounganishwa. Kila mtu makini anaona wazi kwamba video hiyo imetengenezwa, kwani sauti na picha wakati mwingine haviendani. Lakini serikali haioni hilo, inaona video ni halisi.

Hivyo kama serikali haiwezi kutofautisha video ya kutengenezwa na video halisi, ni lazima tuwe makini tunaongea na nani kwenye simu, maana simu ni mojawapo ya chombo cha kuweza kuchota sauti ya mtu na kuitumia unavyotaka.

Ndiyo maana nimeandika makala hii ili niwaombe msamaha wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine. Kama kweli ni wao, na walikuwa na nia njema, basi wanisamehe.

Tunaelekea kujenga utamaduni wa kishenzi katika taifa letu. Utamaduni wa kutoaminiana, utamaduni wa kuwateka watu, kuwapiga na kuwaumiza, utamaduni wa kusingiziana vitu visivyo vya kweli:
"Ushenzi huu tuliusikia kwenye nchi nyingine za jirani na hasa zinazotawaliwa kidikteta. Sasa umeingia kwetu! Inasikitisha, lakini ndiyo ukweli ulio mbele ya macho yetu.

Jambo la kusikitisha ni kwamba vijana wetu wameukumbatia ushenzi huu kwa nguvu zao zote. Vijana wako tayari kuuza utu wao na uhuru wao ili kuutumikia.

Kitu kibaya kuliko vyote kwa maisha ya mwanadamu ni kupoteza uhuru wake, uhuru wa kuchagua jema na baya, wa kuamua kukubali au kukataa na wa kusimamia mawazo yako. Kupoteza uhuru ni sawa na kupoteza uhai.

Tumesikia kwenye vyombo vya habari vijana wakizua uongo kwamba Dk. Slaa alikuwa na mpango wa kumdhuru Zitto Kabwe kwa sumu.

Dk. Slaa ni kati ya watu wachache wa taifa hili wanaoongozwa na fikra. Huwezi kuongozwa na fikra ukawa na mawazo ya kutoa roho ya binadamu mwenzako. Mtu anayeongozwa na fikra, anapambana kwa hoja na wala si kwa silaha na sumu.

Sote tunamfahamu Dk. Slaa kwa kupambana kwa hoja, na wala huyu si mtu wa kutoa roho za watu. Hivyo vijana wanaolipwa kueneza uongo huu wajue watapoteza yote, wanapoteza uhuru wao na uongo wao hauwezi kushinda maana daima ukweli una nguvu zaidi ya kifo.

Tuliamua kuingia kwenye siasa za vyama vingi ili vishindane kwa hoja na kutangaza sera na itikadi. Wananchi wavutiwe na hoja, wavutiwe na sera na kuvichagua. Lakini utamaduni huu uliozuka wa kuwazushia watu ugaidi na mambo mengine ya kuzua ni ushenzi na ni dalili za woga na kutojiamini.

Katika harakati za kulijenga taifa, hakuna anayetamani kusikia maisha ya mtu binafsi juu ya analala wapi, analala na nani, anakula nini, anavaa nini, anasali wapi, ana sura gani, ni kabila gani. Tunachotaka kusikia ni mchango wa mtu huyu katika kulijenga taifa letu.

Hata kama mtu huyu ni malaya, lakini anatumia umalaya wake kulijenga taifa letu na kulinda usalama na rasilimali za taifa letu. Mtu huyu ni muhimu kuliko wale wanaojiita ni watakatifu.

Matokeo ya utamaduni huu wa kishenzi ni taifa letu kuingia kwenye ushenzi kamili wa kuchinjana na kumwaga damu.

Tumeanza kuulizana juu ya kuchinja. Wakristo wanataka kuchinja, Waislamu wanataka kuchinja! Na hili litaendelea hadi kwenye kilimo. Kama Muislamu hawezi kula nyama iliyochinjwa na Mkristo, na Mkristo hawezi kula nyama iliyochinjwa na Muislamu, ni mantiki pia kwamba Mkristo hawezi kula chakula alichokilima Muislamu, na Muislamu hatakula chakula alichokilima Mkristo. Na itakwenda hivyo kwa kila jambo ndani ya jamii yetu, hadi kuvurugana na kuipoteza amani yetu ya miaka nenda rudi.

Sote tunajua kwamba fedha nyingi zinatumika ili kuwarubuni vijana kuukumbatia utamaduni huu mpya wa kishenzi. Ni bahati mbaya kwamba vijana wetu wanashindwa kujifunza kutokana na matukio ya mataifa mengine; kujifunza kwamba ushenzi huu mwisho wake si mzuri.

Na kutambua ukweli kwamba ushenzi huu haujafanikiwa popote duniani. Watapata fedha za muda; watazitumia; zitakwisha. Matatizo yatakuwa yako pale pale na Tanzania yetu itakuwa pale pale.

Mwalimu Nyerere alitufundisha kwamba fedha si msingi wa maendeleo; ukombozi wa fikra unaweza kutuelekeza kwenye maendeleo, lakini si fedha.

Hivyo katika hali kama hii, nisingeweza kujibu maswali ya vijana wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine kwa simu. Wakitaka nitawajibu kwa barua pepe.

Kupanga ni kuchangua, tumechagua kujenga taifa la kutoaminiana na kutiliana shaka kwa kila jambo. Kama hii ni hatua ya maendeleo, historia ndiyo mwamuzi.

Source: Makala Tanzania Daima

Ndiyo Karugedo ni vizuri kumtetea jirani yetu wa Ibwera Bukoba.Wasilete zao bana hawa C.M
 
Tety mapadri wanatufundusha kusameana kwa hilo bado msimamo wangu huko pale pale kwa nafasi aliyonayo padri na lugha aliyotumia ni kali mno. Kwa suala la vijana kweli inakatisha tamaa. Sijui nafasi yako tety kwa jamii kwa upande wangu kuwaita wapumbavu bado haitoshi maana ni zaidi ya hapo. Lakini sio kwa padri kuita watu hivyo
hata yesu ilipobidi aliwafundisha watu kwa kuwaita enyi kizazi cha uzinzi mbona mna mioyo migumu?? sioni kosa la padri kuwaita wapumbavu jina hilo
 
Upumbavu na ujinga hauishii kwa hao vijana tuu,unakwenda mbali zaidi. Hebu fikirieni kiongozi wa hadhi ya kitaifa katika chama tena chama kinachotawala ana andamana na vijana wa aina hiyo katika ziara zake mikoani kwa gharama za chama ili tuu hao vijana wamsaidie kueneza uzandiki na upuuzi kwa jamii iliyojichokea kwa matatizo, na inahitaji zaidi kusikia mbinu za kuondokana na umasikini wao zaidi ya propaganda za kipuuzi zisizo tija.
Kiongozi/ viongozi wa aina hiyo huu ujumbe wa Karugendo unawahusa kwa kiasi kikubwa zaidi.
 
Ila? We unadhani kwanini hajapeleka sauti huko kwa wanafunzi wa Uandishi feki?Nadhani hajaruhusu kupeleka sauti kwa sababu ya kutokua na uhakika na hao vijana kutoka st.augustine!
 
Punguza jaziba padri hata kama hukutaja majina lakini sio vizuri kusema vijana wapumbavu tafadhari tumia lugha mbadala kufikisha ujumbe.

unatatizo gani wewe?padri katoa hoja wewe unashambulia mtu?kwani mpumbavu ni tusi?hata kama kakulenga usingeonesha kukerwa kako kwa kumshambulia mtu na ndiyo mana ametumia hilo neno..sasa ebu sema ukweli kama wewe si mpumbavu?ni mpumbavu tu..coz umeacha ukweli unakimbilia upumbavu huku ukiujua uhalisia..ni mpumbavu tu wewe.
 
Vijana hawa wameamua kuwasaliti na kuwauza wazazi wao,kaka,dada na binamu zao ..hakika Mungu anajua cha kuwalipa.
 
Natumaini kuwa Pasco naye ataisoma makala hii. Yeye alitaka kutuaminisha, kwa kusisitiza kila anapopata nafasi, kuwa ile tape ya Lwakatare ni "authentic," kama anavyosema mwenyewe
.
Mkuu Jasusi, nimeisoma makala na kuielewa!, japo siijua profesional rasmi ya Padri Privatus Karugendo, ila ni mimi ndie niliyeisimami makala fulani kwenye Gazeti la Mtanzania, kutoka kwa Askofu aliyemfuta sacrament ya upadirisho huyu Padri Karugendo kutoka na kwenda kinyume cha mafundisho ya Ukatoliki kwa maneno na matendo, ndio maana mmemshuhudia anavyitushuhudia humu kuwa watu fulani, hawawezi kupanga kufanya jambo fulani!.

Nasema salini na kuomba watu wasiconfess, vinginevyo watu kama kina Karugendo, watatafuta pa kutokea!.
Kuna watu wanaabudu watu, na nikasema hata shetani mwanzo alikuwa malaika!, na kuna watu mpaka kesho, wanamtumikia shetani disguised as God, wakijua wanamtumikia Mungu!, kumbe wanamtumikia Shetani, bila wao kujijua!. Kuna watu hawana moral authority kuzungumzia baadhi ya issues za morality za wenzao!.

With 15 years kwenye AV Production, naweza kabisa kutumika kama "amicus curiae" kwenye determination ya authenticity ya ile video kuwa "bonafide genuine!". Ila genuinity yake sio determinant ya "admissibility as evidence" before the court of law!.

Ila pia la rushwa kwenye media, nimeisha lizungumza sana hapa!-Waandishi wa Habari na Bahasha: Sio Kila Bahasha ni Rushwa ...

Pasco.
 
hata siku hizi Yuda iskarioti bado wako wanatanga tanga duniani kwa gharama ya 50,000 tshs wanakuuza jumla jumla
 
I can see the correlation kati yake na Dr. Slaa. WANAWAKE NA MATATIZO YA NDOA. Haishangazi kuona anamtetea sana.

Halafu huyu jamaa katika mada zake nyingi, yeye sana sana hugusia wanawake au ngono. Ninafikiri ana kaugonjwa fulani. Siyo ajabu hata Upadri ulinyea njia kwa sababu ya mada za ngono.

Hawa ndiyo dizaini ya tunaosikia wanawambia waumini wao kuwa, kutokuwa na mahusiano na Israel ni laana kwa Tanzania.

Hata ICC kuna Mapadre wanaokabiliwa na mashitaka. Kanisa pia lina mapadre walioacha njia na kufanya vitendo vya kishetani (Kulawiti).

Point yangu ni kwamba, siyo kila wanaoitwa Mapadre ni Mapadre katika macho ya Mungu. Shetani anakuja na sura nyingi.

I'm sorry kwa watu waliokuwa wanakwenda kutubu mbele yake. Moja ya article zake kipande chake hiki hapa chini,
Mimi ni Padri wa Kanisa Katoliki. Sisi wakatoliki tuna kitu kinachoitwa Sakramenti ya kitubio. Waumini wanatubu dhambi zao kwa Padri. Sina lengo na kutaja dhambi za watu. Ninautumia huu kama mfano wa kutusaidia. Kwa kipindi cha miaka 18, niliyoungamisha, sikukutana na familia hata moja yenye Uaminifu katika ndoa. Sikukutana na mtu hata mmoja, mwenye uaminifu katika mapenzi:


Kwa maana kwamba kila mtu mwenye ndoa niliyemuungamisha, alitaja dhambi ya kuzini na kutembea nje ya ndoa!


Kwa maana kwamba kila mtu mwenye mpenzi niliyemuungamisha, alitaja dhambi ya kukosa uaminifu kwa mpenzi wake.


Nimeishi Ulaya, nimeungamisha, hali ilikuwa hivyo hivyo. Nimeishi Mbeya, nimeugamisha, hali ilikuwa hivyo hivyo. Nimeishi Karagwe, nimeungamisha, hali ilikuwa hivyo hivyo. Ninataja sehemu mbali mbali ili isije ikachukuliwa kwamba tabia ya kutokuwa na uaminifu katika ndoa na mapenzi ni ya sehemu Fulani.


Nimekaa kwenye parokia moja ya Bushagaro Karagwe, kwa kipindi cha zaidi ya miaka kumi. Kipindi chote hicho nimeshuhudia watu wakifa kwa UKIMWI. Watu niliowafahamu, niliowaungamisha, watu tuliokuwa tukisali pamoja. Kwa kipindi chote hicho nimeshuhudia watu walio kwenye ndoa na wenye wapenzi wakiungama dhambi ya kuzini. Na kipindi hicho UKIMWI, ulikuwa unapamba moto.
 
unatatizo gani wewe?padri katoa hoja wewe unashambulia mtu?kwani mpumbavu ni tusi?hata kama kakulenga usingeonesha kukerwa kako kwa kumshambulia mtu na ndiyo mana ametumia hilo neno..sasa ebu sema ukweli kama wewe si mpumbavu?ni mpumbavu tu..coz umeacha ukweli unakimbilia upumbavu huku ukiujua uhalisia..ni mpumbavu tu wewe.
Kweli jamiiforums imeingiliwa siku hizi. Wewe ferre au ---- hivi hata kusoma hujui? Mimi nimesema kwa mtazamo wangu na kwa nafasi ya padri katika jamii sijamshambulia mtu. Na najua wewe ukiitwa mpumbavu na mtu lazima utachukia. Hivyo ndio pumbavu ni tusi kama hutaki ni msimamo wako lakini siku nyingine usilushe ngumi ukiitwa hivyo. Na suala la kuguswa mimi kama kijana ni kweli limenigusa maana naamini kusikia matamshi mbadala kutoka kwa mapadri wa kanisa nalo sali kila jumapili sio kuita watu wapumbavu. Wakati tunafundiswa na hao mapadri kuepukana na chuki kwa watu wote.
 
Punguza jaziba padri hata kama hukutaja majina lakini sio vizuri kusema vijana wapumbavu tafadhari tumia lugha mbadala kufikisha ujumbe.
'Vijana wapumbavu'? Hiyo phrase sijaiona kwenye hii makala ya Padri. Nimesoma neno baada ya neno na kurudia mara kadhaa bado sijaliona. Nakaamua kutumia MS word kulitafuta neno wapumbavu kwenye makala hii lakn hata hivo sikulipata. Ninachoweza kusema hilo neno umelizua mwenyewe, nakujitukana au kuwatukana mwenyewe hao vijana aliwamaanisha Padri kuwa ni WAPUMBAVU. Nami nakuunga mkono kuwa hao vijana ni wapumbavu.
 
.
With 15 years kwenye AV Production, naweza kabisa kutumika kama "amicus curiae" kwenye determination ya authenticity ya ile video kuwa "bonafide genuine!".
Pasco.
AV production, 15 yrs ago, enzi za analogia, mambo digitali siku hizi bana!.
 
Well said, Pd. Karugendo. Taifa limekosa mwelekeo tena kipindi cha miaka 8 sasa. Awamu ya nne imekuwa ya kipuuzi, dhaifu na upeo mdogo sana kifikra, kidira na hata kiuongozi. Awamu hii imetufikisha hapa tulipo! Tanzania ya kichekesho! Tanzania inayowaza nani achinje ng'ombe! Tanzania inayopewa meli ya kisasa ya uvuvi na mahakama baada ya kuitaifisha kutokana na uvuvi haramu lakini inaiacha meli hiyo izame! Taifa lenye naibu waziri wa elimu mwenye elimu tata! Taifa ........... (jaza mwenyewe upuuzi mwingi tunaoushuhudia). Je tutafika?
 
'Vijana wapumbavu'? Hiyo phrase sijaiona kwenye hii makala ya Padri. Nimesoma neno baada ya neno na kurudia mara kadhaa bado sijaliona. Nakaamua kutumia MS word kulitafuta neno wapumbavu kwenye makala hii lakn hata hivo sikulipata. Ninachoweza kusema hilo neno umelizua mwenyewe, nakujitukana au kuwatukana mwenyewe hao vijana aliwamaanisha Padri kuwa ni WAPUMBAVU. Nami nakuunga mkono kuwa hao vijana ni wapumbavu.
Ni kweli mkuu katumia neno ushenzi. Kwangu mimi na wewe tukisema ni washenzi au wapumbavu haitakua na nguvu kama akisema padri. Na ukitaka kujua kakosea angalia hata suala la udini. Ilibidi aimbe samahani na kutaja sababu sio ahanze kuongelea mazao Kalima mkiristo basi waislam wasile. Haikua na haja ya yote hayo. Anyway ushenzi ni tusi sio vizuri kutumiwa na kiongozi wa dini ndo msimamo wangu
 
AV production, 15 yrs ago, enzi za analogia, mambo digitali siku hizi bana!.
Mkuu Isotope, ni kweli, enzi hizo, tulikuwa na Analogue! lakini mimi Pasco wa jf, nimeingia rasmi TV Newsroom, 1995 nikiwa na Digital Camera yangu sony (personal) na ipo mpaka leo as achieve!. Wakati huo TV zetu zote analogue, nilikuwa nikitumia DV yangu na kuhamisha picha kurudi Aanalogue kwa AV cable!.

Inawezekana mimi ndie VJ (Video Journalst) wa kwanza Tanzania, na kutokana na uwezo wa kupiga picha na kuandika habari, nimekula trips kibao, ikiwemo 4 trips kuripoti UN GA from New York!.

Mwaka fulani nilikamatwa Zanzibar na DV Camera yangu ikazuiliwa na polisi pale Mwembe Madema, ikapelekwa TV wakatoe mkanda kuungalia, by that time, natumia Mini DV ya HD ina save kwenye hard Disc, TVZ hawana hili wala lile, nikafuatwa polisi, nikawatolee mkanda wao wameshindwa!, nilipofika nikasema hii camera haitumii mkanda, na sio video bali ni ya still photo. Nika swich upande wa memory card, nikawaonyesha picha za still, wakajiridhisha kuwa sikupiga picha, nikasindikizwa under escort mpaka bandarini na kutimuliwa!, kufika Dar, kwenye news ya Saa 1:00 usiku, DTV ikaibuka na breaking news ya machafuko ya Zanzibar with video footage!. Hata ile seke seke ya Mwembe Chai, aliyei breaki ni mimi na zile picha nilipiga mimi!. Kitendo cha kumaliza JKT nikaunganisha na JWTZ na ndipo nikaingia Nwesroom kilinifanya niwe kama mjeshi fulani!.

DV kwa TV za Tanzania imeletwa na TBC, enzi hizo TVT, na kwa sasa technology imehamia HD, sisi Tanzania bado tuko kwenye DV, ile mimi kupitia Studio yangu ya PPR, siku nyingi nimeisha hamia kwenye HD nikitumia XD Card camera za Sony, ila bado nalazimika ku export kwa DV kwa sababu mitambo ya TBC ikiplay HD, picha inaonekana kama ina over exposure!.

Ile video ni "bonafide genuine!" kama kuna mengine na tuyasubirie!.

Pasco.
 
Tety mapadri wanatufundusha kusameana kwa hilo bado msimamo wangu huko pale pale kwa nafasi aliyonayo padri na lugha aliyotumia ni kali mno. Kwa suala la vijana kweli inakatisha tamaa. Sijui nafasi yako tety kwa jamii kwa upande wangu kuwaita wapumbavu bado haitoshi maana ni zaidi ya hapo. Lakini sio kwa padri kuita watu hivyo

Kama "pumbavu" ni tusi basi ni tusi kwa mtu yeyote yule atakayetamka, iwe padri au teja, ukisema eti Padri kwa nafasi yake "hakupaswa" utakuwa unakosea, YESU mwenyewe alimuita Herode "mbweha" baada ya kuzidisha upumbavu ndo sembuse Padri,Kuwa kiongozi unapaswa kusema ukweli ikiwapo kuwaita wapumbavu WAPUMBAVU na sio kumridhisha kila mtu kwa maneno matamu
 
Back
Top Bottom