Martin George
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 1,695
- 1,470
RC wa Dar es Salaam Mh. Makonda amempongeza Meya wa jiji lake mstahiki Isaya Mwita kwa namna anavyosimamia miradi ya maendeleo jijini tofauti na viongozi wengine wa CHADEMA ambao kazi yao ni kuwasakizia watoto wa wenzao waingie barabarani wakavunjwe miguu.
Meya Mwita amekuwa mstari wa mbele katika kushirikiana na viongozi wa serikali bila kujali itikadi ya vyama. Makonda ameyasema hayo katika sherehe ya wiki ya maji katika ukumbi wa JNICC.
========
Dar es Salaam. Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda amesifia utendaji kazi wa meya wa jiji Isaya Mwita kwa kile alichodai hayumbishwi na misimamo ya vyama.
Akizungumza leo Machi 16, Makonda alisema Mwita ambaye ni diwani wa CHADEMA hana tabia kama za wenzake na muda mwingi anafikiria maendeleo.
Akiwa katika uzinduzi wa wiki ya maji baada ya Mwita kumkaribisha kuzungumza, Makonda alianza kwa kumtania,
"Meya nilijua utazungumzia maandamano ila niseme wazi namkubali sana Isaya, ni miongoni mwa watu ambao unaweza kukaa nao mkazungumzia maendeleo."
"Hii ndiyo aina ya maandamano inayotakiwa. Tunataka kuandamana kwa kujadili na kutafuta ufumbuzi wa changamoto kwa wananchi tunaowaongoza.
"Wangekuwa wale wengine wangejiweka huko lakini huyu anapenda maendeleo.
"Wengine wanasubiri wawaingize watoto wa watu barabarani waandamane wavunjwe miguu halafu wawatafute watu wa Ulaya wawape hela," amesema Makonda.
Chanzo: Mwananchi
Meya Mwita amekuwa mstari wa mbele katika kushirikiana na viongozi wa serikali bila kujali itikadi ya vyama. Makonda ameyasema hayo katika sherehe ya wiki ya maji katika ukumbi wa JNICC.
========
Dar es Salaam. Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda amesifia utendaji kazi wa meya wa jiji Isaya Mwita kwa kile alichodai hayumbishwi na misimamo ya vyama.
Akizungumza leo Machi 16, Makonda alisema Mwita ambaye ni diwani wa CHADEMA hana tabia kama za wenzake na muda mwingi anafikiria maendeleo.
Akiwa katika uzinduzi wa wiki ya maji baada ya Mwita kumkaribisha kuzungumza, Makonda alianza kwa kumtania,
"Meya nilijua utazungumzia maandamano ila niseme wazi namkubali sana Isaya, ni miongoni mwa watu ambao unaweza kukaa nao mkazungumzia maendeleo."
"Hii ndiyo aina ya maandamano inayotakiwa. Tunataka kuandamana kwa kujadili na kutafuta ufumbuzi wa changamoto kwa wananchi tunaowaongoza.
"Wangekuwa wale wengine wangejiweka huko lakini huyu anapenda maendeleo.
"Wengine wanasubiri wawaingize watoto wa watu barabarani waandamane wavunjwe miguu halafu wawatafute watu wa Ulaya wawape hela," amesema Makonda.
Chanzo: Mwananchi