Patrobas alitaka fursa gani CHADEMA?

Patrobas alitaka fursa gani CHADEMA?

kindikwili

JF-Expert Member
Joined
Oct 5, 2016
Posts
1,862
Reaction score
2,876
Kwanza niseme wazi kabisa kwamba nakubaliana na meneno ya wahenga kwamba mwenzako akinyolewa zako tia maji. Juzi hapa CHADEMA walimvuna ndg Nyalandu kutoka CCM na leo CCM wamemvuna Patrobas , hiyo ndiyo siasa na kila siku mwenyekiti wa CHADEMA anasisitiza kwamba kwenye siasa hakuna rafiki wala adui wa kudumu. Kwahiyo waliiondoka ama ccm , cdm au ACT wametimiza usemi huo.

Ila nimemsikia ndg Patrobas Katambi akisema CCM inatoa fursa kwa vijana tofauti na huko upinzani na kwamba juzi aliona aliyekuwa mwenyekiti wake akiwa chuo amepewa mjumbe wa kamati Tanzanite. Kwa sentensi ile kaonesha wazi kwamba fursa anayoizungunza ni cheo au ulaji ambayo hata hivyo chadema hawawezi kuitoa kwasababu hawana serikali. Hivi kuna fursa zaidi ya kuwa mwenyekiti wa BAVICHA TAIFA? AU MIMI NDIYO SIJUI MAANA YA FURSA KISIASA?. Kwa nafasi aliyokuwa nayo katambi ndani ya CHADEMA mimi naona chama kilimpa fursa tena fursa ya kuonesha uwezo wake , kipaji chake na huenda kwa hiyo nafasi yake angefika mbali. Ndg John Heche alianzia huko na leo ni mbunge au yeye alitaka fursa gani, kuwa mwenyekiti au?

Nimalizie kwa kusema haya, katiba imetoa nafasi na uhuru wa watu kuhama vyama wapendavyo kwahiyo hawa wametekeleza haki yao ya kikatiba wala watu wasitumie muda mwingi kuwalaumu. Ila nalaani sana siasa za fursa, siasa za vyeo, siasa zinazofanya vijana kudhalilisha utu wao ili tu wapate vyeo. Lazima vijana tufanye kazi zingine kujipatia maisha tusitegemee siasa. Tutakuwa wakosoaji wazuri sana, wateteaji wazuri sana kama tuna kazi zetu za kufanya. fanya siasa bila mategemeo ya zawadi na fursa za kupewa bali tutafute fursa wenyewe kwa kuthubutu kugombea nafasi na tuwe wavumilivu ndani ya vyama vyetu. Unaweza kuhamia chadema leo kumbe 2020 ungegombea kwa ccm ungeshinda au unahamia ccm leo kumbe 2020 ilikuwa bahati yako kwa CHADEMA.
Niwatakie watafuta fursa (vyeo ) kazi njema ila at least waje na sababu strong basi.

Kindikwili -Ndanda
 
Kila anayetoka anasema lake, Nyalandu alisema yake na Patrobas kasema yake....
We elewa tu kila mtokaji ana lale la kusema.
Sio lazima liwe la kweli.
 
Patrobas kaongelea ukweli wa muda mrefu...hata ben saanane mmemtumia kama karai
 
Kwanza niseme wazi kabisa kwamba nakubaliana na meneno ya wahenga kwamba mwenzako akinyolewa zako tia maji. Juzi hapa CHADEMA walimvuna ndg Nyalandu kutoka CCM na leo CCM wamemvuna Patrobas , hiyo ndiyo siasa na kila siku mwenyekiti wa CHADEMA anasisitiza kwamba kwenye siasa hakuna rafiki wala adui wa kudumu. Kwahiyo waliiondoka ama ccm , cdm au ACT wametimiza usemi huo.

Ila nimemsikia ndg Patrobas Katambi akisema CCM inatoa fursa kwa vijana tofauti na huko upinzani na kwamba juzi aliona aliyekuwa mwenyekiti wake akiwa chuo amepewa mjumbe wa kamati Tanzanite. Kwa sentensi ile kaonesha wazi kwamba fursa anayoizungunza ni cheo au ulaji ambayo hata hivyo chadema hawawezi kuitoa kwasababu hawana serikali. Hivi kuna fursa zaidi ya kuwa mwenyekiti wa BAVICHA TAIFA? AU MIMI NDIYO SIJUI MAANA YA FURSA KISIASA?. Kwa nafasi aliyokuwa nayo katambi ndani ya CHADEMA mimi naona chama kilimpa fursa tena fursa ya kuonesha uwezo wake , kipaji chake na huenda kwa hiyo nafasi yake angefika mbali. Ndg John Heche alianzia huko na leo ni mbunge au yeye alitaka fursa gani, kuwa mwenyekiti au?

Nimalizie kwa kusema haya, katiba imetoa nafasi na uhuru wa watu kuhama vyama wapendavyo kwahiyo hawa wametekeleza haki yao ya kikatiba wala watu wasitumie muda mwingi kuwalaumu. Ila nalaani sana siasa za fursa, siasa za vyeo, siasa zinazofanya vijana kudhalilisha utu wao ili tu wapate vyeo. Lazima vijana tufanye kazi zingine kujipatia maisha tusitegemee siasa. Tutakuwa wakosoaji wazuri sana, wateteaji wazuri sana kama tuna kazi zetu za kufanya. fanya siasa bila mategemeo ya zawadi na fursa za kupewa bali tutafute fursa wenyewe kwa kuthubutu kugombea nafasi na tuwe wavumilivu ndani ya vyama vyetu. Unaweza kuhamia chadema leo kumbe 2020 ungegombea kwa ccm ungeshinda au unahamia ccm leo kumbe 2020 ilikuwa bahati yako kwa CHADEMA.
Niwatakie watafuta fursa (vyeo ) kazi njema ila at least waje na sababu strong basi.

Kindikwili -Ndanda
Hata Lowassa kilichomleta chadema ni fursa tu!
 
Patrobas kaongelea ukweli wa muda mrefu...hata ben saanane mmemtumia kama karai

Ndg Jinga lao unadhani CDM wangeweza kumfanyia nini Patrobas zaidi ya hiyo nafasi aliyokuwa nayo? Hivi nafasi za uongozi ziko ngapi nadni ya chama au ni kwamba kila anayekuwa mwanachama , mpiganaji apewe fursa ? Lakini fursa ni nini kama mwenyekiti wa BAVICHA au UVCCM atasema hajapewa fursa na chama? naomba unijibu hapa mkuu
 
Dah, huyu jamaa kweli imewauma!
Na kibaya zaidi ndo kwanza yuko kwenye DAWN na sio TWILIGHT kama wale waliokuja ufipa. Imewauma sana chadema hii.
 
Aende tu, wapo vijana wengi na makini sana kuliko yeye kwanza alishaonekana hana tija ndio maana kaondoka. hata iwe kimetolewa 'kitu kdg' kama cha kule Ar poa tu. ILA aelewe kuwa ccm watamtumia kama condom baadae hawatakuwa na issue nae tena.
 
Labda alitaka appreciation na kuwa acknowledged
 
Kwanza niseme wazi kabisa kwamba nakubaliana na meneno ya wahenga kwamba mwenzako akinyolewa zako tia maji. Juzi hapa CHADEMA walimvuna ndg Nyalandu kutoka CCM na leo CCM wamemvuna Patrobas , hiyo ndiyo siasa na kila siku mwenyekiti wa CHADEMA anasisitiza kwamba kwenye siasa hakuna rafiki wala adui wa kudumu. Kwahiyo waliiondoka ama ccm , cdm au ACT wametimiza usemi huo.

Ila nimemsikia ndg Patrobas Katambi akisema CCM inatoa fursa kwa vijana tofauti na huko upinzani na kwamba juzi aliona aliyekuwa mwenyekiti wake akiwa chuo amepewa mjumbe wa kamati Tanzanite. Kwa sentensi ile kaonesha wazi kwamba fursa anayoizungunza ni cheo au ulaji ambayo hata hivyo chadema hawawezi kuitoa kwasababu hawana serikali. Hivi kuna fursa zaidi ya kuwa mwenyekiti wa BAVICHA TAIFA? AU MIMI NDIYO SIJUI MAANA YA FURSA KISIASA?. Kwa nafasi aliyokuwa nayo katambi ndani ya CHADEMA mimi naona chama kilimpa fursa tena fursa ya kuonesha uwezo wake , kipaji chake na huenda kwa hiyo nafasi yake angefika mbali. Ndg John Heche alianzia huko na leo ni mbunge au yeye alitaka fursa gani, kuwa mwenyekiti au?

Nimalizie kwa kusema haya, katiba imetoa nafasi na uhuru wa watu kuhama vyama wapendavyo kwahiyo hawa wametekeleza haki yao ya kikatiba wala watu wasitumie muda mwingi kuwalaumu. Ila nalaani sana siasa za fursa, siasa za vyeo, siasa zinazofanya vijana kudhalilisha utu wao ili tu wapate vyeo. Lazima vijana tufanye kazi zingine kujipatia maisha tusitegemee siasa. Tutakuwa wakosoaji wazuri sana, wateteaji wazuri sana kama tuna kazi zetu za kufanya. fanya siasa bila mategemeo ya zawadi na fursa za kupewa bali tutafute fursa wenyewe kwa kuthubutu kugombea nafasi na tuwe wavumilivu ndani ya vyama vyetu. Unaweza kuhamia chadema leo kumbe 2020 ungegombea kwa ccm ungeshinda au unahamia ccm leo kumbe 2020 ilikuwa bahati yako kwa CHADEMA.
Niwatakie watafuta fursa (vyeo ) kazi njema ila at least waje na sababu strong basi.

Kindikwili -Ndanda
Patrobas katambi ameama kwani....! Ebu lete CD na FLASH tuone kama ameama kweli
 
Wasalam , wana jamvi nakumbuka wakati tunatoa maneno yetu wakati wa uchaguzi wa mwaka 2015 nilionya na kuwaambia vyama pinzani haswa Chadema kwa kumpokea MHE Lowassa ndani ya chama chao ndio mwanzo wa kufa upinzani hilo linaenda kutimia hata kabla ya kuingia duru la pili la uchaguzi ndani ya nchi hii ya Tanzania mwaka 2020, kwa kuona wimbi la watu maarufu na vijana wenye elimu wakiondoka kurudi chama tawala cha Ccm, Patrobas Katambi ni kijana ambae amenistua sana leo achilia mbali Masha, Kitila Mkumbo, Albert Msando pamoja na Mwigamba.

Ukimchukua Patrobas unaweza kumlinganisha na kijana Humphrey polepole ambae amekuzwa katika misingi imara ya chama na kukomaa hadi kufika mahali alipo, kwa maaana nyingine chama cha mapinduzi kiliitambua hazina iliyomo ndani ya polepole na kuilea na kumfikisha mapaka alipo, maana yake hawakuupuza uwezo alionao polepole, nitaeleleza kwa kifupi kwanini nimeguswa na kuhama kwa huyu kijana haswa kwa kuzichambua kauli zake mwenyewe kwa kuzinukuuu alipokuwa anajieleza katika mkutano wa chama cha mapinduzi.

"Wapinzani wengi wanahubiri mabadiliko ila kiuhalisia wao wanaishi maisha ya kishetani wakati raia wanaumia" mwisho wa kunukuuu, nimepata wakati mgumu kuifanyia kazi kauli, je wapinzani ni wap? na Raia ni wapi? na maisha ya kishetani ni yapi? wakati Mhe Rais John Magufuli anapewa nguvu na mamlaka ya kupeperusha bendera ya chama wakatia wa kampeni za Urais alisema waziwazi bila ya kupepesa macho kuwa atapambana na rushwa na mafisadi haijalishi walikuwa wapi na katika chama kipi, na kweli Mhe Rais ametekeleza maneno yake kwa matendo bila ya kusitasita na wengine kuwakemea hadharani bila ya aibu ndani ya chama chake hata nje ya chama chake, Kama ni kweli Bwana Patrobas umeguswa na nguvu chanya ambayo Mhe Rais ameionesha karibu sana kwa mapambano sababu haya mapambano si ya mda mfupi kama wengi wadhaniavyo, uliposema raia wanaumia je uliimaanisha wanachama wanyonge waliopo chadema au ulimaaanisha raia wote ndani ya nchi hiii? jibu unalo wewe kama ni ndani ya chama cha chadema hilo ni halisi na huwezi kulificha ni chama ambacho kimebeba ukanda na uabinafsi, bila ya kuwa wa kanda Fulani huwezi kufaidi matunda ya chama ukiwemo mgawanyo wa uongozi na mapato ya chama, ingawa we ulikuwa mwenyekiti wa Bavicha hapo ndio nafika Napata shaka au kuongeza Imani na wewe yawezekana unaishi unayoyahubiri


"Kwa upinzani kijana ni karai katika ujenzi wa ghorofa" hii ni kauli yako nyingine ambayo pia imenigusa mtima wangu, kama ulitumia nguvu zako nyingi kuitumikia chadema na mwenyekiti wako uliyemkimbia Bw. Mbowe , na malipo yake hayalingani na kile ulichokuwa unapigania kila siku, hiyo ni hakika kabisa kwa kijana mwenye akili timamu, yaani hauna matatizo ya akili lazima ujitazame na ujiulize thamani yako iko wapi ? kama kijana, na hii ni kwa vijana wote wa kitanzania, kama upo mahali na unatoa mchango Mkubwa ambao unaleta matokeo chanya mahali ulipo, lakini wenye kuyapata matokeo yale hawauthamini mchango wako, ni budi ujiulize thamani yako pale iko wapi?

"Leo hii upinzani umegubikwa na umimi, ubinafsi na makundi" Siamini kama hili ndio umeliona leo Ndugu yangu Patrobas, utawala wowote kuanzia ngazi ya familia ukikosa utawala wenye misimamo na busara , tatizo hili utokea , vivyo hivyo katika vyama vyote vya siasa haijalishi ni chama tawala au cha upinzani, vivyohivyo katika uongozi wa nchi, mimi binafsi nakushauri kama ulikuwa umeshathiirika na tatizo kama hilo, jitibu haraka na uliache huko ulipotoka kama unaona huwezi kujitibu tafuta matabibu, utajitengenezea heshima na baadae kuja kuwa Kiongozi mzuri, namshukuru sana Mhe rais John Magufuli kwa kuonesha njia vijana sasa wameanza kuuona ukweli unaogusa nafsi zao.


"Kama nitaitwa msaliti basi nasaliti ubinafsi, kwa watu binafsi, kwa maslahi ya taifa"Dah kauli nzito sana hiii kwa kijana kama wewe kuitoa, hakika umegundua ubinfsi uliopo chadema, kuanzia Kiongozi wenu Mkuu na wengineo ndani ya chama , kama ni kweli umeamua kuusaliti ubinafsi, anza kuusaliti ambao upo ndani ya moyo wako, na hili pia nawaambia vijana wote wa Kitanzania ukitaka kufika mbali katika nchi hiii kamwe ubinafsi na umimi usibebe moyo wako, Karibu sana Patrobas ndani ya chama chenye mwelekeo, kaa ukielewa mapambano yanaendelea.

Hongera Rais wangu Magufuli, usivunjike moyo , wameanza kukubali unachokipigania, aluta continua....................................
 
Back
Top Bottom