Patrick Rutabanzibwa: UKWELI ni upi?


Mkuu bibikuku, kimsingi nakubaliana na maelezo yako. Basi tuseme Ulimwengu alijiuzulu nafasi ya ukuu wa Wilaya.

Tiba
 

Nchi mambo yake yanashangaza sana,mfano hiyo richmond lowasa anasema"hakuna hata jambo moja tulilolifanya bila kumpatia rais taarifa,kuanzia hatua ya mwanzo kabisa...."rais naye anasema"mimi binafsi hiyo richmond siijui kabisa wala sina taarifa ya chochote kilichotokea..." baadaye akihutubia wazee wa dsm dimond jubilee rais aliendelea"lowasa hakuwa na kosa lolote bali alijiuluzu kwa sababu za kisiasa..."sasa nani mkweli hapa?
 
Mengi ndiye aliyekuwa OWNER wa gazeti la Mwanahalisi

hivyo alikuwa ni bosi wake Kubenea

Je mengi huyo huyo ndiye owner wa hili gazeti jipya la Kubenea?
 
The Boss wakati mwingine matumizi ya neno Fisadi huwa hayaeleweki. Fisadi kwako kwa mwingine anaweza kuwa ni mchapakazi anayezitolea jasho pesa zake kwa njia ya halali. Hivi una habari nchi hii kila mtu anayepita akiendesha gari hata kama ni la serikali anaitwa na baadhi ya watu kuwa ni fisadi? Na kama mhusika hana ushahidi wa kuthibitisha ufisadi wa mtuhumiwa anaishia kusema ndio walewale tu!! Inawezekana kabisa hata wewe the Boss kuna maeneo wanakuita Fisadi tu.
 

hapo wote wakweli
 
Katili huyu jamaa sana hakika ni mtusi
Unaposema Katili una maana gani ndugu? Fafanua ni ukatili gani aliokufanyia wewe au mtu mwingine unayemjua na ikiwezekana weka ushahidi hapa tuutafakari. Vinginevyo itauwa ni maneno ya vijiweni tu.

Kingine nakushauri kama msomi uache "stereotyping" au "generalization" kwa maana ya kuhukumu jamii nzima kwa kutumia kosa au tabia za mtu mmoja mmoja toka kwenye jamii husika. Hapa unataka kutuaminisha kuwa Mtusi yeyote ni mtu katili bila kutoa ushahidi wowote kuthibitisha hilo. Je akitokea mtu wa nje ya nchi akasema watanzania wote ni punda wa kubeba madawa ya kulevya kwa sababu tu kuna baadhi ya watu wamekamatwa nje atakuwa sahihi?
 
Katika jambo ambalo wanasiasa (wa chama tawala na wapinzani wao) wamefanikiwa sana nchi hii ni kulifanya suala la ufisadi kuwa ni dhana tu ya kisiasa. Hivi sasa haijulikani wanapoongelea ufisadi wanamaanisha nini hasa na mafisadi ndio akina nani kwani kwa sasa hili neno linatumika kama silaha ya mwanasiasa ya kuwashambulia wapinzani wake. Matokeo yake hakuna mtu anayeweza kutiwa hatiani kwa kutumia hii dhana ya kisiasa ya ufisadi. Kwa bahati mbaya zaidi hata waandishi wa habari wametekwa na hilo wimbi la kufanya ufisadi kuwa ni dhana tu ya kisiasa.
 
Hivi kwa mfano nipashe imekosea , shutuma apewe Mengi ?
 

Unajua kukubali kukosolewa nako ni dalili ya uanaume, haya nimekubali kukosolewa ndugu yangu
 
Ukiongea na watu wengi aliofanya nao kazi ama wanaomjua kwa ukaribu watakueleza kuwa Patrick is one of the brilliant technocrats in this country. Additionally, I've been told that he's hard working, fearless, highly ethical and a tough cookie.
Inakuwa ni ngumu kuamini which is which.
 
Unajua kukubali kukosolewa nako ni dalili ya uanaume, haya nimekubali kukosolewa ndugu yangu
Ndugu yangu heshima mbele.

Angalizo lako siyo 'uanaume' au 'uanamke' peke yake bali pia ni mzizi wa falsafa ya kujifunza na katika kufanya hivyo, ndiyo hatua moja mbele kimaendeleo hupatikana.

Hata mimi ukinisoma sehemu ukagundua kuwa nimepungukiwa uelewa fulani, basi nitashukuru sana ukinigusa sikioni na kuniambia mapungufu yangu.

Tuko wote.
 

Du na Obama tena kweli wewe unataka tugeuzwe Libya, bwana tusiwasemeseme wamarekani tuwaache waje kujichimbia zao mafuta na kuvuna gesi
 
Toka huko kwenye makabila ujadili hoja. Wenzio huko tulitoka kitambo. Ukitoka hapo utasema ni dini. Ovyoo!
 
Du na Obama tena kweli wewe unataka tugeuzwe Libya, bwana tusiwasemeseme wamarekani tuwaache waje kujichimbia zao mafuta na kuvuna gesi
Sasa kama hii mitambo ingekuwa ina ufisadi wowote Hillary Clinton wala si Obama asingethubutu kwenda Ubungo na kuipa baraka zake. Hii ni pasua kichwa na sioni jawabu. Richmond-Dowans-now Symbion-Obama
 

Nakubaliana na wewe mkuu...binafsi kuna mambo alinifanyia mazuri sana tena bado nikiwa kijana mwanachuo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…