Mathias Raymond Nyakapala
JF-Expert Member
- Mar 1, 2017
- 2,181
- 1,494
#MWENYEKITI_BAVICHA_TAIFA_ATOA_SHUKRANI
Ndugu Viongozi wa CHADEMA na Wanachama wote wa CHADEMA Salam kwenu.
Ninawasalimu kwa Salamu za Chama.
Siku ya 01.12.2017 Kamati Tendaji ya Baraza La Vijana CHADEMA liliniamini na kunichagua kunipa dhamana kubwa zaidi ya Kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Vijana CHADEMA Tanzania na kuwaongoza vijana wenye fikra za kuleta Mapinduzi ya Kisiasa, Kiuchumi na Kijamii kupitia falsafa, itikadi na Sera za CHADEMA.
Ninapenda kutoa shukrani kubwa kwenu kwa imani hii mliyonipa na kuona kwamba nina uwezo wa kuliongoza Baraza letu la Vijana BAVICHA.
Ninahisi deni kubwa kwenu wanachama na chama changu na ninaahidi kuwatumikia kwa uaminifu mkubwa na kwa pamoja tukishirikiana tutaliinua Baraza letu katika Viwango vingine. Ninahitaji ushirikiano na utayari wenu.
Ninatambua hali ya kisiasa ya serikali ya awamu ya tano, ninafahamu ni kwa kiasi gani tumechoshwa na udhalimu wake wa kuongoza serikali bila ya kufuata sheria na taratibu zilizowekwa, kukiukwa kwa misingi ya kidemokrasia, kuvunjwa kwa haki za binadamu kwa kuteswa, kudhalilishwa, kutishiwa na hata kufanywa kwa majaribio ya kutolewa uhai wa viongozi wetu.
Pamoja na yote haya, napenda kuwahakikishia CHADEMA itasimama, na tutakwenda kuidhibiti serikali kikamilifu. Tukawe hodari katika kupigania haki zetu, misingi ya utawala bora na Demokrasia katika taifa letu kusudi tukadhibiti matumizi ya rasilimali zetu na na kuleta uhuru wa kweli wa kiuchumi, kifikra na Maendeleo katika maisha ya Watanzania.
Jana 06/12/2017 Kikao Cha Kamati Kuu ya chama chetu rasmi kiliweza kuniidhinisha kuwa Mjumbe Halali wa Vikao vya Kamati Kuu Tukufu ya chama chetu, Na Naishukuru sana Kamati Kuu kwa imani hiyo kwangu na kwa kukubali pia kuchaguliwa kwangu na Kamati Tendaji ya BAVICHA Taifa, Niliahidi kuwa mwaminifu na uwepo wangu kuwa wafaida kwa chama chetu kwa kipindi chote cha uongozi wangu.
Asanteni Kwa Kuniamini.
PATRICK OLE SOSOPI
MWENYEKITI BAVICHA TAIFA.
#To_Be_Is_To_Do
Ndugu Viongozi wa CHADEMA na Wanachama wote wa CHADEMA Salam kwenu.
Ninawasalimu kwa Salamu za Chama.
Siku ya 01.12.2017 Kamati Tendaji ya Baraza La Vijana CHADEMA liliniamini na kunichagua kunipa dhamana kubwa zaidi ya Kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Vijana CHADEMA Tanzania na kuwaongoza vijana wenye fikra za kuleta Mapinduzi ya Kisiasa, Kiuchumi na Kijamii kupitia falsafa, itikadi na Sera za CHADEMA.
Ninapenda kutoa shukrani kubwa kwenu kwa imani hii mliyonipa na kuona kwamba nina uwezo wa kuliongoza Baraza letu la Vijana BAVICHA.
Ninahisi deni kubwa kwenu wanachama na chama changu na ninaahidi kuwatumikia kwa uaminifu mkubwa na kwa pamoja tukishirikiana tutaliinua Baraza letu katika Viwango vingine. Ninahitaji ushirikiano na utayari wenu.
Ninatambua hali ya kisiasa ya serikali ya awamu ya tano, ninafahamu ni kwa kiasi gani tumechoshwa na udhalimu wake wa kuongoza serikali bila ya kufuata sheria na taratibu zilizowekwa, kukiukwa kwa misingi ya kidemokrasia, kuvunjwa kwa haki za binadamu kwa kuteswa, kudhalilishwa, kutishiwa na hata kufanywa kwa majaribio ya kutolewa uhai wa viongozi wetu.
Pamoja na yote haya, napenda kuwahakikishia CHADEMA itasimama, na tutakwenda kuidhibiti serikali kikamilifu. Tukawe hodari katika kupigania haki zetu, misingi ya utawala bora na Demokrasia katika taifa letu kusudi tukadhibiti matumizi ya rasilimali zetu na na kuleta uhuru wa kweli wa kiuchumi, kifikra na Maendeleo katika maisha ya Watanzania.
Jana 06/12/2017 Kikao Cha Kamati Kuu ya chama chetu rasmi kiliweza kuniidhinisha kuwa Mjumbe Halali wa Vikao vya Kamati Kuu Tukufu ya chama chetu, Na Naishukuru sana Kamati Kuu kwa imani hiyo kwangu na kwa kukubali pia kuchaguliwa kwangu na Kamati Tendaji ya BAVICHA Taifa, Niliahidi kuwa mwaminifu na uwepo wangu kuwa wafaida kwa chama chetu kwa kipindi chote cha uongozi wangu.
Asanteni Kwa Kuniamini.
PATRICK OLE SOSOPI
MWENYEKITI BAVICHA TAIFA.
#To_Be_Is_To_Do