feyzal
JF-Expert Member
- Apr 20, 2016
- 8,519
- 17,177
- Thread starter
- #21
PATASHIKA - 15
Walitembea hadi walipofika barabara kuu.
“Twende tukasimame kwenye kile kichaka, tusubiri basi, tukifanikiwa kupata basi itakuwa vema zaidi. Maana nimeona si salama kuendelea kusafiri kwa lile gari lako. Kutumia gari lako itawapa urahisi wa kutupata haraka.” Alisema yule dereva huku akimuonesha Vivian kichaka alichotaka waende. Yule dereva alikimbia hadi kwenye kile kichaka, kuona hivyo Vivian na yeye alikimbia kizembe huku akiwa anakunywa juisi yake kuelekea pale alipoenda yule dereva. Vivian hakuelewa kwa nini alikuwa akitii kila alichoambiwa na yule dereva, lakini pia, hakuona sababu ya kutotii mradi awe na uhakika wa usalama wake.
“Wakati tukiwa hapa, nitajaribu kukuelezea kwa kifupi kuhusu mimi na wewe. Maana sina hakika nini kitafuata dakika chache kutoka sasa. Nimekaa miaka mingi nikiwa nasubiri muda kama huu ili niweze kufanya hiki nikifanyacho sasa kwa faida yenu na Taifa hili…” Alisema yule dereva huku akiwa anavua sura ya bandia aliyokuwa amevaa. Vivian aliweka chini boksi la juisi aliyokuwa anakunywa.
“Naitwa Mwasumbi, Luteni Mwasumbi.”
“Ooooh my God!, kwa hiyo muda wote ule tulikuwa tukiongea na wewe kule kijijini tukidhani kuwa u Askofu Alphonso kumbe haikuwa kweli! Kwa nini umeamua kufanya hivi?” Vivian alisema kwa mshangao mkubwa. Huku sasa akitazamana na sura ya mtu mwingine tofauti na ile ya Askofu Alphonso. Kabla Mwasumbi hajajibu walisikia mlio wa gari ukija kwa kasi. Vivian alitaka kukimbilia barabarani ili kulisimamisha.
“Stop!, usifanye hivyo Vivian, nimekwambia tutapanda basi, huo mlio wa gari si wa basi ni wa gari ndogo tu tena wanaweza kuwa wenyewe!” Mwasumbi alisema huku akimshika mkono Vivian na kuukandamiza chini, Vivian akaanguka chini kutokana na ule mkandamizo.
“Wewe vipi sasa tusipopata hilo basi tutalala hapa? Si bora tukaomba msaada kwenye magari madogo yanayoelekea Kamanga.” Vivian aling’aka kwa hasira na mshangao. “Sikiliza we mtoto, si muda mrefu utajua uko kwenye kisa gani na kwa nini unatafutwa san…” Kauli ya Mwasumbi ilikatishwa na mlio wa gari lilokuwa likija kwa kasi. Mlio ulionyesha kuwa lilikuwa karibu sana na pale walipokuwa wamejificha na lilikuwa kwenye mwendo wa kasi. Mwasumbi alisogea na kuchungulia barabarani kupitia matawi ya kile kichaka walichokuwepo. Macho yake yaliweza kuliona gari aina ya Land Rover 110 rangi ya kijani likiwa na alama kubwa nyeupe, alama hiyo ilikuwa herufi T ubavuni.
“Oooh yeah!, unaona sasa ndiyo wenyewe, wanatutafuta!” Mwasumbi alisema kwa kunong’ona. Vivian alibaki ametoa macho wala hakuwa anajua kinachoendela.
“Vivian, naomba nikueleze kwa kirefu kuhusu kisa hiki. Mwaka 1967 kulikuwa na harakati kubwa sana hapa nchini. Ilikuwa ni wakati ambao Mwalimu Nyerere alikuwa katika harakati kubwa za kutaka kuonyesha kuwa nchi ilikuwa huru kutoka katika mikono ya wakoloni. Mambo mengi yalifanyika, nuruni na gizani, ya kusemeka na ambayo hatuwezi hata kuyatamka. Mengi yalitokea, machache yaliandikwa na ambayo mnaweza kuyasoma leo. Harakati ziliendelea sana hadi mwaka 1976 ambapo wazungu wengi walikuwa wameshaondoka nchini na Nyerere akaikoleza zaidi ile sera ya Ujamaa na misingi ya Kujitegemea. Kama nilivyosema, kulikuwa na harakati nyingi sana ila ukweli ulikuwa wazi sana kuwa, wazungu waliokuwa hapa nchini walikuwa wakiijua nchi yetu kuliko tulivyokuwa tukiijua wenyewe. Walijua nini kiko wapi na kina faida gani. Wazungu wengi walibaki kulinda maslahi yao kwa kutumia dini. Kanisa Katoliki kwa upande wake walianza ujenzi wa Hospitali ya Bugando mnamo mwaka 1968. Ujenzi huo ulifanywa na kampuni ya Kiyahudi iliyoitwa COSATA. Wayahudi hao walijenga Bugando kwa ustadi mkubwa kama ambavyo walifanya kwa majengo mengine muhimu hapa nchini kama vile KCMC, jengo la Usalama wa Taifa, UDSM na Hospital ya Taifa ya Muhimbili. Lakini hata kabla hawajamaliza ujenzi wake sawasawa, Mwl. Nyerere aliwafukuza Wayahudi hao.
Ufunguzi wa hospitali hiyo ulifanyika rasmi tarehe 3 Novemba 1971. Na baadaye hospital hiyo ilitaifishwa na Serikali mwaka 1972.
Wengi hawakuelewa kwa nini Nyerere aliwafukuza Wayahudi hao. Kulikuwa na uvumi mwingi, lakini kwa sababu mimi kama mwanajeshi nilikuwa jirani sana na mkuu mmoja wa jeshi ambaye alining’ata sikio. Sababu ya kwanza ni ya kisiasa na msimamo wa Nyerere juu ya uhusiano wa Wayahudi na Wapelestina. Lakini pia, kulikuwa na sababu nyingine ya siri ambayo ndiyo inasumbua hadi leo. Nitakueleza sababu zote mbili zilizo sababisha Nyerere akosane na Wayahudi; ya kisiasa yaani uhusiano wa Wapalestina na Wayahudi na hiyo nyingine. Ila hiyo nyingine ndiyo ambayo inanifanya mimi na wewe tuwe tumejificha hapa hii leo.
Wewe ni msomi najua umesoma historia. Kama ujuavyo kuwa Ujerumani ilikuwa ikiitawala Tanganyika tangu mwaka 1885 mara baada ya Carl Peters kusaini mkataba wa kitapeli na viongozi wa kiafrika. Mtu huyo baadaye aliteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro – Moshi mnamo mwaka 1891. Jamaa alikuwa mkatili kiasi kuwa watu wa maeneo hayo walimwita Mkono wa Damu. Nadhani wajua mengi yaliyofanywa na Carl Peters hadi pale majaji wa Kijerumani walipotuma taarifa Ujerumani juu ya ukatili wa huyo jamaa na mwaka 1897 aliondolewa katika shughuli za kikoloni. Ujerumani ikaendelea kutawala Tanganyika huku wajerumani wakiongezeka kumiminika Tanganyika.
Nadhani unajua yaliyotokea kwenye Vita Kuu ya Pili ya Dunia, ambapo baadaye Ujerumani ilishindwa lakini wakati huohuo ikiacha wakimbizi wengi wa Kiyahudi ambao walikuwa wameikimbia Ujerumani. Hapo kabla Waingereza walikuwa wamenunua kama heka 50,000 ndani ya Tanganyika na kuwapangisha Wayahudi. Mara kwa mara Uingereza ilikuwa ikipendekeza kuwa ili kukabiliana na shida ya wakimbizi wa Kiyahudi ni vema Tanganyika, British Guiana, Kenya, Zimbabwe ya wakati huo na Nyasaland zikatengwa na kuwa makazi ya Wayahudi hao. Kwa hivyo baada ya Ujerumani kushindwa vita, nguvu ya chama cha NAZI na shughuli zake zikaathirika sana. Na sasa Tanganyika na Palestina zikawekwa kwenye mchakato wa kuzifanya kuwa makazi ya Wayahudi. Nchi kadhaa za Ulaya na Wamarekani wakawa kwenye kampeni kubwa kuhakikisha hilo linafanikiwa. Mapango huo haukufanikiwa kwa Tanganyika lakini ukafanikiwa kwa Palestina.
Haiko wazi sana kama Nyerere alipata taarifa za ule mpango wa mwaka 1930 wa kuifanya Tanganyika na Palestina kuwa makazi ya Wayahudi. Maana kwa wakati huo Nyerere alikuwa na miaka kumi na tano tu na ni wakati wakati vijana wa NAZI walipofanya maandamano kupinga Wayahudi kupewa Tanganyika. Maandamano hayo yalifanyika Moshi katika Shule ya Kijerumani ya Mweka. Hata hivyo, haina ubishi kuwa Nyerere alikuwa akijua vema historia ya Palestina wakati alipokua akiamua Sera ya Tanzania, kuhusiana na Palestina ule mwaka wa 1977 ambapo alisema anaitambua Palestina na kuwa anaunga mkono Palestine Liberation Organization (PLO). Ngoja nikueleze ili ulewe suala hili kwa upana, japo linaoneka la kisiasa lakini ni muhimu kwako kujua. Tanganyika muda wote ilikuwa mstari wa mbele katika kutaka Palestina ijitawale. Kumekuwa na mivutano mingi sana juu ya suala hili hadi leo. Lakini chanzo chake ni cha kihistoria zaidi. Sasa kuna watu wanaoamini kwa sehemu kubwa kuwa Nyerere hakupenda huduma ya Wayahudi na kuwaondoa kwenye miradi yote kwa sababu ya matashi yake kwa Wapalestina ambayo hayakuja hivi hivi bali yaliletwa na hisia kuwa Palestina na Tanganyika zingekuwa kwenye mkondo mmoja kama mambo yangekwenda kama ilivyopangwa kuwa zote ziwe makazi ya Wayahudi. Japo mpango huo haukufanikiwa kwa Tanganyika…” Kabla hajaendelea na maelezo walisikia mlio mwingine wa gari. Safari hii mlio uliashiria kuwa lilikuwa gari kubwa.
“Daaah! historia yako inasisimua lakini bado haijanipa picha yote ya hili tunalopitia.” Hatimaye Vivian alisema huku akiwa anasimama. Mzee Mwasumbi alijipenyeza hadi sehemu ambayo aliweza kuona upande lilikokuwa linatokea lile gari.
“Twende, ni Basi linakuja.” Mwasumbi alisema. Wote wakawa wanaelekea barabarani Walisimamisha gari na kuingia ndani. Basi lilikuwa limejaa sana hivyo kulikuwa na nafasi ya kusimama kwa shida. Gari lilitembea kwa dakika kama ishirini kisha, Mzee Mwasumbi akapiga kelele.
“Tushushe hicho Kijiji cha mbele hapo!”
Kweli gari lilipofika hicho Kijiji alichokusudia kushuka, lilisimama, wakashuka.
“Upande huu kuna ufukwe wa Ziwa Victoria, kutakuwa na watu wanatusubiri hapo.” Alisema huku wakiwa wanavuka barabara kwenda upande mwingine wa barabara.
Huko kulikuwa na makazi machache ya watu. Walianza kufuata barabara ndogo ya vumbi iliyokuwa ikitelemka kwenda sehemu ambayo Mwasumbi alisema wangekutana na ufukwe.
“Sasa hayo maelezo yako yanahusiana vipi na haya yanayotokea?” Vivian alihoji wakati wakitembea.
“Huyo mkubwa wangu wa jeshi anasema kuna sababu nyingine ya kiusalama ambayo ilisababisha Nyerere asitake Wayahudi waendelee kuwa hapa nchini. Wakati wa Vita ya Pili ya Dunia, Marekani na washirika wake walikuwa wanaelekea kushindwa, hadi pale Marekani walipofanikiwa kutumia lile bomu la Atomic na kuipiga Hiroshima na Nagasaki, Japan. Ili kulipua mabomu hayo, ilihitajika neno la siri ‘password’. Maneno ya siri ya kufyatulia mabomu hayo yalitengenezwa na kuwekwa na mtengenezaji ambaye ni Myahudi. Myahudi aliyevumbua bomu hilo, Bwana J. Robert Oppenheimer alitengeneza maneno ya siri. Neno la siri la lile bomu lililolipua Hiroshima lilikuwa ni ‘Little Boy’. Wakati lile neno la siri la lile bomu lililolipua Nagasaki ilikuwa ‘Fat Man’.
Baada ya kwisha vita hiyo, huku Marekani na washirika wake wakiwa wameshinda, ilikuja kugundulika kuwa, baada ya Bwana J. Robert Oppenheimer kulazimishwa kutoa kanuni za kutengeneza bomu hilo kwa Serikali ya Marekani, aliona kuna umuhimu wa kutengeneza bomu jingine ambalo likipigwa kwa wakati mmoja na lile la Atomic huondoa madhara yanayoweza kuletwa na bomu hilo la Atomic. Ikiwa na maana kuwa hilo bomu jingine lina uwezo wa kulidhibiti lile la Atomic. Inasemekana wazo hilo alikuwa nalo akiwa katika hatua za mwisho za kutengeneza bomu la Atomic. Hivyo alitengeneza kanuni ya kutengeneza hilo bomu jingine, lakini hadi leo haijulikani mahali ambapo kanuni hiyo imewekwa. Kumekuwa na harakati kubwa za kutafuta mahali ambapo Myahudi huyo alificha karatasi zenye kanuni hiyo. Mashirika ya ujasusi yanaamini kuwa kuna siri kubwa katika maneno ya siri aliyoyatoa Bwana J. Robert Oppenheimer kulipulia yale mabomu mawili ya Atomic. Maneno ‘Little Boy’ and ‘Fat Man’ inasemekana yana siri na ufunguo wa kujua sehemu na mtu ambaye ana kanuni ya kuwezesha kutengeneza hilo bomu jingine la kulidhibiti lile bomu la Atomic. Katika kuchimba na kufuatilia wapi hiyo kanuni inaweza kuwa, ilikuja kugundulika kuwa mjomba wake na Bwana J. Robert Oppenheimer aitwaye Eud Benjamin, ambaye aliingia Tanganyika miaka hiyo kama walivyoingia wakimbizi wengine ndiye Fat Man. Myahudi huyo alikuwa mtaalamu wa mambo ya utabibu wa binadamu. Hivyo akajikuta anaishia kuwa Daktari katika hospitali ya Bugando.
Daktari huyo alikuwa maarufu sana hadi pale alipouawa katika usiku ambao wewe, Milka na Maganga mlizaliwa. Wakati huo yaani mwaka 1981 alikuwa na umri wa miaka 41 na inaaminika wakati bomu la Atomic lilipotumika kwa mara ya kwanza kule Japan mwaka 1945 yeye alikuwa na miaka 5 tu.
Neno ‘Fat Man’ lilikuja kutambuliwa kuwa ndiyo huyo mjomba wa Bwana J. Robert Oppenheimer. Lakini neno Little Boy halikuwa limegundulika hadi hapo baadaye baada ya kifo cha huyo mjomba wake na mgunduzi wa bomu la Atomic, hapa namaanisha kifo cha Daktari wa Kiyahudi Eud Benjamin katika Hospitali ya Bugando …” Kabla hajaendelea Mwasumbi alikatishwa na swali la Vivian
“Kwa hiyo usiku ule tuliozaliwa una nini sasa?”
“Jambo la kwanza ninalotaka ujue ni kuwa wewe ni Milka na Milka ni wewe. Nikiwa na maana kuwa mama Maganga alienda kujifungulia Mwanza katika Hospitali ya Bugando. Alifanya hivyo kwa vile mama yake mzazi alikuwa akiishi Mwanza hivyo kama wafanyavyo wanawake wengi wa Ki-tanzania, huenda kujifungulia kwa mama zao. Maana hilo huwapa haueni ya kisaikolojia kuwa watapata msaada wa uzoefu toka kwa mama zao na hali ya kujaliwa itakuwa juu. Na kwa mujibu wa kumbukumbu zilizopatikana wakati wa kuzaliwa wewe na Maganga huduma ilitolewa na yule Daktari wa Kiyahudi. Kwa vile tayari mashirika mengi ya kimataifa ya Kijasusi yalikuwa yameshapata fununu kuhusiana na mahali alipokuwa huyo mjomba wake yule mgunduzi wa bomu la Atomic, walikuwa wameshaweka majajusi kufuatilia nyendo za huyo Myahudi kwa vile walikuwa wakitafuta maana ya neno Litle Boy na wapi zilipokuwa kanuni za kutengeneza bomu la kudhibiti bomu la Atomic…” Kabla Mwasumbi hajaendelea zaidi, mlio wa risasi ulisikika. Wote wakashtuka!
“Pancha au nini?” Vivian alihoji, hakuwa anajua mlio wa risasi. Hakuwahi kusikia wala kuona risasi ikipigwa.
“Hapana ni risasi!”
“Sikiliza, Vivian, sitaki watukamate wote, maana wewe sasa ni wa muhimu kuliko mimi, najihisi kama nimeshamaliza kazi yangu. Ufukweni si mbali toka hapa, ukifika huko, utakuta kuna boti ndogo ya kijani, waambie mimi nimekuelekeza kwenda pale, waambie Luteni Mwasumbi ameniagiza kuja, wao ni wanajeshi, hawajui wewe ni nani ila watakupeleka sehemu salama. Najua utaonana na Hellen, msimulie haya na yeye atakusimulia yote niliyomsimulia yeye na Maganga.
Ukiona mambo yanaharibika na unahitaji msaada wa haraka na uhakika basi utapiga hizi namba +255785975443…” Hata kabla Mwasumbi hajamaliza maelezo yake mara walisikia gari likiunguruma kuja upande waliokuwepo.
“Vivian, I love you so much and I always wanted to see you, nashukuru nimekuona. Jitahidi sana kuificha hiyo alama hapo pajani asiione mtu yeyote. Kama unataka kujua ukweli kuhusu hiyo namba na wakati huohuo uendelee kuwa salama, basi kuna watu wanne tu ambao unaweza kuwauliza. Mtu niliyekupa hiyo namba ya simu, Maganga, mimi au yule Daktari wa Kiyahudi japo na yeye anaweza kukudhuru akigundua kuwa umeshagundulika na unatafutwa….haya nenda…mimi nitajitahidi kuwazuia hapa ili kukupa wewe nafasi ya kufika ufukweni….tafadhali kuwa makini na kinywa chako.” Mwasumbi alisema hayo maneno kwa hisia kali kisha akamvuta Vivian na kumbusu. Wakati huu mlio wa gari ulikuwa jirani zaidi, Mwasumbi alimvuta Vivian hadi pembeni ya barabara, wakabana nyuma ya nyumba moja ya nyasi eneo hilo.
“Haya nenda, pita kwenye hayo mashamba hadi ufike ufukweni, ukiwapata nendeni, kama nitatoka hai najua nitakapokupata. Kama sitotoka hai nakutakia kila la heri mwanangu!”
“Mbona sikuelewi, unanitisha, unanihuzunisha, unanichanganya na kuniweka kwenye sintofahamu!” Viviani alimudu kusema huku akiwa anasukumwa na Mwasumbi kama ishara ya kumhimiza aondoke eneo lile.
“Natamani ningekusimulia kisa chote ila nachelea wote tutakuwa maiti hapa au twaweza kuangukia kwenye masahibu mazito na mateso. Chukua hii…” Hatimaye Mwasumbi, aling’oa nywele chache zilizokuwa kichwani kwake akampatia Vivian.
“Ipo siku utazihitaji hizi.” Mwasumbi alisema huku safari hii akichomoa bastola iliyokuwa mgongoni kwake.
“Go, go, go!” Alipiga kelele. Kusikia hivyo, Vivivan alikurupuka kuelekea kwenye vichaka vilivyokuwa kwenye mashamba yaliyokuwa jirani na eneo hilo. Alitembea kwa shida, maana hakuwa mtu aliyezoea taabu. Mawazo mengi yalikuwa kichwani. Kwa mara ya kwanza akajikuta anafanya kitu asichokielewa, ila hakuwa na namna zaidi ya kufanya hivyo. Alimfikiri Mwasumbi, alimfikiria Maganga na Milka kwa wakati mmoja huku akiwa bado anakatiza vichaka kueleke upande kulikokuwa na Pwani ya Ziwa Victoria.
Walitembea hadi walipofika barabara kuu.
“Twende tukasimame kwenye kile kichaka, tusubiri basi, tukifanikiwa kupata basi itakuwa vema zaidi. Maana nimeona si salama kuendelea kusafiri kwa lile gari lako. Kutumia gari lako itawapa urahisi wa kutupata haraka.” Alisema yule dereva huku akimuonesha Vivian kichaka alichotaka waende. Yule dereva alikimbia hadi kwenye kile kichaka, kuona hivyo Vivian na yeye alikimbia kizembe huku akiwa anakunywa juisi yake kuelekea pale alipoenda yule dereva. Vivian hakuelewa kwa nini alikuwa akitii kila alichoambiwa na yule dereva, lakini pia, hakuona sababu ya kutotii mradi awe na uhakika wa usalama wake.
“Wakati tukiwa hapa, nitajaribu kukuelezea kwa kifupi kuhusu mimi na wewe. Maana sina hakika nini kitafuata dakika chache kutoka sasa. Nimekaa miaka mingi nikiwa nasubiri muda kama huu ili niweze kufanya hiki nikifanyacho sasa kwa faida yenu na Taifa hili…” Alisema yule dereva huku akiwa anavua sura ya bandia aliyokuwa amevaa. Vivian aliweka chini boksi la juisi aliyokuwa anakunywa.
“Naitwa Mwasumbi, Luteni Mwasumbi.”
“Ooooh my God!, kwa hiyo muda wote ule tulikuwa tukiongea na wewe kule kijijini tukidhani kuwa u Askofu Alphonso kumbe haikuwa kweli! Kwa nini umeamua kufanya hivi?” Vivian alisema kwa mshangao mkubwa. Huku sasa akitazamana na sura ya mtu mwingine tofauti na ile ya Askofu Alphonso. Kabla Mwasumbi hajajibu walisikia mlio wa gari ukija kwa kasi. Vivian alitaka kukimbilia barabarani ili kulisimamisha.
“Stop!, usifanye hivyo Vivian, nimekwambia tutapanda basi, huo mlio wa gari si wa basi ni wa gari ndogo tu tena wanaweza kuwa wenyewe!” Mwasumbi alisema huku akimshika mkono Vivian na kuukandamiza chini, Vivian akaanguka chini kutokana na ule mkandamizo.
“Wewe vipi sasa tusipopata hilo basi tutalala hapa? Si bora tukaomba msaada kwenye magari madogo yanayoelekea Kamanga.” Vivian aling’aka kwa hasira na mshangao. “Sikiliza we mtoto, si muda mrefu utajua uko kwenye kisa gani na kwa nini unatafutwa san…” Kauli ya Mwasumbi ilikatishwa na mlio wa gari lilokuwa likija kwa kasi. Mlio ulionyesha kuwa lilikuwa karibu sana na pale walipokuwa wamejificha na lilikuwa kwenye mwendo wa kasi. Mwasumbi alisogea na kuchungulia barabarani kupitia matawi ya kile kichaka walichokuwepo. Macho yake yaliweza kuliona gari aina ya Land Rover 110 rangi ya kijani likiwa na alama kubwa nyeupe, alama hiyo ilikuwa herufi T ubavuni.
“Oooh yeah!, unaona sasa ndiyo wenyewe, wanatutafuta!” Mwasumbi alisema kwa kunong’ona. Vivian alibaki ametoa macho wala hakuwa anajua kinachoendela.
“Vivian, naomba nikueleze kwa kirefu kuhusu kisa hiki. Mwaka 1967 kulikuwa na harakati kubwa sana hapa nchini. Ilikuwa ni wakati ambao Mwalimu Nyerere alikuwa katika harakati kubwa za kutaka kuonyesha kuwa nchi ilikuwa huru kutoka katika mikono ya wakoloni. Mambo mengi yalifanyika, nuruni na gizani, ya kusemeka na ambayo hatuwezi hata kuyatamka. Mengi yalitokea, machache yaliandikwa na ambayo mnaweza kuyasoma leo. Harakati ziliendelea sana hadi mwaka 1976 ambapo wazungu wengi walikuwa wameshaondoka nchini na Nyerere akaikoleza zaidi ile sera ya Ujamaa na misingi ya Kujitegemea. Kama nilivyosema, kulikuwa na harakati nyingi sana ila ukweli ulikuwa wazi sana kuwa, wazungu waliokuwa hapa nchini walikuwa wakiijua nchi yetu kuliko tulivyokuwa tukiijua wenyewe. Walijua nini kiko wapi na kina faida gani. Wazungu wengi walibaki kulinda maslahi yao kwa kutumia dini. Kanisa Katoliki kwa upande wake walianza ujenzi wa Hospitali ya Bugando mnamo mwaka 1968. Ujenzi huo ulifanywa na kampuni ya Kiyahudi iliyoitwa COSATA. Wayahudi hao walijenga Bugando kwa ustadi mkubwa kama ambavyo walifanya kwa majengo mengine muhimu hapa nchini kama vile KCMC, jengo la Usalama wa Taifa, UDSM na Hospital ya Taifa ya Muhimbili. Lakini hata kabla hawajamaliza ujenzi wake sawasawa, Mwl. Nyerere aliwafukuza Wayahudi hao.
Ufunguzi wa hospitali hiyo ulifanyika rasmi tarehe 3 Novemba 1971. Na baadaye hospital hiyo ilitaifishwa na Serikali mwaka 1972.
Wengi hawakuelewa kwa nini Nyerere aliwafukuza Wayahudi hao. Kulikuwa na uvumi mwingi, lakini kwa sababu mimi kama mwanajeshi nilikuwa jirani sana na mkuu mmoja wa jeshi ambaye alining’ata sikio. Sababu ya kwanza ni ya kisiasa na msimamo wa Nyerere juu ya uhusiano wa Wayahudi na Wapelestina. Lakini pia, kulikuwa na sababu nyingine ya siri ambayo ndiyo inasumbua hadi leo. Nitakueleza sababu zote mbili zilizo sababisha Nyerere akosane na Wayahudi; ya kisiasa yaani uhusiano wa Wapalestina na Wayahudi na hiyo nyingine. Ila hiyo nyingine ndiyo ambayo inanifanya mimi na wewe tuwe tumejificha hapa hii leo.
Wewe ni msomi najua umesoma historia. Kama ujuavyo kuwa Ujerumani ilikuwa ikiitawala Tanganyika tangu mwaka 1885 mara baada ya Carl Peters kusaini mkataba wa kitapeli na viongozi wa kiafrika. Mtu huyo baadaye aliteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro – Moshi mnamo mwaka 1891. Jamaa alikuwa mkatili kiasi kuwa watu wa maeneo hayo walimwita Mkono wa Damu. Nadhani wajua mengi yaliyofanywa na Carl Peters hadi pale majaji wa Kijerumani walipotuma taarifa Ujerumani juu ya ukatili wa huyo jamaa na mwaka 1897 aliondolewa katika shughuli za kikoloni. Ujerumani ikaendelea kutawala Tanganyika huku wajerumani wakiongezeka kumiminika Tanganyika.
Nadhani unajua yaliyotokea kwenye Vita Kuu ya Pili ya Dunia, ambapo baadaye Ujerumani ilishindwa lakini wakati huohuo ikiacha wakimbizi wengi wa Kiyahudi ambao walikuwa wameikimbia Ujerumani. Hapo kabla Waingereza walikuwa wamenunua kama heka 50,000 ndani ya Tanganyika na kuwapangisha Wayahudi. Mara kwa mara Uingereza ilikuwa ikipendekeza kuwa ili kukabiliana na shida ya wakimbizi wa Kiyahudi ni vema Tanganyika, British Guiana, Kenya, Zimbabwe ya wakati huo na Nyasaland zikatengwa na kuwa makazi ya Wayahudi hao. Kwa hivyo baada ya Ujerumani kushindwa vita, nguvu ya chama cha NAZI na shughuli zake zikaathirika sana. Na sasa Tanganyika na Palestina zikawekwa kwenye mchakato wa kuzifanya kuwa makazi ya Wayahudi. Nchi kadhaa za Ulaya na Wamarekani wakawa kwenye kampeni kubwa kuhakikisha hilo linafanikiwa. Mapango huo haukufanikiwa kwa Tanganyika lakini ukafanikiwa kwa Palestina.
Haiko wazi sana kama Nyerere alipata taarifa za ule mpango wa mwaka 1930 wa kuifanya Tanganyika na Palestina kuwa makazi ya Wayahudi. Maana kwa wakati huo Nyerere alikuwa na miaka kumi na tano tu na ni wakati wakati vijana wa NAZI walipofanya maandamano kupinga Wayahudi kupewa Tanganyika. Maandamano hayo yalifanyika Moshi katika Shule ya Kijerumani ya Mweka. Hata hivyo, haina ubishi kuwa Nyerere alikuwa akijua vema historia ya Palestina wakati alipokua akiamua Sera ya Tanzania, kuhusiana na Palestina ule mwaka wa 1977 ambapo alisema anaitambua Palestina na kuwa anaunga mkono Palestine Liberation Organization (PLO). Ngoja nikueleze ili ulewe suala hili kwa upana, japo linaoneka la kisiasa lakini ni muhimu kwako kujua. Tanganyika muda wote ilikuwa mstari wa mbele katika kutaka Palestina ijitawale. Kumekuwa na mivutano mingi sana juu ya suala hili hadi leo. Lakini chanzo chake ni cha kihistoria zaidi. Sasa kuna watu wanaoamini kwa sehemu kubwa kuwa Nyerere hakupenda huduma ya Wayahudi na kuwaondoa kwenye miradi yote kwa sababu ya matashi yake kwa Wapalestina ambayo hayakuja hivi hivi bali yaliletwa na hisia kuwa Palestina na Tanganyika zingekuwa kwenye mkondo mmoja kama mambo yangekwenda kama ilivyopangwa kuwa zote ziwe makazi ya Wayahudi. Japo mpango huo haukufanikiwa kwa Tanganyika…” Kabla hajaendelea na maelezo walisikia mlio mwingine wa gari. Safari hii mlio uliashiria kuwa lilikuwa gari kubwa.
“Daaah! historia yako inasisimua lakini bado haijanipa picha yote ya hili tunalopitia.” Hatimaye Vivian alisema huku akiwa anasimama. Mzee Mwasumbi alijipenyeza hadi sehemu ambayo aliweza kuona upande lilikokuwa linatokea lile gari.
“Twende, ni Basi linakuja.” Mwasumbi alisema. Wote wakawa wanaelekea barabarani Walisimamisha gari na kuingia ndani. Basi lilikuwa limejaa sana hivyo kulikuwa na nafasi ya kusimama kwa shida. Gari lilitembea kwa dakika kama ishirini kisha, Mzee Mwasumbi akapiga kelele.
“Tushushe hicho Kijiji cha mbele hapo!”
Kweli gari lilipofika hicho Kijiji alichokusudia kushuka, lilisimama, wakashuka.
“Upande huu kuna ufukwe wa Ziwa Victoria, kutakuwa na watu wanatusubiri hapo.” Alisema huku wakiwa wanavuka barabara kwenda upande mwingine wa barabara.
Huko kulikuwa na makazi machache ya watu. Walianza kufuata barabara ndogo ya vumbi iliyokuwa ikitelemka kwenda sehemu ambayo Mwasumbi alisema wangekutana na ufukwe.
“Sasa hayo maelezo yako yanahusiana vipi na haya yanayotokea?” Vivian alihoji wakati wakitembea.
“Huyo mkubwa wangu wa jeshi anasema kuna sababu nyingine ya kiusalama ambayo ilisababisha Nyerere asitake Wayahudi waendelee kuwa hapa nchini. Wakati wa Vita ya Pili ya Dunia, Marekani na washirika wake walikuwa wanaelekea kushindwa, hadi pale Marekani walipofanikiwa kutumia lile bomu la Atomic na kuipiga Hiroshima na Nagasaki, Japan. Ili kulipua mabomu hayo, ilihitajika neno la siri ‘password’. Maneno ya siri ya kufyatulia mabomu hayo yalitengenezwa na kuwekwa na mtengenezaji ambaye ni Myahudi. Myahudi aliyevumbua bomu hilo, Bwana J. Robert Oppenheimer alitengeneza maneno ya siri. Neno la siri la lile bomu lililolipua Hiroshima lilikuwa ni ‘Little Boy’. Wakati lile neno la siri la lile bomu lililolipua Nagasaki ilikuwa ‘Fat Man’.
Baada ya kwisha vita hiyo, huku Marekani na washirika wake wakiwa wameshinda, ilikuja kugundulika kuwa, baada ya Bwana J. Robert Oppenheimer kulazimishwa kutoa kanuni za kutengeneza bomu hilo kwa Serikali ya Marekani, aliona kuna umuhimu wa kutengeneza bomu jingine ambalo likipigwa kwa wakati mmoja na lile la Atomic huondoa madhara yanayoweza kuletwa na bomu hilo la Atomic. Ikiwa na maana kuwa hilo bomu jingine lina uwezo wa kulidhibiti lile la Atomic. Inasemekana wazo hilo alikuwa nalo akiwa katika hatua za mwisho za kutengeneza bomu la Atomic. Hivyo alitengeneza kanuni ya kutengeneza hilo bomu jingine, lakini hadi leo haijulikani mahali ambapo kanuni hiyo imewekwa. Kumekuwa na harakati kubwa za kutafuta mahali ambapo Myahudi huyo alificha karatasi zenye kanuni hiyo. Mashirika ya ujasusi yanaamini kuwa kuna siri kubwa katika maneno ya siri aliyoyatoa Bwana J. Robert Oppenheimer kulipulia yale mabomu mawili ya Atomic. Maneno ‘Little Boy’ and ‘Fat Man’ inasemekana yana siri na ufunguo wa kujua sehemu na mtu ambaye ana kanuni ya kuwezesha kutengeneza hilo bomu jingine la kulidhibiti lile bomu la Atomic. Katika kuchimba na kufuatilia wapi hiyo kanuni inaweza kuwa, ilikuja kugundulika kuwa mjomba wake na Bwana J. Robert Oppenheimer aitwaye Eud Benjamin, ambaye aliingia Tanganyika miaka hiyo kama walivyoingia wakimbizi wengine ndiye Fat Man. Myahudi huyo alikuwa mtaalamu wa mambo ya utabibu wa binadamu. Hivyo akajikuta anaishia kuwa Daktari katika hospitali ya Bugando.
Daktari huyo alikuwa maarufu sana hadi pale alipouawa katika usiku ambao wewe, Milka na Maganga mlizaliwa. Wakati huo yaani mwaka 1981 alikuwa na umri wa miaka 41 na inaaminika wakati bomu la Atomic lilipotumika kwa mara ya kwanza kule Japan mwaka 1945 yeye alikuwa na miaka 5 tu.
Neno ‘Fat Man’ lilikuja kutambuliwa kuwa ndiyo huyo mjomba wa Bwana J. Robert Oppenheimer. Lakini neno Little Boy halikuwa limegundulika hadi hapo baadaye baada ya kifo cha huyo mjomba wake na mgunduzi wa bomu la Atomic, hapa namaanisha kifo cha Daktari wa Kiyahudi Eud Benjamin katika Hospitali ya Bugando …” Kabla hajaendelea Mwasumbi alikatishwa na swali la Vivian
“Kwa hiyo usiku ule tuliozaliwa una nini sasa?”
“Jambo la kwanza ninalotaka ujue ni kuwa wewe ni Milka na Milka ni wewe. Nikiwa na maana kuwa mama Maganga alienda kujifungulia Mwanza katika Hospitali ya Bugando. Alifanya hivyo kwa vile mama yake mzazi alikuwa akiishi Mwanza hivyo kama wafanyavyo wanawake wengi wa Ki-tanzania, huenda kujifungulia kwa mama zao. Maana hilo huwapa haueni ya kisaikolojia kuwa watapata msaada wa uzoefu toka kwa mama zao na hali ya kujaliwa itakuwa juu. Na kwa mujibu wa kumbukumbu zilizopatikana wakati wa kuzaliwa wewe na Maganga huduma ilitolewa na yule Daktari wa Kiyahudi. Kwa vile tayari mashirika mengi ya kimataifa ya Kijasusi yalikuwa yameshapata fununu kuhusiana na mahali alipokuwa huyo mjomba wake yule mgunduzi wa bomu la Atomic, walikuwa wameshaweka majajusi kufuatilia nyendo za huyo Myahudi kwa vile walikuwa wakitafuta maana ya neno Litle Boy na wapi zilipokuwa kanuni za kutengeneza bomu la kudhibiti bomu la Atomic…” Kabla Mwasumbi hajaendelea zaidi, mlio wa risasi ulisikika. Wote wakashtuka!
“Pancha au nini?” Vivian alihoji, hakuwa anajua mlio wa risasi. Hakuwahi kusikia wala kuona risasi ikipigwa.
“Hapana ni risasi!”
“Sikiliza, Vivian, sitaki watukamate wote, maana wewe sasa ni wa muhimu kuliko mimi, najihisi kama nimeshamaliza kazi yangu. Ufukweni si mbali toka hapa, ukifika huko, utakuta kuna boti ndogo ya kijani, waambie mimi nimekuelekeza kwenda pale, waambie Luteni Mwasumbi ameniagiza kuja, wao ni wanajeshi, hawajui wewe ni nani ila watakupeleka sehemu salama. Najua utaonana na Hellen, msimulie haya na yeye atakusimulia yote niliyomsimulia yeye na Maganga.
Ukiona mambo yanaharibika na unahitaji msaada wa haraka na uhakika basi utapiga hizi namba +255785975443…” Hata kabla Mwasumbi hajamaliza maelezo yake mara walisikia gari likiunguruma kuja upande waliokuwepo.
“Vivian, I love you so much and I always wanted to see you, nashukuru nimekuona. Jitahidi sana kuificha hiyo alama hapo pajani asiione mtu yeyote. Kama unataka kujua ukweli kuhusu hiyo namba na wakati huohuo uendelee kuwa salama, basi kuna watu wanne tu ambao unaweza kuwauliza. Mtu niliyekupa hiyo namba ya simu, Maganga, mimi au yule Daktari wa Kiyahudi japo na yeye anaweza kukudhuru akigundua kuwa umeshagundulika na unatafutwa….haya nenda…mimi nitajitahidi kuwazuia hapa ili kukupa wewe nafasi ya kufika ufukweni….tafadhali kuwa makini na kinywa chako.” Mwasumbi alisema hayo maneno kwa hisia kali kisha akamvuta Vivian na kumbusu. Wakati huu mlio wa gari ulikuwa jirani zaidi, Mwasumbi alimvuta Vivian hadi pembeni ya barabara, wakabana nyuma ya nyumba moja ya nyasi eneo hilo.
“Haya nenda, pita kwenye hayo mashamba hadi ufike ufukweni, ukiwapata nendeni, kama nitatoka hai najua nitakapokupata. Kama sitotoka hai nakutakia kila la heri mwanangu!”
“Mbona sikuelewi, unanitisha, unanihuzunisha, unanichanganya na kuniweka kwenye sintofahamu!” Viviani alimudu kusema huku akiwa anasukumwa na Mwasumbi kama ishara ya kumhimiza aondoke eneo lile.
“Natamani ningekusimulia kisa chote ila nachelea wote tutakuwa maiti hapa au twaweza kuangukia kwenye masahibu mazito na mateso. Chukua hii…” Hatimaye Mwasumbi, aling’oa nywele chache zilizokuwa kichwani kwake akampatia Vivian.
“Ipo siku utazihitaji hizi.” Mwasumbi alisema huku safari hii akichomoa bastola iliyokuwa mgongoni kwake.
“Go, go, go!” Alipiga kelele. Kusikia hivyo, Vivivan alikurupuka kuelekea kwenye vichaka vilivyokuwa kwenye mashamba yaliyokuwa jirani na eneo hilo. Alitembea kwa shida, maana hakuwa mtu aliyezoea taabu. Mawazo mengi yalikuwa kichwani. Kwa mara ya kwanza akajikuta anafanya kitu asichokielewa, ila hakuwa na namna zaidi ya kufanya hivyo. Alimfikiri Mwasumbi, alimfikiria Maganga na Milka kwa wakati mmoja huku akiwa bado anakatiza vichaka kueleke upande kulikokuwa na Pwani ya Ziwa Victoria.