kilimobiznet
Member
- Jun 14, 2015
- 25
- 12
Habari wadau,
Salam kutoka Kilimo Business na Sekretarieti ya Chama cha wakulima wahitimu Tanzania (Tanzania Graduate Farmers Association www.graduatefarmers.co.tz).
Kwa niaba ya sekretatiat ya TGFA na Kilimo Business tunapenda kuwatangazia kuwa Kilimo Business and Associates kwa Kushirikiana na Tanzania Graduate Farmers Association (TGFA) inaendelea kuuza mbegu bora za mazao ya MBAAZI, CHOROKO, DENGU, MAHARAGWE na KUNDE zenye uzao wa kutosha na kuendana na mazingira husika kote nchini. Mbegu hizi zimezalishwa na makampuni yaliyothibitishwa na pia kuthibitishwa na Mamlaka za ubora Tanzania na kununuliwa na TGFA kwa ajili ya kusambazwa kwa wanachama wake na wakulima waliojisajili na watakaohitaji kote Tanzania.
KWA NINI NI MUHIMU KUJIPATIA MBEGU ZINAZOSAMBAZWA NA TGFA?!
1. Kupata mbegu za hakika na zilizothibitishwa na Taasisi za viwango kwa bei nzuri.
2. Kupata ushauri elekezi wa mbinu bora za kilimo kuzingatia sheria na taratibu
3. Kuunganishwa na soko la hakika ndani na nje ya nchi kupitia mradi wa SITA (Kuhudumia masoko ya India na Asia) kupitia kampuni za IMARA (INDIA), Quality Pulses, ETG, KIBUASA, Ndota Farms n.k
4. Kuunganishwa katika network ya wazalishaji na wasindikaji wa mazao jamii ya mikunde.
5. Kuunganishwa na wataalamu na washauri waliobobea katika sayansi ya kilimo na utunzaji wa zao husika.
6. Kuwa miongoni wa wanachama wa TGFA
Namna ya kupata na kutoa oda ya mbegu
1. Toa order yako kwa njia ya namba zifuatazo tupigie simu ama email kilimobizne@gmail.com cc info@graduatefarmers.co.tz ama tandikie sms kwa 0789856246 ama whatsapp 0753843321 hapo juu ama
2. Jaza Form kwa njia ya mtandao Fomu ya Taarifa muhimu za wakulima na wadau wa Mbaazi, Choroko, Dengu, Maharage n.k kwa ajili ya taarifa muhimu za Mradi wako (Taarifa hizi ni siri hazitatolewa kwa yeyote yule)
Angalizo: Kuwa na taarifa muhimu za eneo unalotaka kulima, aina na kiasi cha mbegu unahitaji na lini
(Kama huna taarifa za kutosha tafadhali tupigie simu ama email kilimobizne@gmail.com cc info@graduatefarmers.co.tz ama tandikie sms kwa 0789856246 ama whatsapp 0753843321 anza kwa jina lako na namba ya simu na ulipo)
Aina za mbegu na muda wa kupatikana: Mbegu za mazao hayo ziko aina tofauti tofauti kulingana na eneo na hata uhitaji wa soko hivyo ZINGATIA hali ya hewa ya eneo lako na hata uhitaji wa soko. USILIME TU KWA SABABU MIKUNDE NI DILI halafu ukakosa soko.
MUDA WA UPATINAJI WA MBEGU: Mbegu hizi zitaanza kuuzwa na kupatikana mwez wa 9 katikati mpaka wa 1 mwishoni. Kokote Tanzania utapata mbegu utakazotaka na katika vituo ambavyo utaelekezwa.
Zingatia
- Epuka kununua mbegu sokoni ama minadani na ambazo hazijafungashwa kwani sio tu utapata mbegu zisizo na ubora bali waweza sambaza magonjwa ambayo yako katika mbegu hiyo
- Epuka kununua mbegu ambayo imeisha muda wake kukaa katika kifungashio. Unashauriwa kununua mbegu yenye maelezo ya kutosha ikionyesha battch namba, aina, tarehe ya kuzalishwa na tarehe ya kupakiwa na hata asilimia ya uzao kwa kiasi cha mbegu
- Usinunue mbegu iliyokaa dukani zaidi ya miezi 6 mpaka utakapojiridhisha ama kuuliza mtaalamu kwani uzao wake utakuwa umepungua.
- Usinunue mbegu na kuotesha pasina kuuliza na kupata ushauri kwamba bi aina hgani na wakati gani kuotesha ama kuvuna
- Usilime ama kuzalisha bila kuwa na taarifa ya kutosha kuhusuhitaji la soko hasa kuzingatia aina, ufungashaji, uchukuzi na hata aina ya mazao yanayohitajina na viwango vya ubora
TGFA NI AKINA NANI?
TGFA www.graduatefarmers.co.tz ni Taasisi iliyosajiliwa mwaka 2000 kama taasisi ya Kiraia katika sekta binafsi yenye nia ya kuwaunganisha WAJASIRIAMALI KATIKA KILIMO BIASHARA kote Tanzania. TGFA ina makao makuu Morogoro na wawakilishi katika mikoa na wilaya zote Tanzania na ina nia ya kukuza biashara zao, kupata masoko ya hakika, kupata pembejeo kwa pamoja na bei nzuri, kuendeleza elimu na uelewa wa wanachama na jamii pamoja na kutoa ushauri elekezi katika minyororo ya thamani ya kilimo biashara kama uzalishaji, usindikaji, usafiri, teknolojia, habari n.k . KWa sasa TGFA ina wanachama 5000 ambapo wanachama 300 ni vikundi na taasisi za vijana wajasiriamali, 20 makampuni, 15 Vyama vya ushirika. TGFA ni mwanachama hai wa TAHA, EAGC, ANSAF, TPSF na ACT.
Mazao jamii ya mikunde kwa takriban miaka minne 4 sasa yamekuwa na uhitaji mkubwa sana sokoni hasa masoko ya nje (Mbaazi na Dengu) lakini pia kumekuwa na changamoto kubwa sana ya upatikanaji wa pembejeo bora, salama na za hakika hasa mbegu, Mbolea na Mashine.
Kutatua changamoto hiyo TGFA kuanzia mwaka 2015 imekuwa ikitoa huduma ya kusambaza mbegu bora na ushauri wa kilimo bora cha mazao jamii ya Kunde na hata kuwaunganisha na masoko ya ndani na nje ya nchi. Mwaka 2014 TGFA iliweza kusambaza jumla ya tani 8 za mbegu za mbaazi kwa wanachama wake tu na mwaka 2015 iliweza kusambaza mbegu za mbaazi tani 10, choroko tani 3 na Degu tani 3 na iliweza kuunganisha wanachama wake na wanunuzi.
KILIMO BUSINESS AND ASSOCIATES NIAKINA NANI?!
Kilimo Business ni Kampuni ya kibiashara iliyosajiliwa mwaka 2015 yenye nia ya kusambaza bidhaa na huduma katika mnyororo wa thamani wa kilimo Biashara iliyo na makao makuu Arusha na wawakilishi katika majiji na mji mikubwa Tanzania.
Tunapenda kutoa shukrani kwa wadau mbalimbali wanaoshiriki na kuomba kushiriki kwenye mafunzo na semina elekezi ya Kilimo Biashara cha mazao jamii ya mikunde hasa Choroko, Dengu, Mbaazi, Kunde, Ngwara n.k.
MRADI WA KUSAMBAZA MBEGU BORA NA USHAURI WA MAZAO JAMII YA KUNDE NA NAFAKA
Chama cha Wakulima Whitimu Tanzania (Tanzania Graduate Farmers Association www.graduatefarmers.co.tz wameignia mkataba na Wasambazaji wa mbegu, Wanunuzi wa mazao jamii ya mikunde kama IMARA, ETG, QUALITY PULES, KILIMO MARKETS ambao wana masoko tayari INDIA na nje ya nchi ili kuweza kusambaza mbegu bora na kuunganisha wazalishaji na masoko. Hivyo TGFA imeingia mkataba na mamlaka za uthibiti wa mbegu na usafirishaji wa Mbegu ili kuwawezesha wajasiriamali na wakulima walio na nia na uzoefu katika kilimo biashara kununua mbegu hizi kwa Wakati na kwa njia salama.
Kwa mawasiliano zaidi piga simu ama tuma sms kwa namba 0789856246 ama 0718664645 ama 0753843321 omba kuongea na Juma Bruno Ngomuo. Email ni kilimobiznet@gmail.com