SoC04 Serikali ifanye haya kwenye kilimo kuhakikisha taifa linapiga hatua

Tanzania Tuitakayo competition threads

Edson Eagle

Member
Apr 20, 2024
26
11
Serikali itizame katika mambo yafuatayo ili kuhakikisha Tanzania tunapiga hatua katika kilimo kwa miaka ijayo.

1. Kuhakikisha wakulima na wafugaji wanapewa elimu itakayowaongoza katika kutengeneza kilimo kilicho bora na chenye manufaa makubwa.

2. Kuwe na utaratibu mzuri utakao wainua wakulima na wafugaji kifedha ili waweze kumudu gharama zakuendesha kilimo na ufugaji ulio bora.

3. Viongozi kwa kushirikiana na wataalamu wa kilimo na ufugaji wahakikishe wanawatembelea wakulima mara kwa mara kujua maendeleo yao na changamoto zinazowakabiri.

4. Kutengeneza masoko imara na yenye muongozo mzuri ili wakulima wanapoamua kuuza mazao yao wawe na sehemu ya kuuzia tena kwa bei nzuri.

5. Kuboresha nyanja zote za kilimo ikiwa ni pamoja na vyanzo vya maji ili kuwafanya wakulima waendeshe kilimo chao bila kuwa na hofu ya kukosekana kwa mvua ama mvua kuzidi.

6. Kuruhusu uwepo wa wawekezaji wa nje(wenye kuleta manufaa nasio kinyume chake) katika sekta ya kilimo na ufugaji ili kuweka ushindani katika uzalishaji wa mazao bora.

7. Kuwepo na mipaka baina ya wakulima na wafugaji ili kuepusha migogoro isiyo ya lazima katika sekta ya kilimo.

8. Kuhakikisha mbolea, mbegu na dawa zinazozalishwa kwaajiri ya kutumika kwa wakulima zinachunguzwa kwa usahihi nakuthibitishwa juu ya ubora wake ili ziwe zenye kuleta manufaa.
 
Kuhakikisha mbolea, mbegu na dawa zinazozalishwa kwaajiri ya kutumika kwa wakulima zinachunguzwa kwa usahihi nakuthibitishwa juu ya ubora wake ili ziwe zenye kuleta manufaa.
Well, tuwe na nfumo wa kuwawajibisha watakaoleta uzembe katika ubora. Hili ni kosa la uhujumu uchumi binafsi kabisa.

Niweke mbolea hewa, au nipulize dawa feki au chanjo feki halafu nipate hasara. Inabidi niwashtaki mnyororo mzima wa bidhaa hiyo hadi mchawi apatikane.

Asante kwa andiko
 
Back
Top Bottom