William Mshumbusi
JF-Expert Member
- Mar 27, 2012
- 1,792
- 2,421
Jamani naomba ushauri juu ya híi cm ya mke wangu.
Tulianza urafiki tu kama miaka mitatu ivi wote tukiwa chuo. Kwa wakati huo alikuwa na cm nzuri aina ya samsung ila kila tukikaa nae alikuwa anaacha cm kwingine mara rafiki yangu anachati nayo facebook, mara haina chaji, mara nimeisahau na sababu nyingi tu na sikuweza ata kuigusa kwa takribani miaka miwili.
Kwa kuwa niko mwaminifu sana nilijaribu kuicha cm yangu wazi kwake. Zinaingia sms bila kujua ya nani namwambia nisomee, alikuwa akikataa lkn baadae alikubaliana na hayo. Siku nyingine najifanya kama nimeisahau kwake ili kuonesha uaminifu.
Baada ya ndoa alikuja bila cm. Alisema cm yake ilipotea siku ya harusi kwenye salóon aliyokuwa akipambwa na wamemfidia fedha taslim na haoni haja ya kununua cm kwani atakuwa anatumia yangu.
Mwezi wa sita mwaka jana nilipata safari ya kikazi nikalazimika kumnunulia cm ila tuwasiliane nae tukiwa mbali.
Cha kushangaza cm hiyo anaificha sana. Ikiita anaweza asipokee. Aniambii lolote kuhusiana na cm labda nani kapiga kasema nini ananisalimia au la kama ambavyo nafanya mimi.
Akiöngea kwenye cm mazungumzo ni ya mkato na yasiyoeleweka. Utasikia mara Sawa.... Aa.... Sina... Nimesahau..... Yupo. Au nimeelewa yani neno moja tu alafu anakata cm.
Kingine amejiunga na facebook nazani kwa jina jingine kwani yuko bize na facebook lakini kila nikimtafuta kwenye fb simpati.
Leo ndio alikuwa ameenda kujifungua kwa bahati nzuri nikabahatika kushika cm yake na kuifungua ni password kila sehemu, fonebook, sms, call log na kadhalika.
Nishaurini nifanye nini na cm ya mke wangu.
Nilifika hospital leo asubui sana saa moja kasoro. Nikamfata mke wangu kumsabai
alikuwa akisubiri ruhusa. Kwa upole nikamuuliza juu ya password. Nakumwomba anijibu ili roho itulie na nianze kufikiri juu ya mtoto pekee. Mke badala ya kunijibu akaangua kilio wodini. Ni machozi macho mekundu analia tu. Sikujua analilia nini.
Mida ya saa moja na nusu daktari wa zamu alipofika alipokuta kile kilio akaniuliza kunanini. Nikamjibu anasema dumbo linamuuma. Sasa imebidi asiruhusiwe mpaka mchana waone hali yake.
Sa analilia nini ata sijui. Na kwanini asinipe tu hiyo password mi moyo utulie .
Ma mkwe nae katimba hosptal imebidi tu kumdokeza kasema nisubiri kidogo nae kama kanishangaa iv
UP TO DATE 15th Jan 2013 20:00
Nilienda kwa fundi simu nikaambiwa angeweza kuondoa password kwa kuifrash CM Ila itafuta kila kumbukumbu yani sms zote, majina na itakuwa kama mpya nikaona nimekwama hapo. Nikaenda kwenye ofisi za tigo nikiwa na laini yake kitambulisho chake na cheti cha ndoa yetu.
Wakakataa kunipa ushirikiano wakidai mpaka nipewe idhini police. Wanadai wangewajibika kama ningepata habari ambazo zingepelekea mtu kudhurika na wanalinda uhuru wa mteja.
Nikaenda police wamesema hawezi kuunda shitaka la kijinai au la madai ambalo lingepelekea wao kunipa idhini kufatilia cm wala laini.
Kufika hospitali tayari mke wangu alikuwa karuhusiwa.
Nikafika nyumbani majira ya saa 10 jioni. Nikamkuta ma mkwe, Mama mzazi, shangazi mmoja na nikaambiwa mchungaji ba mkwe yupo njiani anakuja na kunamaongezi sebuleni.
Kabla ya mazungumzo mke wangu alitoa sara kali kukemea na kufukuza mapepo.
Mama mzazi akaanza kunilalamikia kuwa sijafurahia mtoto. Mbona sikuuliza kabla mpaka sku ya kujifungua. Sijatoa pole kwa mzazi mara cn zawadi.
Katikati ya mazungumzo mke akadakia "password ni mwaka wangu wa kuzaliwa"
Jamani aibu. Nikatoa laini ile nilikuwa nimeitoa kwenye CM YAKE na kuweka kwenye Cm yangu. Mama yangu mzazi akaja pembeni yangu. Kuweka mwaka wake tu laini ile ikafunguka. Masikini aibu....
Fonebook hakuna kitu. Hakuna sms wala nini.
Kwa aibu sikuona haja ya ya kufata cm yake kuifungua tena mbele yao. Nikaomba msamaha tukasameheana wote mama akatoa tsh 50,000 na mama mkwe hivo ivo shangazi akatoa ahadi tu. Kabla ya kufunga mazungumzo mchungaji na Baba wakafika. Wakaambiwa mi ni mtoto yameisha tukapiga sara tu.)
mh kuifata cm yake lengo nimrudishie wife mara ikaingia sms. Kuiangalia ilikuwa ni sms ya 17 toka nichukue cm. Na nikaona kuna misscall kibao.
Nikasema nizisome zote ndio nirizike...
Masikini password tulizopewa hazifungui cm hii. Nikamuuliza tena mbona cm haifunguki na hizo password.
Alivyonijibu sasa ni amazing. Ni kwa kuashiria kiburi ila maneno aliyosema ni aibu kwangu ata kuyaweka hapa......
Ila poa tu...
"Siri ya simu hiyo ni yangu. Wewe haikuhusu kabisa.
Ulinioa sababu uliniwin kunipa mimba tu. Sikufichi mtoto ni wako ila hutakaa ujue siri za maisha yangu.
Nilishakuwin kwa mama na wazazi wako na ukirudisha mada hiyo tena ntasema we ndio umeziweka izo password. Kwa taarifa yako ata babaangu mzazi hawezi kukubali kuifungua cm hii... "
ni ujumbe wa maneno kama hayo sema sikuweza kuurekodi ila nahisi sijaukosea sana
sasa naiogopa mpaka nyumba kanitishia hadi maisha kuendelea kuzifatilia
natamani nitoroke tu
Tulianza urafiki tu kama miaka mitatu ivi wote tukiwa chuo. Kwa wakati huo alikuwa na cm nzuri aina ya samsung ila kila tukikaa nae alikuwa anaacha cm kwingine mara rafiki yangu anachati nayo facebook, mara haina chaji, mara nimeisahau na sababu nyingi tu na sikuweza ata kuigusa kwa takribani miaka miwili.
Kwa kuwa niko mwaminifu sana nilijaribu kuicha cm yangu wazi kwake. Zinaingia sms bila kujua ya nani namwambia nisomee, alikuwa akikataa lkn baadae alikubaliana na hayo. Siku nyingine najifanya kama nimeisahau kwake ili kuonesha uaminifu.
Baada ya ndoa alikuja bila cm. Alisema cm yake ilipotea siku ya harusi kwenye salóon aliyokuwa akipambwa na wamemfidia fedha taslim na haoni haja ya kununua cm kwani atakuwa anatumia yangu.
Mwezi wa sita mwaka jana nilipata safari ya kikazi nikalazimika kumnunulia cm ila tuwasiliane nae tukiwa mbali.
Cha kushangaza cm hiyo anaificha sana. Ikiita anaweza asipokee. Aniambii lolote kuhusiana na cm labda nani kapiga kasema nini ananisalimia au la kama ambavyo nafanya mimi.
Akiöngea kwenye cm mazungumzo ni ya mkato na yasiyoeleweka. Utasikia mara Sawa.... Aa.... Sina... Nimesahau..... Yupo. Au nimeelewa yani neno moja tu alafu anakata cm.
Kingine amejiunga na facebook nazani kwa jina jingine kwani yuko bize na facebook lakini kila nikimtafuta kwenye fb simpati.
Leo ndio alikuwa ameenda kujifungua kwa bahati nzuri nikabahatika kushika cm yake na kuifungua ni password kila sehemu, fonebook, sms, call log na kadhalika.
Nishaurini nifanye nini na cm ya mke wangu.
Nilifika hospital leo asubui sana saa moja kasoro. Nikamfata mke wangu kumsabai
alikuwa akisubiri ruhusa. Kwa upole nikamuuliza juu ya password. Nakumwomba anijibu ili roho itulie na nianze kufikiri juu ya mtoto pekee. Mke badala ya kunijibu akaangua kilio wodini. Ni machozi macho mekundu analia tu. Sikujua analilia nini.
Mida ya saa moja na nusu daktari wa zamu alipofika alipokuta kile kilio akaniuliza kunanini. Nikamjibu anasema dumbo linamuuma. Sasa imebidi asiruhusiwe mpaka mchana waone hali yake.
Sa analilia nini ata sijui. Na kwanini asinipe tu hiyo password mi moyo utulie .
Ma mkwe nae katimba hosptal imebidi tu kumdokeza kasema nisubiri kidogo nae kama kanishangaa iv
UP TO DATE 15th Jan 2013 20:00
Nilienda kwa fundi simu nikaambiwa angeweza kuondoa password kwa kuifrash CM Ila itafuta kila kumbukumbu yani sms zote, majina na itakuwa kama mpya nikaona nimekwama hapo. Nikaenda kwenye ofisi za tigo nikiwa na laini yake kitambulisho chake na cheti cha ndoa yetu.
Wakakataa kunipa ushirikiano wakidai mpaka nipewe idhini police. Wanadai wangewajibika kama ningepata habari ambazo zingepelekea mtu kudhurika na wanalinda uhuru wa mteja.
Nikaenda police wamesema hawezi kuunda shitaka la kijinai au la madai ambalo lingepelekea wao kunipa idhini kufatilia cm wala laini.
Kufika hospitali tayari mke wangu alikuwa karuhusiwa.
Nikafika nyumbani majira ya saa 10 jioni. Nikamkuta ma mkwe, Mama mzazi, shangazi mmoja na nikaambiwa mchungaji ba mkwe yupo njiani anakuja na kunamaongezi sebuleni.
Kabla ya mazungumzo mke wangu alitoa sara kali kukemea na kufukuza mapepo.
Mama mzazi akaanza kunilalamikia kuwa sijafurahia mtoto. Mbona sikuuliza kabla mpaka sku ya kujifungua. Sijatoa pole kwa mzazi mara cn zawadi.
Katikati ya mazungumzo mke akadakia "password ni mwaka wangu wa kuzaliwa"
Jamani aibu. Nikatoa laini ile nilikuwa nimeitoa kwenye CM YAKE na kuweka kwenye Cm yangu. Mama yangu mzazi akaja pembeni yangu. Kuweka mwaka wake tu laini ile ikafunguka. Masikini aibu....
Fonebook hakuna kitu. Hakuna sms wala nini.
Kwa aibu sikuona haja ya ya kufata cm yake kuifungua tena mbele yao. Nikaomba msamaha tukasameheana wote mama akatoa tsh 50,000 na mama mkwe hivo ivo shangazi akatoa ahadi tu. Kabla ya kufunga mazungumzo mchungaji na Baba wakafika. Wakaambiwa mi ni mtoto yameisha tukapiga sara tu.)
mh kuifata cm yake lengo nimrudishie wife mara ikaingia sms. Kuiangalia ilikuwa ni sms ya 17 toka nichukue cm. Na nikaona kuna misscall kibao.
Nikasema nizisome zote ndio nirizike...
Masikini password tulizopewa hazifungui cm hii. Nikamuuliza tena mbona cm haifunguki na hizo password.
Alivyonijibu sasa ni amazing. Ni kwa kuashiria kiburi ila maneno aliyosema ni aibu kwangu ata kuyaweka hapa......
Ila poa tu...
"Siri ya simu hiyo ni yangu. Wewe haikuhusu kabisa.
Ulinioa sababu uliniwin kunipa mimba tu. Sikufichi mtoto ni wako ila hutakaa ujue siri za maisha yangu.
Nilishakuwin kwa mama na wazazi wako na ukirudisha mada hiyo tena ntasema we ndio umeziweka izo password. Kwa taarifa yako ata babaangu mzazi hawezi kukubali kuifungua cm hii... "
ni ujumbe wa maneno kama hayo sema sikuweza kuurekodi ila nahisi sijaukosea sana
sasa naiogopa mpaka nyumba kanitishia hadi maisha kuendelea kuzifatilia
natamani nitoroke tu