Castle_Lite
JF-Expert Member
- Sep 10, 2016
- 3,533
- 6,930
Mungu akubariki katika tafakari ya mateso ya Bwana wetu Yesu Kristo siku ya Leo.
- Yesu Kristo aliikuta Pasaka.
Tunaona kwenye Biblia kuwa Mipango ya kumkamata na Kumuua ilipangwa kipind cha majirio ya Passover.
Marko 14:1-2
"1 Baada ya siku mbili ilikuwa sikukuu ya Pasaka, na mikate isiyochachwa; wakuu wa makuhani na waandishi wakatafuta njia ya kumkamata kwa hila na kumwua.
2 Kwa maana walisema, Isiwe kwa wakati wa sikukuu, isije ikatokea ghasia katika watu. "
Passover inatokana na neno la Kiebrania, Pesach. ni sikukuu muhimu sana kwa Wayahudi inayokumbuka tukio la kihistoria la ukombozi wao kutoka utumwani Misri.
Wana wa Israeli walikuwa watumwa nchini Misri, Mungu alimtuma Musa awaokoe.Baada ya mapigo 10 kwa Wamisri, Farao aliwaruhusu waondoke
Ule Usiku wa pigo la mwisho, malaika wa mauti alipita Misri, Nyumba za Waisraeli zilipakwa damu ya kondoo mlangon, Malaika “alipita juu” ya nyumba hizo (ndiyo maana Passover = kupita juu), Akaziacha . Ila alikuwa anaua Wazaliwa wa Kwanza kwenye nyumba ambazo hazina Hiyo damu ya mwana Kondoo.
Pasaka ya Wakristo ilikuja baada ya Yesu. ni sikukuu inayoadhimisha kufufuka kwa Yesu Kristo baada ya kusulubiwa.
Yesu alisulubiwa siku ya Ijumaa, Alizikwa kaburin na Baada ya siku tatu (Jumapili),alifufuka kutoka kwa wafu.
Wakristo Duniani Kote wanasherehekea Pasaka na sio Passover. Na kipind hiki kiliongezewa na zile siku 40 alizofunga Yesu akiwa Jagwani.
Kwenye siku hizi 40 za Maandalizi kabla ya Pasaka. Wakristo hufunga na kujizuia baadhi ya vitu vya Anasa na starehe nyingne.
Kwanini Nyama Hailiwi siku ya Ijumaa?.
Nyama ilichukuliwa kama chakula cha anasa huko zamani na Kuacha kula nyama ni ishara ya unyenyekevu kwa Wakristo. kujinyima na kuonyesha mshikamano na mateso yake Bwana wetu Yesu Kristo aliyokutana nayo siku ya Ijumaa.
Madhehebu Mengne kama Wakatoliki Huruhusu samaki kwa madai kuwa sio Nyama ya Kuchinja wakisanikisha na tukio lile la Kuchinja mwana Kondoo kwenye siku ya Passover (nchini Misri).
Nikutakie tafakari njema ya siku ya Ijumaa Kuu.
- Yesu Kristo aliikuta Pasaka.
Tunaona kwenye Biblia kuwa Mipango ya kumkamata na Kumuua ilipangwa kipind cha majirio ya Passover.
Marko 14:1-2
"1 Baada ya siku mbili ilikuwa sikukuu ya Pasaka, na mikate isiyochachwa; wakuu wa makuhani na waandishi wakatafuta njia ya kumkamata kwa hila na kumwua.
2 Kwa maana walisema, Isiwe kwa wakati wa sikukuu, isije ikatokea ghasia katika watu. "
Passover inatokana na neno la Kiebrania, Pesach. ni sikukuu muhimu sana kwa Wayahudi inayokumbuka tukio la kihistoria la ukombozi wao kutoka utumwani Misri.
Wana wa Israeli walikuwa watumwa nchini Misri, Mungu alimtuma Musa awaokoe.Baada ya mapigo 10 kwa Wamisri, Farao aliwaruhusu waondoke
Ule Usiku wa pigo la mwisho, malaika wa mauti alipita Misri, Nyumba za Waisraeli zilipakwa damu ya kondoo mlangon, Malaika “alipita juu” ya nyumba hizo (ndiyo maana Passover = kupita juu), Akaziacha . Ila alikuwa anaua Wazaliwa wa Kwanza kwenye nyumba ambazo hazina Hiyo damu ya mwana Kondoo.
Pasaka ya Wakristo ilikuja baada ya Yesu. ni sikukuu inayoadhimisha kufufuka kwa Yesu Kristo baada ya kusulubiwa.
Yesu alisulubiwa siku ya Ijumaa, Alizikwa kaburin na Baada ya siku tatu (Jumapili),alifufuka kutoka kwa wafu.
Wakristo Duniani Kote wanasherehekea Pasaka na sio Passover. Na kipind hiki kiliongezewa na zile siku 40 alizofunga Yesu akiwa Jagwani.
Kwenye siku hizi 40 za Maandalizi kabla ya Pasaka. Wakristo hufunga na kujizuia baadhi ya vitu vya Anasa na starehe nyingne.
Kwanini Nyama Hailiwi siku ya Ijumaa?.
Nyama ilichukuliwa kama chakula cha anasa huko zamani na Kuacha kula nyama ni ishara ya unyenyekevu kwa Wakristo. kujinyima na kuonyesha mshikamano na mateso yake Bwana wetu Yesu Kristo aliyokutana nayo siku ya Ijumaa.
Madhehebu Mengne kama Wakatoliki Huruhusu samaki kwa madai kuwa sio Nyama ya Kuchinja wakisanikisha na tukio lile la Kuchinja mwana Kondoo kwenye siku ya Passover (nchini Misri).
Nikutakie tafakari njema ya siku ya Ijumaa Kuu.