Pasco Tuombe radhi CHADEMA-Umemwelewa Vibaya Hon Mbowe

Status
Not open for further replies.
Kikwete hakuanzisha mchakato wa katiba kama mwenyekiti wa CCM, bali alianzisha kama raisi, hivyo alipaswa kupongezwa kama raisi. CDM wameshasema siku zote wanaheshimu sheria zilizopo zinazomtambua Kikwete kuwa raisi. Hata hivyo wanapinga uhalali wa sheria hizo, hence uhalali wa raisi.

Heshima kwako Tuko,

Mwenyekiti wa CCM na Rais wa JMT Jakaya Mrisho kikwete aliongoza kikao cha CC na kuafiki Dowwans ilipwe.Mwenyekiti wa CCM na Rais wa JMT aliongoza kikao cha wabunge wa CCM na kuamuru malipo ya Dowans yasilipwe.Mwenyekiti wa CCM na Rais wa JMT kwenye sherehe za kutimiza miaka 34 hairuka Dowans asema hawajui wala hana hisa pia hajawahi kukutana nao.

Mifano yote mitatu inamzungumzia mtu mmoja mwenye kofia mbili ,Kikwete ni rais na ni mwenyekiti wa CCM .Mtu huyu Kikwete anaweza kutambulishwa kwa kofia mojawapo kutegemea na shughuli anayoifanya inaegemea wapi lakini bado hawezi kuikana au kuidharau kofia nyingine.

Mheshimiwa Rais Kikwete na Mwenyekiti wa CCM alipohutubia sherehe za miaka 34 Dodoma kofia ya uenyekiti wa CCM ilikuwa ikitajwa zaid kuliko Rais wa JMT kwakuwa alikuwa kwenye sherehe zinazowahusu CCM zaidi.Tunaweza kusema alikuwa kichama zaidi.Mheshimiwa Rais Kikwete anapompokea mgeni eg balozi wa nchi nyingine anakuwa kiserekali ziadi hivyo kofia ya Urais inachukua nafasi yake.

Mheshimiwa Freeman Mbowe alikuwa katika nafasi nzuri sana kumpongeza Kikwete kama Mwenyekiti wa CCM kwa kukubali kuandaa mchakato wa mabadiliko ya katiba ingawa CCM hawakuliweka kwenye ilani yao ya uchaguzi.Ipo point moja muhimu sana hapa CHADEMA waliweka kwenye ilani yao mchakato wa kubadili katiba.

[1] CCM wamechukua baadhi ya mambo mazuri kutoka CHADEMA.

[2] CCM haiwezi kufanya hivyo bila ridhaa ya mwenyekiti wake ambae ni Kikwete,sasa kulikuwa na shida gani KUB kumaddress kama Mwenyekiti.

[3] Kwakuwa CHADEMA hawamtambui Kikwete kama Rais wa JMT,je ipo kanuni ya bunge inayowalazimisha kumaddress kikwete kama Rais ?.kama haipo ni kwanini CHADEMA wanatuzuga kwamba hawamtabui ?.

[4] Ifike mahali CHADEMA iache kuzungusha zungusha watuambie ukweli bila kificho wakifanya hivyo watakuwa huru.Hawatakuwa na sababu za kutoa maelezo kitendo cha mwenyekiti wao kupeana mikono na Rais Kikwete na tabasamu la nguvu.
 
Habari za jioni waheshimiwa,

Nimesoma thread mbili moja ililetwa awali na ndugu Pasco ikielezea kilichojiri Bungeni na ya pili ilikuwa kukanusha yale aliyoyasema Pasco na kumtaka aombe radhi thread ya kumtaka Pasco aombe radhi imeletwa na Mheshimiwa Regia Mtema. Naomba ninukuu ujumbe wa thread hizo kisha tuangalie nini amekosea Pasco? na je anastahili kuomba radhi?
Watch TBC Live toka Bungeni!
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amekubali yaishe, wanamtambua JK kama Rais, Wanampongeza!
Mbowe ameomba reconciliation for the sake of Umoja wa Kitaifa.

Big Up kwa Freeman Mbowe, sio siri mimi binafsi nilikuwa simuheshimu sana Mbowe nikimuona kama spoon fed leader.
Kuanzia sasa ni heshima mbele! Huo ndio uanamume, kukubali kushindwa na kukubali yaishe!

Mbowe amewashukuru wapiga kura kwa kura walizoipigia Chadema!.

Hiki Mbowe alichokifanya Bungeni, ndicho Dr. Slaa alichotakiwa kukifanya ile siku ya kutangazwa matokeo!

Nilisema that was a golden missed opportunity. Sasa Mbowe amerekebisha makosa ya Dr. Slaa. Chadema sasa inarudi juu!

Kuna posti niliwahi kuiposti kuwa Chadema hawajajipanga, nilishambuliwa piga ua. Sasa nasema Chadema imeanza kujipanga. Big up!.

Kwanza mlibanaaa... mwisho mmeachia... I'm glad I was damm right!

Chadema sasa tusonge mbele, hata mimi nikirudi uraiani, naweza kufikiria kujiunga Chadema, kuimarisha nguvu!

Asante sana Freeman Mbowe!.

Update 1: Angalizo!.
Kuna kitu kinaitwa expressly na impliedly!
Expressly ni kwa Mbowe kutangaza kwamba sasa Chadema inamtambua Rais!
Impliedly ni pale Mbowe alipompongeza rais, akamsifu, akamshukuru na bla bla bla nyingi za kusifu na kutukuza na kuonyesha spirit ya reconciliation.

mkubali msikubali, Chadema imemtambua Rais JK impliedly na wamekubali yaishe zaidi ya hapo ni ubishi tuu, vinginevyo Mbowe afanya Press Conference afafanue na kukazia kutomtambua JK!

Pasco.

attachment.php

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...li-yaishe-yamtambua-rais-yampongeza-rais.html

Regia akamjibu kama ifuatavyo..................



Mkuu Pasco.Heshima mbele.

Nimeamua kuanzisha thread hii kwa makusudi kabisa ila kuondoa upotoshaji ambao umeufanya hasa kwa wale ambao hawajatazama Bunge. Kuna watu wengi tu hawajatazama Bunge na hawatapata muda wa kutazama hivyo ukisema kuwa CHADEMA tumekubali yaishe na kumtambua Rais si kweli. Kwanza napenda ieleweke kuwa kumpongeza mtu ni tamaduni ya kawaida kabisa na pale mtu anapostahili pongezi basi hana budi kupongezwa.

Alichokisema Mbowe ni kumpongeza Rais kwa kukubali kuandaa Mchakato wa Mabadiliko ya Katiba Mpya pamoja na kwamba suala hili halikuwa kwenye ilani ya Chama Cha Mapinduzi(CCM). Hayo mengine ya kumtambua hajasema. Kuongeza ni suala la kawaida sana. Na amesisitiza kuwa atapongeza kila zuri litakapofanywa iwe kwa chama au kwa serikali. Hansard ikitoka nitaweka hapa.

Naomba uiondoe thread yako. Ili usipotoshe na wengine pia.

Kutoka Mjengoni
Aluta Continua.

Kisha Regia akasema..........................

Ki ukweli Bunge limeniboa hasa..Yaani kipindi cha maswali kikiisha sijisikii tena kusikiliza mipasho na vijembe vyao.Jumatatu ifike haraka tumalize kuchangia hii hotuba ya Rais inayotupa nafasi ya kuogeleoa popte unapotaka.

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...adhi-chadema-umemwelewa-vibaya-hon-mbowe.html



My take,

Ukisoma vizuri utaona alichokisema Pasco ndicho alichokisema Regia haya ni mawazo yangu naomba nililete kwenu Magreat Thinkers wa ukweli mlichambua mwenye haki yake mumpe!

Shukran.
 
Mkuu Ngongo,
kama hukupata kusoma haya na kama hutokuwa mvivu naomba ugonge hapa

Heshima kwako Crashwise,

Mkuu nimesoma gazeti la Tanzania Daima ingawa silipendi kwasababu halina tofauti na gazeti la Uhuru linapokuja suala la CCM.Mwanahabari samsoni Mwigamba si mwandishi wa habari huru yuko tayari kusema jambo lolote hata ikiwa ni kupindisha hoja ili kumfurahisha bosi wake mheshimiwa F Mbowe.
 
Kaka usilazimishe mambo, sijakuelewa unataka kufikisha ujumbe gani -1+1=0. walichosungumza hawa watu wawili havifanani kabisa
 
Mimi sifurahii bunge hili kabisa maana nasikia kila mbunge kupongeza tu kupongeza baba, kupongeza mama, kupongeza spika mwanamke, kupongeza rahisi, kupongeza wapiga kura, kupongeza hadi lini jamani?

Mmoja wa kike kasema tunapaswa kupongeza serikali ya CCM kwa kuleta maendeleo hadi demand ya umeme ikawa kubwa zaidi ya supply. Halafu ujinga huu unashangiliwa kwa kugonga meza.

Mimi simo
 
Ifike wakati mfanye kama hivi pale mnapoona upotoshwaji unafanyika kwa vyama vingine hii itawasaidia kuonekana mnasimamia haki na nidhamu ya JF. Siku zote huwa nasisitiza umuhimu wa kuheshimiana na kutokuzuliana maneno. Jana kina HR na Kafulila walizuliwa kuwa wameangushwa kwenye kugombea uenyekiti wa PAC na POC, Sijakusikia wewe Regina wana Mkumbo kuwarekebisha watu na kuwaeleza ikweli mlinyamaza kimya. Ila mkiguswa nyie mtaanzisha thread za kuomba msamehewe. Uungwana ni kufanya yasio wachukiza wengine sio kuacha kufanywa yanayokuchukiza wewe tu.

Ahibal nasi matuhibul nafsik penda nafsi ya mwenzako kama unavyoipenda nafsi yako.


Shukran.

Heshima kwako MS,

Mkuu maneno mazito sana.
 
Kaka usilazimishe mambo, sijakuelewa unataka kufikisha ujumbe gani -1+1=0. walichosungumza hawa watu wawili havifanani kabisa

Ohh okay kivipi labda unaweza kuelezea? mfano Pasco ametumia neno "Impliedly na Expressly" je umemwelewa kwenye hayo maneno?
 
Heshima kwako Jmushi1.

Mkuu tuko pamoja KUB mheshimiwa F Mbowe alitakiwa ampongeze JK kama mwenyekiti wa CCM na akwepe kabisa kutaja cheo cha rais ningekuwa mtu wa kwanza kumshikia bango Pasco lakini kwa hili hastahili kabisa kuomba radhi.
Hawezi kukwepa kutaja jina la rais kwasababu ni rais kwa mujibu wa sheria na katiba yetu kuukuu, hilo alishalisema, na si raisi wa kuchaguliwa na umma wa waTZ.
 
Mkuu Pasco.Heshima mbele.

Nimeamua kuanzisha thread hii kwa makusudi kabisa ila kuondoa upotoshaji ambao umeufanya hasa kwa wale ambao hawajatazama Bunge. Kuna watu wengi tu hawajatazama Bunge na hawatapata muda wa kutazama hivyo ukisema kuwa CHADEMA tumekubali yaishe na kumtambua Rais si kweli. Kwanza napenda ieleweke kuwa kumpongeza mtu ni tamaduni ya kawaida kabisa na pale mtu anapostahili pongezi basi hana budi kupongezwa.

Alichokisema Mbowe ni kumpongeza Rais kwa kukubali kuandaa Mchakato wa Mabadiliko ya Katiba Mpya pamoja na kwamba suala hili halikuwa kwenye ilani ya Chama Cha Mapinduzi(CCM). Hayo mengine ya kumtambua hajasema. Kuongeza ni suala la kawaida sana. Na amesisitiza kuwa atapongeza kila zuri litakapofanywa iwe kwa chama au kwa serikali. Hansard ikitoka nitaweka hapa.

Naomba uiondoe thread yako. Ili usipotoshe na wengine pia.

Kutoka Mjengoni
Aluta Continua.
Tukubali mh. Mbowe hapa kateleza; hapakuwepo sababu yeyote ya kumumwagia sifa JK kwa hili suala la kuridhia mchakato wa katiba, kwasababu hakufanya hivyo kwa nia njema, bali kwa lengo la kuteka nyara mchakato huo. Aidha kama kiongozi wa kambi ya upinzani, wengi wetu tulitegemea alaani hiki kitendo cha bunge letu kupoteza muda mwingi kuzungumzia hotuba ya rais badala ya kushughulikia matatizo chungu nzima yanayo kabili nchi yetu/
 
Ohh okay kivipi labda unaweza kuelezea? mfano Pasco ametumia neno "Impliedly na Expressly" je umemwelewa kwenye hayo maneno?
Impliedly, ni kwamba Mkubwa Pasco anajaribu kuelezea kutokana na hisia zake na hajasimama kwenye kitu halisi ila anajaribu kulazimisha tafsiri kwa interest zake
 
Impliedly, ni kwamba Mkubwa Pasco anajaribu kuelezea kutokana na hisia zake na hajasimama kwenye kitu halisi ila anajaribu kulazimisha tafsiri kwa interest zake

Kama Mbowe kampongeza Rais kama anavyosema Regia basi ndio mwanzo mwema wa yale aliyoyatabiri Pasco........
 
MS... pitia thread ya pasco ...soma post moja baada ya nyingine... utaona jinsi alivyo edit na kuirembesha kwa picha thread yake kutokana na kuteleza kwa makusudi...itakusaidia kwani naona unapata shida sana kumtetea pasco bila hoja ...wakati yeye mwenyewe baada ya kuchangia akaingia mitini jumla ... na akaanza kutoa thanks kwa wote waliomchallenge
 
Hapaswi Mtu kutumia muda wake katika mambo ya kipuuzi, Muungwana ni Mtu ambae anatakiwa kuchunga muda wake na kuutumia katika mambo ya kheri tu.
 
Tatizo lako wewe Mohammed Shossi unajiona ni Great Thinker kuliko wote humu JF. Ajikwezae hushushwa...
 
Hapaswi Mtu kutumia muda wake katika mambo ya kipuuzi, Muungwana ni Mtu ambae anatakiwa kuchunga muda wake na kuutumia katika mambo ya kheri tu.

Nadhani kumtambua Rais na kuchangia hotuba yake si jambo la kipuuzi Mchungaji, hizi ni chnagamoto tu bahati nzuri mie sina chama nipo huru na na enjoy kuwa huru, hawa walio walk out kwenye hotuba ya "Rais" leo wanachangia hotuba ya "Rais" siku zote nawaambia siasa maigizo refer CUF Zanzibar na yaliyojiri kwenye kura za kamati za Bunge! Hivi lini tutazinduka!
 
Mgosi onga uwedi?

Sijifanyi great thinker nilichokiona mimi pengine sijakielewa ndio maana nimeileta kwenu hoja hii....

siijui hiyo lugha uliyoanza nayo kama ni tusi likurudie. Kwa kifupi ni kuwa nimepitia kwa makini mabishano yako kwenye thread ya Mh. Regia Mtema hivyo ndivyo ulivyo hata kwenye thread nyingine nyingi pia. Umejiweka nafasi ya Great Thinker bora kuliko wote hapa JF. Nini umuhimu wa thread yako hii?
 
Ndugu Shossi

asante ka jicho la 3. Regia (msemaji wa Chadema? au katumwa? au kakurupuka kama kawaida ya wanachadema?) hajui anachomaanisha, anapindua maneno kupindisha ukweli na hali halisi.

Pamoja na vioja na vituko vya kutaka kulazimisha kutambua Urais na kumratambua Rais, ni kichekesho.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom