Pape Ousmane Sakho (POS) usilewe mafanikio ya kiatu cha goli bora, bado una safari ndefu

Tipstipstor

JF-Expert Member
Nov 29, 2021
1,531
3,331
Ahlanbik kutoka Lombardia ndani ya jiji la Bergamo kaskazini mwa nchi ya Italy:

Jana nlifanikiwa kuitazama mechi ya miamba ya soka nchini Tanzania ,Simba dhidi ya timu ya Geita Gold nikiwa hapa Italy kupitia Azam max, niseme tu pongezi ziwaendee Azam kwa kutuwezesha diasporas tulioko huku ughaibuni kuweza kuburudika na soka la nyumbani kwetu Tanzania. Ukiacha kuwa mshabiki mkubwa wa timu kubwa ya hapa jijini kwetu Bergamo, Atalanta Bergamasca Calcio (Atalanta B.C), bado nimeendelea kuwa mshabiki kindakindaki (die hard fan) wa Simba Sc. Naamini simba ina potential ya kuja kuwa timu kubwa kabisa Africa na duniani kwa ujumla.

Katika kuicheki hii mechi ya simba dhidi ya geita gold, nimegundua jambo moja kumhusu bwana mdogo Sakho, raia kutoka Senegal. Sakho ni mchezaji mzuri na ikiwa atatuliza akili na kuwekeza juhudi uwanjani basi anauwezo wa kufika mbali sana. Ila nilichokiona toka mwisho wa msimu uliopita ni kuwa bwana mdogo huyu ameanza kulewa sifa , simuoni yule Sakho aliyekuwa na uchu kutokea timu ya teungueth ya pale Senegal.

Sakho siku hizi amekuwa haeleweki anachokicheza uwanjani, amekuwa anajali zaidi kelele za wakaanga chips jukwaani (mashabiki) wanavyomshangilia pale anavyopigapiga chenga huku akisahau majukumu yake kiwanjani. Kwa wanaomfahamu kocha Zoran Maki wanajua kuwa huwa hana ujamaa na mchezaji yeyote hata kama unasifiwa au kukubalika na mashabiki.Mtakuwa mashahidi pale alipomtoa Jonas Mkude kabla ya hata kuisha kipindi cha kwanza. Zoran hahitaji mbwembwe nyingi kiwanjani.Falsafa yale inahitaji mchezaji awe na kasi akiwa na mpira au hana mpira, pia kucheza direct football basi.

Kwa sakho ,mafanikio ya kupewa tuzo ya goli bora yameanza kumdanganya na kujiona kuwa ameshakuwa mchezaji mwenye uhakika wa namba pale simba, nimwambie tu kuwa kwa kocha huyu hakuna mwenye uhakika wa namba pale simba , ukimzingua tu anakuzingua.Game kadhaa sasa zinlmepita sioni successful dribbles (take-ons) kutoka kwa sakho, sioni assists na kiwango chake cha complete passes kimeshuka pia. Anaingiza mambo mengi kwenye aspect of his game badala ya kucheza basic football tu. Akumbuke kuwa benchi la simba lina wachezaji wengi wazuri kama kina Okwa ambao wanafanya juu chini kumshawishi kocha ili wawe sehemu ya first eleven. Waliokaribu na kijana Sakho wamwambie tu kuwa abadilike aache ubinafsi wa mafanikio yake binafsi na badala yake acheze kwa ajili ya timu. Pia apunguze kila muda kutaka kuwa na mpira kitendo kinachomfanya kushuka sana chini kuja kufata mpira na kuanza kupiga chenga kijiji cha wachezaji wa timu pinzani. Atulie juu eneo la umbali wa 40yard kutoka katika goli la timu pinzani ili mipira imfate yeye na si kazi yake kuja kuifuata mipira nyuma.
 
Ahlanbik kutoka Lombardia ndani ya jiji la Bergamo kaskazini mwa nchi ya Italy:

Jana nlifanikiwa kuitazama mechi ya miamba ya soka nchini Tanzania ,Simba dhidi ya timu ya Geita Gold nikiwa hapa Italy kupitia Azam max, niseme tu pongezi ziwaendee Azam kwa kutuwezesha diasporas tulioko huku ughaibuni kuweza kuburudika na soka la nyumbani kwetu Tanzania. Ukiacha kuwa mshabiki mkubwa wa timu kubwa ya hapa jijini kwetu Bergamo, Atalanta Bergamasca Calcio (Atalanta B.C), bado nimeendelea kuwa mshabiki kindakindaki (die hard fan) wa Simba Sc. Naamini simba ina potential ya kuja kuwa timu kubwa kabisa Africa na duniani kwa ujumla.

Katika kuicheki hii mechi ya simba dhidi ya geita gold, nimegundua jambo moja kumhusu bwana mdogo Sakho, raia kutoka Senegal. Sakho ni mchezaji mzuri na ikiwa atatuliza akili na kuwekeza juhudi uwanjani basi anauwezo wa kufika mbali sana. Ila nilichokiona toka mwisho wa msimu uliopita ni kuwa bwana mdogo huyu ameanza kulewa sifa , simuoni yule Sakho aliyekuwa na uchu kutokea timu ya teungueth ya pale Senegal.

Sakho siku hizi amekuwa haeleweki anachokicheza uwanjani, amekuwa anajali zaidi kelele za wakaanga chips jukwaani (mashabiki) wanavyomshangilia pale anavyopigapiga chenga huku akisahau majukumu yake kiwanjani. Kwa wanaomfahamu kocha Zoran Maki wanajua kuwa huwa hana ujamaa na mchezaji yeyote hata kama unasifiwa au kukubalika na mashabiki.Mtakuwa mashahidi pale alipomtoa Jonas Mkude kabla ya hata kuisha kipindi cha kwanza. Zoran hahitaji mbwembwe nyingi kiwanjani.Falsafa yale inahitaji mchezaji awe na kasi akiwa na mpira au hana mpira, pia kucheza direct football basi.

Kwa sakho ,mafanikio ya kupewa tuzo ya goli bora yameanza kumdanganya na kujiona kuwa ameshakuwa mchezaji mwenye uhakika wa namba pale simba, nimwambie tu kuwa kwa kocha huyu hakuna mwenye uhakika wa namba pale simba , ukimzingua tu anakuzingua.Game kadhaa sasa zinlmepita sioni successful dribbles (take-ons) kutoka kwa sakho, sioni assists na kiwango chake cha complete passes kimeshuka pia. Anaingiza mambo mengi kwenye aspect of his game badala ya kucheza basic football tu. Akumbuke kuwa benchi la simba lina wachezaji wengi wazuri kama kina Okwa ambao wanafanya juu chini kumshawishi kocha ili wawe sehemu ya first eleven. Waliokaribu na kijana Sakho wamwambie tu kuwa abadilike aache ubinafsi wa mafanikio yake binafsi na badala yake acheze kwa ajili ya timu. Pia apunguze kila muda kutaka kuwa na mpira kitendo kinachomfanya kushuka sana chini kuja kufata mpira na kuanza kupiga chenga kijiji cha wachezaji wa timu pinzani. Atulie juu eneo la umbali wa 40yard kutoka katika goli la timu pinzani ili mipira imfate yeye na si kazi yake kuja kuifuata mipira nyuma.
Vipi manzese mvua inanyesha?
 
Hakuna asiyekubali uwezo mkubwa wa Sakho hasa ule ujasiri wa kukokota mpira na kuwafuata mabeki uso kwa macho ambao washambuliaji wengi duniani hawana. Lakini ni wakati sasa wa benchi la ufundi la Simba kusimama imara kwa manufaa ya timu nzima na kumwelekeza Sakho aache kucheza kwa manufaa yake binafsi badala yake acheze kwa manufaa ya timu nzima. Lakini kila siku anapopiga chenga zisizo na faida kwa timu halafu mashabiki hoya hoya wanapomshangalia jukwaani halafu benchi la ufundi nalo lipo kimya hakuna mtu mmoja kwenye benchi la makocha anayesimama na kumkemea kijana ndio anazidi kuharibu na kuigharimu timu. Mbaya zaidi kila siku utamkuta kwenye "first eleven" maana yake benchi la ufundi linaridhika na upuuzi anaoufanya uwanjani.

Mfano mzuri mechi ya jana mwenzake Okrah katumia muda mfupi sana kuisaidia Simba kuweza kupata ushindi kwa sababu ya kucheza kwa malengo na manufaa ya timu matokeo yake kafunga goli na kusababisha penalti. Wakati yeye Sakho katumia muda mwingi uwanjani kwa:-
1. Kutaka kufunga mwenyewe"badala ya kutoa "assist" kwa wenzake hata akiwa "impossible angle"
2. Kupiga chenga zisizo na faida.
3. Kupoteza mipira mingi sana pasipo na sababu za msingi
4. Muda mwingi alikuwaa anakaa na mpira miguuni kwake badala ya kuipeleka timu haraka mbele kabla Geita hawajajipanga
5. Muda mwingi alikuwa anashuka chini na kumuacha Phiri yupo "isolated" matokeo yake hata zile "second ball" bado Geita walikuwa wanazichukua kirahisi.
6. Alikuwa analzimisha kupiga kona amabzo zilikuwa hazifiki vizuri golini wakati Simba ina watu warefu Kanoute na Outara.

Kwa ufupi benchi la ufundi la Simba liache kumlea Sakho maana ipo siku atawagharimu tu.

Ni mtizamo tu.
 
Sakho ni mpumbavu.
Kwanza ni mbinafsi,pili akipoteza mpira hakabi.

Bora Hata Kibu D
 
Sakho ni homa ya vipindi... Atakufurahisha mechi moja, mechi 5 atacheza utumbo... Na tena ndio hivo ameshauza nyago kwenye kideo duniani kazi ipo...

Alianza kupata umaarafu hasa wakati wa kombe la Mapinduzi... Toka hapo ameshakuwa 'fadha'....
 
Kama kuna mchezaji ambae hatakiwi kukaa benchi Simba basi ni Okrah ni vile tu huyu mwalimu ana mawenge yule hatakiwi kukaa benchi kabisa ni mchezaji mwenye faida sana uwanjani.
 
Umesema mara mbili kwenye UZI wako kwamba upo Italy maana yake kwa mwenye akili anajua kabsa upo KAWE.

Unadanganya kwa manufaa ya nani POPOMA?
 
Jana kanikera saana Sakho. Kocha pia aliendelea kuzingua kwenye Sub zake. Anatoa mchezaji ambae gem limemkubali anaacha Sakho ambae akuwa lolote
 
Back
Top Bottom